聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

1 Peter

3

1妻子与丈夫
1Nanyi wake, jiwekeni chini ya mamlaka ya waume zenu, ili kama wako waume wowote wasioamini neno la Mungu, wapate kuamini kwa kuuona mwenendo wenu. Haitakuwa lazima kwenu kusema neno,
2因为他们看见了你们敬畏和纯洁的生活。
2kwani wataona jinsi mwenendo wenu ulivyo safi na wa kumcha Mungu.
3不要单注重外表的装饰,就如鬈头发、戴金饰、穿华丽衣服;
3Katika kujipamba kwenu msitegemee mambo ya njenje, kama vile mitindo ya kusuka nywele, kujivalia vitu vya dhahabu na nguo maridadi.
4却要在里面存着温柔安静的心灵,作不能毁坏的装饰,这在 神面前是极宝贵的。
4Bali, uzuri wenu unapaswa kutokana na hali ya ndani ya utu wa kweli, uzuri usioharibika wa wema na utulivu wa roho, ambao ni wa thamani kubwa mbele ya Mungu.
5因为古时仰望 神的圣洁妇女,正是这样装饰自己,顺服丈夫,
5Ndivyo walivyojipamba hapo kale wanawake waadilifu waliomtumainia Mungu; walijiweka chini ya mamlaka ya waume zao.
6像撒拉听从亚伯拉罕,称他为主一样;你们若行善,不怕任何恐吓,就是撒拉的女儿了。
6Sara kwa mfano alimtii Abrahamu na kumwita yeye bwana. Ninyi mmekuwa sasa binti zake kama mkitenda mema bila kuogopa tisho lolote.
7照样,你们作丈夫的,也要合情合理的与妻子同住。要体谅她比你软弱,要尊敬她,因为她是和你一同承受生命的恩典的。这样,就使你们的祷告不受拦阻。
7Kadhalika nanyi waume, katika kuishi na wake zenu mnapaswa kutambua kwamba wao ni dhaifu na hivyo muwatendee kwa heshima; maana nao pia watapokea pamoja nanyi zawadi ya uzima anayowapeni Mungu. Hapo ndipo sala zenu hazitakataliwa.
8为义受苦的有福了总括来说,你们要彼此同心,互相体恤,亲爱像弟兄,满有温柔,存心谦卑。
8Mwisho nasema hivi: mnapaswa kuwa na moyo mmoja, na fikira moja; mnapaswa kupendana kidugu, kuwa wapole na wanyenyekevu ninyi kwa ninyi.
9不要以恶报恶,以辱骂还辱骂,倒要祝福,因为你们就是为此蒙召,好叫你们承受福气。
9Msiwalipe watu ovu kwa ovu, au tusi kwa tusi; bali watakieni baraka, maana ninyi mliitwa na Mungu mpate kupokea baraka.
10因为“凡希望享受人生,要看见好日子的,就要禁止舌头不出恶言,嘴唇不说诡诈的话;
10Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, anapaswa kuacha kusema mabaya na kuacha kusema uongo.
11也要离恶行善,寻找并追求和睦。
11Na ajiepushe na uovu, atende mema, atafute amani na kuizingatia.
12因为主的眼睛看顾义人,他的耳朵垂听他们的呼求;但主的脸敌对作恶的人。”
12Maana Bwana huwatazama kwa wema waadilifu na kuzisikiliza sala zao. Lakini huwapa kisogo watu watendao maovu."
13如果你们热心行善,有谁能害你们呢?
13Ni nani atakayeweza kuwadhuru ninyi kama mkizingatia kutenda mema?
14就算你们要为义受苦,也是有福的。”不要怕人的恐吓,也不要畏惧。”
14Lakini, hata kama itawapasa kuteseka kwa sababu ya kutenda mema, basi, mna heri. Msimwogope mtu yeyote, wala msikubali kutiwa katika wasiwasi.
15只要心里尊基督为圣,以他为主;常常作好准备,去回答那些问你们为什么怀有盼望的人,
15Lakini mtukuzeni Kristo kama Bwana mioyoni mwenu. Muwe tayari kumjibu yeyote atakayewaulizeni juu ya matumaini yaliyo ndani yenu,
16但要用温柔敬畏的心回答。当存无愧的良心,使那些诬赖你们这在基督里有好品行的人,在毁谤你们的事上蒙羞。
16lakini fanyeni hivyo kwa upole na heshima. Muwe na dhamiri njema, kusudi mnapotukanwa, wale wanaosema ubaya juu ya mwenendo wenu mwema kama Wakristo, waone aibu.
17如果 神的旨意是要你们受苦,那么为行善受苦,总比为行恶受苦好。
17Maana ni afadhali kuteseka kwa sababu ya kutenda mema, kama Mungu akipenda, kuliko kuteseka kwa sababu ya kutenda uovu.
18因为基督也曾一次为你们的罪死了,就是义的代替不义的,为要领你们到 神面前。就肉体的方面说,他曾死去;就灵的方面说,他复活了;
18Kwa maana Kristo mwenyewe alikufa kwa ajili ya dhambi zenu; alikufa mara moja tu na ikatosha, mtu mwema kwa ajili ya waovu, ili awapeleke ninyi kwa Mungu. Aliuawa kimwili lakini akafanywa hai kiroho;
19他借这灵也曾去向那些在监管中的灵宣讲,
19na kwa maisha yake ya kiroho alikwenda kuwahubiria wale roho waliokuwa kifungoni.
20他们就是挪亚建造方舟的日子、 神容忍等待的时候,那些不顺从的人。当时进入方舟、借着水得救的人不多,只有八个。
20Hao ndio wale waliokataa kumtii Mungu alipowangoja kwa saburi wakati Noa alipokuwa anatayarisha ile safina. Ndani ya chombo hicho ni watu wachache tu, yaani watu wanane, waliookolewa majini,
21这水预表的洗礼,现在也拯救你们:不是除去肉体的污秽,而是借着耶稣基督的复活,向 神许愿常存纯洁的良心。
21ambayo yalikuwa mfano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo si shauri la kuondoa uchafu mwilini, bali ni ahadi kwa Mungu inayofanyika katika dhamiri njema. Huwaokoeni kwa njia ya ufufuo wa Yesu Kristo,
22基督已进到天上,在 神右边,众天使、有权势的、有能力的,都服从了他。
22ambaye alikwenda mbinguni na sasa amekaa upande wa kulia wa Mungu, anatawala juu ya malaika, wakuu na wenye enzi.