聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

1 Peter

4

1要有受苦的心志
1Maadamu Kristo aliteseka kimwili, nanyi pia mnapaswa kujiimarisha kwa nia hiyo yake; maana mtu akisha teseka kimwili hahusiki tena na dhambi.
2好叫你们不再随从人的私欲,只顺从 神的旨意,在世上度余下的光阴。
2Tangu sasa, basi, maisha yaliowabakia kuishi hapa duniani yanapaswa kuongozwa na matakwa ya Mungu, si na tamaa za kibinadamu.
3因为你们过去随从教外人的心意,行邪淫、私欲、醉酒、荒宴、狂饮和可憎拜偶像的事,时候已经够了。
3Wakati uliopita mlikuwa na muda mrefu wa kufanya mambo wanayofanya watu wasiomjua Mungu. Mliishi maisha ya anasa, ubinafsi, ulevi, ugomvi, kunywa mno na ya ibada haramu za sanamu.
4他们见你们不再与他们同奔那纵情放荡的路,就觉得奇怪,毁谤你们。
4Sasa, watu hao wasiomjua Mungu wanashangaa wanapoona kwamba hamwandamani nao tena katika hali ya kuishi vibaya, na hivyo wanawatukaneni.
5他们必要向那位预备要审判活人死人的主交帐。
5Lakini watapaswa kutoa hoja juu ya jambo hilo mbele yake Mungu aliye tayari kuwahukumu wazima na wafu!
6因此,那些死人也曾有福音传给他们,好使他们的肉体受了人要受的审判,他们的灵却靠 神活着。
6Kwa sababu hiyo, hao waliokufa ambao walikuwa wamehukumiwa katika maisha yao ya kimwili kama anavyohukumiwa kila mmoja, walihubiriwa Habari Njema kusudi katika maisha yao ya kiroho waishi kama aishivyo Mungu.
7按照恩赐彼此服事万物的结局近了,所以你们要谨慎警醒地祷告。
7Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na nidhamu, ili mweze kusali.
8最重要的是要彼此切实相爱,因为爱能遮盖许多的罪。
8Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi.
9你们要互相接待,不发怨言。
9Muwe na ukarimu ninyi kwa ninyi bila kunung'unika.
10你们要作 神各样恩赐的好管家,各人照着所领受的恩赐彼此服事。
10Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine, kama vile uwakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu.
11讲道的,应当按着 神的圣言讲;服事的,应当按着 神所赐的力量服事,为要在一切事上,使 神借耶稣基督得荣耀。荣耀、权能都是他的,直到永永远远。阿们。
11Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumika anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina.
12为基督受苦的有福了亲爱的,有火炼的试验临到你们,不要以为奇怪,好像是遭遇非常的事,
12Wapenzi wangu, msishangae kuhusu majaribio makali mnayopata kana kwamba mnapatwa na kitu kisicho cha kawaida.
13倒要欢喜,因为你们既然在基督的受苦上有分,就在他荣耀显现的时候,可以欢喜快乐。
13Ila furahini kwamba mnashiriki mateso ya Kristo ili mweze kuwa na furaha tele wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
14你们要是为基督的名受辱骂,就有福了!因为 神荣耀的灵,住在你们身上。
14Heri yenu ikiwa mnatukanwa kwa sababu ya jina la Kristo; jambo hilo lamaanisha kwamba Roho mtukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yetu.
15你们中间不可有人因为杀人、或偷窃、或行恶、或好管闲事而受苦。
15Asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu ambaye anapaswa kuteseka kwa sababu ni muuaji, mwizi, mhalifu au mwovu.
16如果因为作基督徒而受苦,不要以为羞耻,倒要借着这名字荣耀 神。
16Lakini kama mtu akiteseka kwa sababu ni Mkristo, basi asione aibu, bali amtukuze Mungu, kwa sababu mtu huyo anaitwa kwa jina la Kristo.
17因为审判从 神的家开始,就在这时候了。如果先从我们起头,那不信从 神福音的人,结局将要怎样呢?
17Wakati wa hukumu umefika, na hukumu hiyo inaanza na watu wake Mungu mwenyewe. Ikiwa hukumu hiyo inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasioamini Habari Njema ya Mungu?
18“如果义人仅仅得救,不敬虔和犯罪的人,又会变成怎样呢?”
18Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni vigumu kwa watu waadilifu kuokolewa; itakuwaje basi kwa wasiomcha Mungu na wenye dhambi?"
19所以那顺着 神的旨意而受苦的人,要继续地行善,把自己的生命交托那信实的创造者。
19Kwa hiyo, wale wanaoteseka kufuatana na matakwa ya Mungu, wanapaswa, kwa matendo yao mema, kujiweka chini ya Muumba wao ambaye ni wa kuaminika kabisa.