聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

1 Timothy

4

1预言日后有人背道
1Roho asema waziwazi kwamba siku za baadaye watu wengine wataitupilia mbali imani; watazitii roho danganyifu na kufuata mafundisho ya pepo.
2这教训是出于说谎的人的虚伪,他们的良心好像被烧红的铁烙了一般。
2Mafundisho ya namna hiyo yanaenezwa na watu waongo wadanganyifu, ambao dhamiri zao ziko kama zimechomwa kwa chuma cha moto.
3他们禁止嫁娶,禁戒食物。食物本是 神所造的,是给信主和认识真理的人存感谢的心领受的。
3Watu hao hufundisha kwamba ni makosa kuona na pia kula vyakula fulani. Lakini Mungu aliviumba vyakula hivyo, ili wale walio waumini na ambao wanapata kuujua ukweli, wavitumie kwa shukrani.
4因为凡 神所造的,都是好的,只要存感谢的心领受,没有一样是可以弃绝的;
4Kila kitu alichoumba Mungu ni chema, wala hakuna kinachohitaji kukataliwa, bali vyote vipokelewe kwa sala ya shukrani,
5都因着 神的道和人的祈求成为圣洁了。
5kwa sababu neno la Mungu na sala hukifanya kitu hicho kikubalike kwa Mungu.
6要作信徒的榜样你若把这些事提醒弟兄们,就是基督耶稣的好仆役,常在信仰的话语上,和你所遵从美善的教训上得着培养。
6Kama ukiwapa ndugu wote maagizo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, ukijiendeleza kiroho kwa maneno ya imani na mafundisho ya kweli, ambayo wewe umeyafuata.
7总要弃绝世俗以及老妇的无稽之谈;要操练自己达到敬虔的地步。
7Lakini achana na hadithi zile zisizo za kidini na ambazo hazina maana. Jizoeshe kuishi maisha ya uchaji wa Mungu.
8因为操练身体,益处还少;唯独操练敬虔,凡事有益,享有今生和来世的应许。
8Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
9这话是可信的,是值得完全接纳的。
9Usemi huo ni wa kusadikika kabisa na unastahili kukubaliwa.
10我们也是为这缘故劳苦努力,因为我们的盼望在于永活的 神。他是万人的救主,更是信徒的救主。
10Sisi tunajitahidi na kufanya kazi kwa bidii kwani tumemwekea tumaini letu Mungu aliye hai ambaye ni Mwokozi wa watu wote, na hasa wale wanaoamini.
11这些事你要嘱咐人,教导人。
11Wape maagizo hayo na mafundisho hayo.
12不要叫人小看你年轻,总要在言语、行为、爱心、信心和纯洁上,都作信徒的榜样。
12Usikubali mtu yeyote akudharau kwa sababu wewe ni kijana, lakini jitahidi uwe mfano kwa wanaoamini: katika usemi wako, mwenendo wako, upendo, imani na maisha safi.
13在我来以前,你要专心宣读圣经、劝勉和教导。
13Tumia wakati wako na juhudi yako katika kusoma hadharani Maandiko Matakatifu, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
14不要忽略你所得的恩赐,就是众长老按手时借着预言赐给你的。
14Usiache kukitumia kile kipaji cha Kristo ndani yako ulichopewa kwa maneno ya manabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
15这些事你要认真实行,专心去作,使众人看出你的长进来。
15Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.
16你要谨慎自己,留心自己的教训。在这些事上要有恒心,因为你这样作,不但能救自己,也能救那些听你的人。
16Angalia sana mambo yako mwenyewe, na mafundisho yako. Endelea kufanya hayo maana ukifanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.