1凡负轭作奴仆的,应当看自己的主人是配受十分的敬重,免得 神的名和道理被人亵渎。
1Watumwa wote wanapaswa kuwaheshimu wakuu wao ili kusiwe na sababu ya watu kulitukana jina la Mungu na mafundisho yetu.
2奴仆有信主的主人,不可因为他们是弟兄而轻看他们;倒要加意服事他们,因为这些受到服事的益处的,是信主蒙爱的人。你要把这些事教导人,劝勉人。
2Watumwa ambao wakuu wao ni Wakristo wasiwadharau kwani ni ndugu zao. Badala yake, wanapaswa kuwatumikia hata vizuri zaidi, maana hao wanaopata faida kutokana na kazi yao ni waumini ambao wanawapenda. Unapaswa kufundisha na kuhubiri mambo haya.
3敬虔与知足如果有人传别的教义,不接受我们的主耶稣基督纯正的话语,和那敬虔的道理,
3Mtu yeyote anayefundisha kinyume cha mambo haya, na ambaye hakubaliani na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo na mafundisho ya dini,
4他是自高自大,一无所知,反而专好问难争辩,由此产生妒忌、纷争、毁谤、恶意的猜疑,
4huyo amejaa majivuno na wala hajui chochote. Ni mtu wa kupenda ubishi na magombano juu ya maneno matupu, na hiyo husababisha wivu, ugomvi, matusi, shuku mbaya,
5就和那些心术败坏,丧失真理的人不断地争竞。他们视敬虔为得利的门路。
5na ubishi usio na kikomo kutoka kwa watu ambao akili zao zimeharibika, na ambao hawana tena ukweli. Wanadhani dini ni njia ya kujipatia utajiri.
6其实敬虔而又知足,就是得大利的途径,
6Kweli dini humfanya mtu awe tajiri sana, ikiwa anatosheka na vitu alivyo navyo.
7因为我们没有带什么到世上来,也不能带什么去。
7Maana hatukuleta kitu chochote hapa duniani, wala hatutachukua chochote.
8只要有衣有食,就应当知足。
8Kwa hiyo basi, kama tunacho chakula na mavazi, tunapaswa kuridhika navyo.
9但那些想要发财的人,就落在试探中和陷阱里;又落在许多无知而有害的私欲里,使人沉沦在败坏和灭亡中;
9Lakini wale wanaotaka kutajirika huanguka katika majaribu, na kunaswa katika mtego wa tamaa nyingi mbaya za kipumbavu, ambazo huwavuta mpaka kwenye uharibifu na maangamizi.
10因为贪财是万恶之根。有人贪爱钱财,就被引诱离开真道,用许多痛苦把自己刺透了。
10Kwa maana kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote. Watu wengine wametamani sana kupata fedha hata wakatangatanga mbali na imani, na wameivunja mioyo yao kwa huzuni nyingi.
11要为信仰打那美好的仗但你这属 神的人啊,应该逃避这些事,要追求公义、敬虔、信心、爱心、忍耐和温柔。
11Lakini wewe, mtu wa Mungu, jiepushe na mambo hayo. Zingatia uadilifu, uchaji wa Mungu, imani, mapendo, subira na unyenyekevu.
12要为信仰打那美好的仗,持定永生;你是为这永生而蒙召的,又在许多的证人面前承认过美好的信仰。
12Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi.
13我在赐生命给万物的 神面前,并那在本丢.彼拉多面前见证过美好的信仰的基督耶稣面前嘱咐你,
13Mbele ya Mungu anayevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Yesu Kristo aliyetoa ushahidi na kukiri ukweli mbele ya Pontio Pilato,
14你当毫无玷污,无可指摘地持守这命令,直到我们主耶稣基督的显现。
14nakuamuru ushike maagizo yako na kuyatii kwa uaminifu mpaka Siku ile atakapotokea Bwana wetu Yesu Kristo.
15到了适当的时候,那可称颂的、独一的全能者,万王之王,万主之主,必把基督的显现表明出来。
15Kutokea kwake kutafanyika wakati ufaao uliopangwa na Mungu mwenye heri na aliye Mtawala pekee, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
16只有他永远不死,住在不能接近的光里,没有人见过他,人也不能看见他。愿尊荣和永远的权能都归给他。阿们。
16Yeye peke yake anaishi milele, katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina.
17你要嘱咐那些今世富有的人,叫他们不要心高气傲,也不要寄望在浮动的财富上,却要仰望那厚赐百物给我们享用的 神。
17Waamuru watu walio matajiri katika mambo ya maisha ya sasa, wasijivune, wasiweke tumaini lao katika mali isiyoweza kutegemewa; bali wamtegemee Mungu, ambaye kwa ukarimu hutupatia vitu vyote tuvifurahie.
18又要嘱咐他们行善,在善事上富足,慷慨好施。
18Waamuru watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, na wawe wakarimu na walio tayari kuwashirikisha wengine mali zao.
19这样,就为自己在来世积聚财富,作美好的基础,好叫他们能够得着那真正的生命。
19Kwa namna hiyo watajiwekea hazina ambayo itakuwa kwao msingi imara kwa wakati ujao. Hapo wataweza kujipatia uzima ambao ni uzima wa kweli.
20提摩太啊,你要保守所交托你的,避免世俗的空谈和冒称是知识的那种反调;
20Timotheo, tunza salama yote yale uliyokabidhiwa. Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ubishi wa kipumbavu juu ya kile wanachokiita watu wengine: "Elimu".
21有些人自称有这知识,就偏离了真道。愿恩惠与你们同在。
21Maana wengine wamejidai kuwa na hiyo elimu, na matokeo yake wamepoteza imani. Nawatakieni nyote neema!