1At that time, Herod the tetrarch heard the report concerning Jesus,
1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
2and said to his servants, “This is John the Baptizer. He is risen from the dead. That is why these powers work in him.”
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
3For Herod had laid hold of John, and bound him, and put him in prison for the sake of Herodias, his brother Philip’s wife.
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
4For John said to him, “It is not lawful for you to have her.”
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
5When he would have put him to death, he feared the multitude, because they counted him as a prophet.
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
6But when Herod’s birthday came, the daughter of Herodias danced among them and pleased Herod.
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
7Whereupon he promised with an oath to give her whatever she should ask.
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
8She, being prompted by her mother, said, “Give me here on a platter the head of John the Baptizer.”
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
9The king was grieved, but for the sake of his oaths, and of those who sat at the table with him, he commanded it to be given,
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
10and he sent and beheaded John in the prison.
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
11His head was brought on a platter, and given to the young lady: and she brought it to her mother.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
12His disciples came, and took the body, and buried it; and they went and told Jesus.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
13Now when Jesus heard this, he withdrew from there in a boat, to a deserted place apart. When the multitudes heard it, they followed him on foot from the cities.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
14Jesus went out, and he saw a great multitude. He had compassion on them, and healed their sick.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
15When evening had come, his disciples came to him, saying, “This place is deserted, and the hour is already late. Send the multitudes away, that they may go into the villages, and buy themselves food.”
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
16But Jesus said to them, “They don’t need to go away. You give them something to eat.”
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
17They told him, “We only have here five loaves and two fish.”
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
18He said, “Bring them here to me.”
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
19He commanded the multitudes to sit down on the grass; and he took the five loaves and the two fish, and looking up to heaven, he blessed, broke and gave the loaves to the disciples, and the disciples gave to the multitudes.
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
20They all ate, and were filled. They took up twelve baskets full of that which remained left over from the broken pieces.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21Those who ate were about five thousand men, besides women and children.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22Immediately Jesus made the disciples get into the boat, and to go ahead of him to the other side, while he sent the multitudes away.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
23After he had sent the multitudes away, he went up into the mountain by himself to pray. When evening had come, he was there alone.
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
24But the boat was now in the middle of the sea, distressed by the waves, for the wind was contrary.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
25In the fourth watch of the night, The night was equally divided into four watches, so the fourth watch is approximately 3:00 A. M. to sunrise. Jesus came to them, walking on the sea. see Job 9:8
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
26When the disciples saw him walking on the sea, they were troubled, saying, “It’s a ghost!” and they cried out for fear.
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
27But immediately Jesus spoke to them, saying “Cheer up! It is I! or, I AM! Don’t be afraid.”
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
28Peter answered him and said, “Lord, if it is you, command me to come to you on the waters.”
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
29He said, “Come!” Peter stepped down from the boat, and walked on the waters to come to Jesus.
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
30But when he saw that the wind was strong, he was afraid, and beginning to sink, he cried out, saying, “Lord, save me!”
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
31Immediately Jesus stretched out his hand, took hold of him, and said to him, “You of little faith, why did you doubt?”
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
32When they got up into the boat, the wind ceased.
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
33Those who were in the boat came and worshiped him, saying, “You are truly the Son of God!”
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
34When they had crossed over, they came to the land of Gennesaret.
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
35When the people of that place recognized him, they sent into all that surrounding region, and brought to him all who were sick,
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
36and they begged him that they might just touch the fringe or, tassel of his garment. As many as touched it were made whole.
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.