聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Romans

16

1推荐非比
1Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2请你们在主里用合乎圣徒身分的态度去接待她。无论她在什么事上有需要,请你们都帮助她;因为她曾经帮助许多人,也帮助了我。
2Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia.
3保罗问候众圣徒问候在基督耶稣里与我同工的百基拉和亚居拉;
3Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu.
4他们为了我的性命,置生死于度外,不但我感激他们,连外族的众教会也感激他们。
4Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine.
5也问候他们家里的教会。问候我亲爱的以拜尼妥,他是亚西亚省第一个归入基督的人。
5Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni kwa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo.
6问候马利亚,她为你们多多劳苦。
6Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7问候曾经与我一同被囚的亲族安多尼古和犹尼亚;他们在使徒中是有名望的,也比我先在基督里。
7Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi.
8问候在主里我亲爱的暗伯利。
8Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana.
9问候在基督里与我们同工的珥巴努和我亲爱的士达古。
9Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku.
10问候在基督里蒙称许的亚比利。问候亚里斯多博家里的人。
10Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11问候我的亲族希罗天。问候拿其舒家中在主里的人。
11Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana.
12问候在主里劳苦的土非拿和土富撒。问候亲爱的彼息;她在主里多多劳苦。
12Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana.
13问候在主里蒙拣选的鲁孚和他的母亲;她也是我在主里的母亲。
13Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia.
14问候亚逊其都、弗勒干、赫米、百罗巴、赫马,以及和他们在一起的弟兄们。
14Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15问候非罗罗哥和犹利亚,尼利亚与他的姊妹和阿林巴,以及同他们在一起的众圣徒。
15Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olumpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao.
16你们要用圣洁的亲嘴彼此问安。基督的众教会都问候你们。
16Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
17提防背道的人弟兄们,我劝你们要提防那些离间你们、绊倒你们、使你们违反你们所学的教义的人。你们也要避开他们,
17Ndugu zangu, nawasihi muwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao,
18因为这样的人不服事我们的主基督,只服事自己的肚腹,用花言巧语欺骗老实人的心。
18maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu.
19你们的顺服已经名闻各处,所以我为你们高兴。我愿你们在善事上有智慧,在恶事上毫不沾染。
19Kila mtu amesikia juu ya utii wenu na hivyo mmekuwa sababu ya furaha yangu. Nawatakeni muwe na hekima katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya.
20赐平安的 神快要把撒但践踏在你们脚下。愿我们主耶稣的恩惠与你们同在。
20Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
21问安和颂赞我的同工提摩太和我的亲族路求、耶逊和所西巴德都问候你们。
21Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipatro, wananchi wenzangu, wanawasalimu.
22(我──代笔写这封信的德图──也在主里问候你们。)
22Nami Tertio, ninayeandika barua hii nawasalimuni katika Bwana.
23那接待我也接待全教会的该犹,问候你们。本城的司库以拉都和夸图弟兄问候你们。
23Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu.
24(有些抄本有第24节:“愿我们主耶稣基督的恩惠,与你们众人同在。阿们。”)
24Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.
25 神能依照我所传的福音和耶稣基督所传的信息,照着他奥秘的启示,坚定你们。
25Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya ujumbe wa Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita.
26这奥秘自古以来秘而不宣,但现在借着众先知所写的,照着永恒的 神的谕旨,已经向万国显明出来,使他们相信而顺服。
26Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirisha kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii.
27愿荣耀借着耶稣基督,归给独一全智的 神,直到永远。阿们。
27Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina.