1你们看,父赐给我们的是怎样的爱,就是让我们可以称为 神的儿女,我们也真是他的儿女。因此,世人不认识我们,是因为他们不认识父。
1Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
2亲爱的,现在我们是 神的儿女,将来怎样,还没有显明;然而我们知道:主若显现,我们必要像他,因为我们必要看见他本来是怎样的。
2Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
3凡对他存着这盼望的,就洁净自己,像他一样的洁净。
3Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
4凡是犯罪的,就是作了不法的事;罪就是不法。
4Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
5你们知道主曾经显现,为要除掉罪,他自己却没有罪。
5Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
6凡是住在他里面的,就不犯罪;凡犯罪的,是未曾见过他,也不认识他。
6Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
7孩子们,不要受人欺骗,行义的才是义人,正如主是公义的。
7Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
8犯罪的是出于魔鬼,因为魔鬼从起初就犯罪。因此, 神的儿子显现了,是要除灭魔鬼的作为。
8Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
9凡是从 神生的,就不犯罪,因为 神的生命在他里面;他也不能犯罪,因为他是从 神生的。
9Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
10这样,谁是 神的儿女,谁是魔鬼的儿女,就很明显了。凡不行义的,就不是出于 神,不爱弟兄的,也是这样。
10Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
11应当彼此相爱我们应当彼此相爱,因为这是你们从起初听见的信息。
11Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
12不要像该隐,他是属于那恶者的,他又杀了自己的弟弟。为什么杀他呢?因为他自己的行为是恶的,弟弟的行为是义的。
12Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
13弟兄们,世人若恨你们,不要希奇。
13Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
14我们因为爱弟兄,就知道我们已经出死入生了;不爱弟兄的,仍然住在死中。
14Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
15凡恨弟兄的,就是杀人的。你们知道,杀人的在他里面没有永生。
15Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake.
16主为我们舍命,这样,我们就知道什么是爱;我们也应当为弟兄舍命。
16Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
17凡有世上财物的,看见弟兄穷乏,却硬着心肠不理,他怎能说他心里有 神的爱呢?
17Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
18孩子们,我们爱人,不要只在言语和舌头上,总要在行动和真诚上表现出来。
18Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
19在 神面前可以坦然无惧这样,我们就知道我们是属于真理的。即使我们的心责备我们,在 神面前我们也可以心安理得,因为他比我们的心大,他知道一切。
19Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
20
20Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
21亲爱的,我们的心若不责备我们,在 神面前我们就可以坦然无惧了。
21Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
22凡我们所求的,就必从他得着,因为我们遵守他的命令,作他所喜悦的事。
22na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
23 神的命令,就是要我们信他的儿子耶稣基督的名,并且照着他的吩咐彼此相爱。
23Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
24凡是遵守 神命令的,就住在 神里面, 神也住在他里面。凭着 神所赐给我们的圣灵,我们就可以知道 神住在我们里面。
24Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.