1如何处事待人
1Usimkemee mtu mzee, bali msihi kama vile angekuwa baba yako. Watendee vijana kama ndugu zako,
2劝年老的妇人好像劝母亲;存着纯洁的心,劝青年女子好像劝姊妹。
2wanawake wazee kama mama yako, na wasichana kama dada zako, kwa usafi wote.
3要敬重供养那些无依无靠的寡妇。
3Waheshimu wanawake wajane walio wajane kweli.
4寡妇若有儿孙,就应当让儿孙先在自己家里学习孝道,报答亲恩,因为这在 神面前是蒙悦纳的。
4Lakini mjane aliye na watoto au wajukuu, hao wanapaswa kujifunza kutimiza wajibu wao wa kidini kwa jamaa zao wenyewe na hivyo kuwalipa wazazi wao na wazee wao, kwani hilo ni jambo la kupendeza mbele ya Mungu.
5那无依无靠独居的寡妇,她们仰望 神,昼夜不住地祈求祷告。
5Mwanamke mjane kweli, asiye na mtu wa kumsaidia, amemwekea Mungu tumaini lake na huendelea kusali na kumwomba msaada usiku na mchana.
6寡妇若奢侈宴乐,虽然活着也是死的。
6Lakini mwanamke ambaye huishi maisha ya anasa, huyo amekufa, ingawa yu hai.
7这些事你要嘱咐她们,使她们无可指摘。
7Wape maagizo haya, wasije wakawa na lawama.
8人若连自己的家人也不供养,就是背弃信仰,比不信的人还不如。
8Lakini kama mtu hawatunzi watu wa jamaa yake, hasa wale wa nyumbani kwake, basi, mtu huyo ameikana imani, na ni mbaya zaidi kuliko mtu asiyeamini.
9寡妇登记,年纪必须到达六十岁,只作过一个丈夫的妻子,
9Usimtie katika orodha ya wajane, mjane yeyote ambaye hajatimiza miaka sitini. Tena awe amepata kuolewa mara moja tu,
10并且要有善行的见证:就如养育儿女,接待客旅,替圣徒洗脚,救济困苦的人,尽力行各样的善事等。
10na awe mwenye sifa nzuri: aliyewalea watoto wake vizuri, aliyewakaribisha wageni nyumbani kwake, aliyewaosha miguu watu wa Mungu, aliyewasaidia watu wenye taabu, na aliyejitolea kufanya mambo mema.
11至于年轻的寡妇,不要给她们登记,因为她们一旦情欲冲动而背弃基督的时候,就想结婚。
11Usiwaandikishe wajane vijana, kwani kama tamaa zao za maumbile zikizidi kuwa na nguvu zaidi kuliko kujitolea kwao kwa Kristo watataka kuolewa tena,
12她们被定罪,是因为丢弃了起初的信誓。
12na wataonekana kukosa uaminifu kuhusu ahadi yao ya pale awali.
13同时,她们懒惰惯了,挨家闲游;不但懒惰,而且好说闲话,好管闲事,说不该说的话。
13Wajane kama hao huanza kupoteza wakati wao wakizurura nyumba hata nyumba; tena ubaya zaidi ni kwamba huanza kuwasengenya watu, na kujitia katika mambo ya watu wengine, huku wakisema mambo ambayo hawangepaswa kusema.
14因此,我愿年轻的寡妇结婚,生儿育女,管理家务,不给敌人有辱骂的机会;
14Kwa hiyo ningependelea wajane vijana waolewe, wapate watoto na kutunza nyumba zao ili adui zetu wasipewe nafasi ya kusema mambo maovu juu yetu.
15因为有些人已经转去跟从撒但了。
15Kwa maana wajane wengine wamekwisha potoka na kumfuata Shetani.
16如果信主的妇女家中有寡妇,她就应该救济她们,不要让教会受累。这样,教会就可以救济那些无依无靠的寡妇了。
16Lakini kama mama Mkristo anao wajane katika jamaa yake, yeye anapaswa kuwatunza na si kuliachilia kanisa mzigo huo, ili kanisa liweze kuwatunza wajane wale waliobaki peke yao kabisa.
17那些善于治理教会的长老,尤其是那些在讲道和教导上劳苦的长老,你们应当看他们是配受加倍的敬重和供奉的。
17Wazee wanaowaongoza watu vizuri wanastahili kupata riziki maradufu, hasa wale wanaofanya bidii katika kuhubiri na kufundisha.
18因为经上说:“牛踹谷的时候,不可笼住它的嘴。”又说:“作工的配得工价。”
18Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Usimfunge ng'ombe kinywa anapopura nafaka." na tena "Mfanyakazi astahili malipo yake."
19控诉长老的事,除非有两三个证人,否则不要受理。
19Usikubali kupokea mashtaka dhidi ya mzee yasipowakilishwa na mashahidi wawili au watatu.
20常常犯罪的,你要当众责备他们,使其余的人也有所惧怕。
20Wale wanaotenda dhambi waonye hadharani, ili wengine wapate kuogopa.
21我在 神和基督耶稣以及蒙拣选的天使面前叮嘱你,要毫无成见地持守这些话,行事也不要偏心。
21Nakuamuru mbele ya Mungu, mbele ya Kristo Yesu, na mbele ya malaika watakatifu uyazingatie maagizo haya bila kuacha hata moja, wala kumpendelea mtu yeyote katika kila unachotenda.
22不要匆匆忙忙地替别人按手,也不要在别人的罪上有分,要保守自己清洁。
22Usiharakishe kumwekea mtu yeyote mikono kwa ajili ya kumtumikia Bwana. Usishiriki dhambi za wengine; jiweke katika hali safi.
23因为你的胃不好,而且身体常常软弱,不要单单喝水,可以稍微用点酒。
23Usinywe maji tu, bali unywe divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako, kwani unaugua mara kwa mara.
24有些人的罪是明显的,就先受审判;有些人的罪是后来才显露出来的。
24Dhambi za watu wengine huonekana waziwazi, nazo zawatangulia kwenye hukumu; lakini dhambi za wengine huonekana tu baadaye.
25照样,善行也是明显的,就算不明显,也不能隐藏。
25Vivyo hivyo, matendo mema huonekana waziwazi, na hata yale ambayo si dhahiri hayawezi kufichika.