1问安
1Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2写信给在哥林多 神的教会,就是在基督耶稣里已经被分别为圣,蒙召为圣徒的人,和所有在各地呼求我们主耶稣基督的名的人。基督是他们的主,也是我们的主。
2tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3愿恩惠平安从我们的父 神和主耶稣基督临到你们。
3Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4为信徒感谢 神我因着 神在基督耶稣里赐给你们的恩典,常常为你们感谢我的 神,
4Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5因为你们在他里面凡事都富足,很有口才,知识丰富,
5Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6就如我们为基督所作的见证在你们中间得到坚立一样,
6kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7以致你们在恩赐上一无所缺,殷切盼望着我们主耶稣基督的显现;
7hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8他也必坚定你们到底,使你们在我们主耶稣基督的日子无可指摘。
8Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 神是信实的,他呼召了你们,是要你们与他的儿子我们主耶稣基督连合在一起。
9Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10基督是分开的吗?弟兄们,我凭着我们主耶稣基督的名,劝你们大家要同心,在你们中间不要分党,只要在同一的心思、同一的意念上团结起来。
10Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11我的弟兄们,革来氏家里的人向我提到你们,说你们中间有纷争。
11Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12我的意思就是,你们各人说,我是保罗派的,我是亚波罗派的,我是矶法派的,我是基督派的。
12Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, "Mimi ni wa Paulo," mwingine: "Mimi ni wa Apolo," mwingine: "Mimi ni wa Kefa," na mwingine: "Mimi ni wa Kristo,".
13基督是分开的吗?保罗为你们钉了十字架吗?你们受洗是归入保罗的名下吗?
13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14我感谢 神,除了基利司布和该犹以外,我没有给你们任何人施过洗,
14Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15所以你们没有人可以说是受洗归入我名下的。
15Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16我也给司提反一家的人施过洗;此外,有没有给别人施过洗,我就不记得了。
16(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17基督差遣我,不是要我去施洗,而是去传福音;不是靠着智慧的言论去传,免得基督的十字架失去了效力。
17Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18基督是 神的能力和智慧因为十字架的道理,对走向灭亡的人来说是愚笨的,但对我们这些得救的人,却是 神的大能。
18Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19因为经上记着说:“我要灭绝智慧人的智慧,废弃聪明人的聪明。”
19Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali."
20智慧人在哪里?经学家在哪里?今世的辩士在哪里? 神不是使属世的智慧变成了愚笨吗?
20Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
21因为在 神的智慧里,世人凭自己的智慧,既然不能认识 神, 神就乐意借着所传的愚笨的道理,去拯救那些信的人。
21Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22犹太人要求神迹,希腊人寻找智慧,
22Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23我们却传扬钉十字架的基督;在犹太人看来是绊脚石,在外族人看来是愚笨的,
23lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24但对那些蒙召的人,不论是犹太人或希腊人,基督是 神的能力, 神的智慧。
24lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25因为 神的愚笨总比人智慧, 神的软弱总比人刚强。
25Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26弟兄们,你们想想,你们这些蒙召的,按人来看有智慧的不多,有权势的不多,出身尊贵的也不多。
26Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27但是 神却拣选了世上愚笨的,使那些有智慧的羞愧。他也拣选了世上软弱的,使那些刚强的羞愧。
27Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28他也拣选了世上卑贱的和被人轻视的,以及算不得什么的,为了要废弃那些自以为是的,
28Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29使所有的人在 神面前都不能自夸。
29Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30你们因着 神得以在基督耶稣里,他使基督成了我们的智慧;就是公义、圣洁和救赎,
30Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31正如经上所说的:“夸口的应当靠着主夸口。”
31Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana."