聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

1 John

2

1我们的维护者基督
1Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini, ikijatokea mtu akatenda dhambi, tunaye mmoja ambaye hutuombea kwa Baba, ndiye Yesu Kristo aliye mwadilifu kabisa.
2他为我们的罪作了赎罪祭,不仅为我们的罪,也为全人类的罪。
2Kristo ndiye sadaka iondoayo dhambi zetu; wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.
3我们若遵守 神的命令,这样,就知道我们已经认识他。
3Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.
4凡是说“我已经认识他”,却不遵守他命令的,就是说谎的人,真理就不在他里面了。
4Mtu akisema kwamba anamjua, lakini hazitii amri zake, basi mtu huyo ni mwongo, na ukweli haumo ndani yake.
5然而凡是遵守他的道的,他爱 神的心就的确在他里面完全了。这样,我们就知道我们是在 神里面了。
5Lakini mtu yeyote anayeshika neno la Mungu, huyo ndiye aliye na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hivi ndivyo tunavyoweza kuwa na hakika kwamba tunaungana naye:
6凡说自己是住在他里面的,就应该照着他所行的去行。
6mtu yeyote anayesema kwamba ameungana na Mungu, anapaswa kuishi kama alivyoishi Yesu Kristo.
7爱弟兄的就是住在光明中亲爱的,我写给你们的,不是一条新命令,而是你们本来就有的旧命令。这旧命令就是你们听过的道。
7Wapenzi wangu, amri hii ninayowaandikieni si amri mpya; ni amri ileile ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Amri hiyo ya zamani ni ule ujumbe mliousikia.
8然而,因为黑暗渐渐消逝,真光已在照耀,我写给你们的也是一条新命令,这在 神和在你们来说,都是真的。
8Hata hivyo, amri hii ninayowaandikieni ni amri mpya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu pia. Maana giza linatoweka, na mwanga wa ukweli umekwisha anza kuangaza.
9凡是说自己在光明中,却恨他的弟兄的,他到现在还在黑暗里。
9Yeyote asemaye kwamba yumo katika mwanga, lakini anamchukia ndugu yake, mtu huyo bado yumo gizani.
10凡是爱弟兄的,就是住在光明中,在光明中他就不会跌倒。
10Yeyote ampendaye ndugu yake, yuko katika mwanga, na hamna chochote ndani yake kiwezacho kumkwaza mtu mwingine.
11凡是恨弟兄的,就是在黑暗里,也在黑暗里行事。他不知道往哪里去,因为黑暗弄瞎了他的眼睛。
11Lakini anayemchukia ndugu yake, yumo gizani; anatembea gizani, na hajui anakokwenda, maana giza limempofusha.
12孩子们,我写信给你们,因为你们的罪因着主的名已经得到赦免。
12Ninawaandikieni ninyi watoto, kwa kuwa dhambi zenu zimeondolewa kwa jina la Kristo.
13父老们,我写信给你们,因为你们认识太初就存在的那一位。青年们,我写信给你们,因为你们已经胜过那恶者。
13Nawaandikieni ninyi kina baba kwani mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo, Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule Mwovu.
14孩子们,我写信给你们,因为你们认识父。父老们,我写信给你们,因为你们认识太初就存在的那一位。青年们,我写信给你们,因为你们强壮, 神的道在你们心里,你们也胜过了那恶者。
14Nawaandikieni ninyi watoto, kwa sababu mnamjua Baba. Nawaandikieni ninyi kina baba, kwa kuwa mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo. Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mna nguvu; neno la Mungu limo ndani yenu na mmemshinda yule Mwovu.
15不要爱世界和世上的东西。人若爱世界,爱父的心就不在他里面了。
15Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
16原来世上的一切,就如肉体的私欲,眼目的私欲和今生的骄傲,都不是出于父,而是从世界来的。
16Vitu vyote vya ulimwengu-tamaa mbaya za mwili, vitu wanavyoviona watu na kuvitamani, majivuno yasababishwayo na mali-vyote hivyo havitoki kwa Baba, bali vyatoka kwa ulimwengu.
17这世界和世上的私欲都要渐渐过去,但那遵行 神旨意的却存到永远。
17Ulimwengu pamoja na vitu vyake vyote vyenye kutamanika unapita; lakini mtu atendaye atakalo Mungu, anaishi milele.
18敌基督者否认耶稣是基督孩子们,现在是末世的时候了。你们听过敌基督者要来,现在已经有不少敌基督起来了;因此我们就知道这是末世的时候了。
18Watoto, mwisho u karibu! Mlikwisha sikia kwamba adui wa Kristo anakuja, na sasa adui wengi wa Kristo wamekwisha fika, na hivyo twajua kwamba mwisho u karibu.
19他们从我们中间离去,这就表明他们是不属于我们的。其实他们并不属于我们,如果真的属于我们,就一定会留在我们中间。
19Watu hao wametokea kati yetu lakini hawakuwa kweli wa kwetu na ndiyo maana walituacha; Kama wangalikuwa wa kwetu, wangalibaki nasi. Lakini waliondoka, wakaenda zao, kusudi ionekane wazi kwamba hawakuwa kamwe wa kwetu.
20你们从那圣者得着膏抹,这是你们都知道的。
20Ninyi, lakini, mlipata kumiminiwa Roho Mtakatifu na Kristo, na hivyo mnaujua ukweli.
21我写信给你们,不是因为你们不明白真理,而是因为你们明白,又因为谎言绝不会出于真理的。
21Basi, nawaandikieni, si kwa kuwa hamuujui ukweli, bali kwa sababu mnaujua; na pia mnajua kwamba uongo wowote haupatikani katika ukweli.
22那么,谁是说谎的呢?不就是那否认耶稣是基督的吗?否认父和子的,他就是敌基督的。
22Mwongo ni nani? Ni yule anayekana kwamba Yesu ni Masiha. Mtu wa namna hiyo ni adui wa Kristo--anamkana Baba na Mwana.
23凡否认子的,就没有父;承认子的,连父也有了。
23Maana yeyote anayemkana Mwana, anamkana pia Baba; na yeyote anayemkubali Mwana, anampata Baba pia.
24至于你们,总要把起初所听见的存记在你们心里;你们若把起初所听见的存记在心里,你们也就住在子和父里面了。
24Basi, ujumbe ule mliousikia tangu mwanzo na ukae mioyoni mwenu. Kama ujumbe huo mliousikia tangu mwanzo ukikaa ndani yenu, basi, mtaishi daima katika umoja na Mwana na Baba.
25他应许给我们的,就是永远的生命。
25Na ahadi aliyotuahidia sisi ndiyo hii: uzima wa milele.
26我把这些事写给你们,是指着那些欺骗你们的人说的。
26Nimewaandikieni mambo haya kuhusu wale wanaotaka kuwapotosha ninyi.
27你们既然在你们里面有从主领受的膏抹,就不需要别人教导你们了,因为在一切事上有主的膏抹教导你们;这膏抹是真的,不是假的,你们应该按着他所教导的住在他里面。
27Lakini, kwa upande wenu ninyi, Kristo aliwamiminieni Roho wake. Na kama akiendelea kukaa ndani yenu, hamhitaji kufundishwa na mtu yeyote. Maana Roho wake anawafundisheni kila kitu na mafundisho yake ni ya kweli, si ya uongo. Basi shikeni mafundisho ya huyo Roho na kubaki katika muungano na Kristo.
28 神的儿女就不犯罪孩子们,你们要住在主里面。这样,他若显现,我们就可以坦然无惧;他来的时候,我们也不至惭愧地躲避他了。
28Naam, watoto, kaeni ndani yake kusudi wakati atakapotokea tuwe hodari bila kuwa na sababu ya kujificha kwa aibu Siku ya kuja kwake.
29你们既然晓得 神是公义的,就应当知道所有行公义的都是从他生的。
29Mnajua kwamba Kristo ni mwadilifu kabisa; basi, mnapaswa kujua pia kwamba kila mtu atendaye mambo adili ni mtoto wa Mungu.