1渴望天上的居所
1Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono.
2我们现今在这帐棚里面叹息,渴望迁到那天上的住处,好像换上新的衣服;
2Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
3如果穿上了,就不会赤身出现了。
3Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
4我们这些在帐棚里面的人,劳苦叹息,是由于不愿意脱去这个,却愿意穿上那个,使这必死的被生命吞灭。
4Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
5那在我们身上完成了工作,使我们达成这目标的,就是 神。他已经把圣灵赐给我们作凭据。
5Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
6我们既然一向都是坦然无惧的,又知道住在身内就是与主分开
6Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
7(因为我们行事是凭着信心,不是凭着眼见),
7Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
8现在还是坦然无惧,宁愿与身体分开,与主同住。
8Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
9因此,我们立定志向,无论住在身内或是与身体分开,都要讨主的喜悦。
9Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
10因为我们众人都必须在基督的审判台前显露出来,使各人按着本身所行的,或善或恶,受到报应。
10Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
11劝人与 神和好我们既然知道主是可畏的,就劝勉众人。我们在 神面前是显明的,我盼望在你们的良心里也是显明的。
11Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
12我们不是又再向你们推荐自己,而是给你们机会以我们为乐,使你们可以应付那些只夸外貌不夸内心的人。
12Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
13如果我们疯狂,那是为了 神;如果我们清醒,那是为了你们。
13Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
14原来基督的爱催逼着我们,因为我们断定一个人替众人死了,众人就都死了。
14Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
15他替众人死了,为的是要使活着的人不再为自己活着,却为那替他们死而复活的主而活。
15Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
16所以,从今以后,我们不再按照人的看法认识人;虽然我们曾经按照人的看法认识基督,但现在不再这样了。
16Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
17如果有人在基督里,他就是新造的人,旧事已经过去,你看,都变成新的了!
17Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
18这一切都是出于 神,他借着基督使我们与他自己和好,并且把这和好的职分赐给我们,
18Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
19就是 神在基督里使世人与他自己和好,不再追究他们的过犯,并且把和好的道理托付了我们。
19Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
20因此,我们就是基督的使者, 神借着我们劝告世人。我们代替基督请求你们:跟 神和好吧!
20Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
21 神使那无罪的替我们成为有罪的,使我们在他里面成为 神的义。
21Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.