1作基督的精兵
1Basi, wewe mwanangu, uwe na nguvu katika neema tunayopata katika kuungana na Kristo Yesu.
2又应当把你在许多见证人面前从我这里听见的,交托给那些又忠心又能够教导别人的人。
2Chukua yale mafundisho uliyonisikia nikitangaza mbele ya mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu wanaoaminika, ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
3你应当和我同受磨难,好像基督耶稣的精兵。
3Shiriki katika mateso kama askari mwaminifu wa Kristo yesu.
4当兵的人不让世务缠身,为要使那招兵的人欢喜。
4Mwanajeshi vitani hujiepusha na shughuli za maisha ya kawaida ili aweze kumpendeza mkuu wa jeshi.
5竞赛的人若不遵守规则,就不能得冠冕。
5Mwanariadha yeyote hawezi kushinda na kupata zawadi ya ushindi kama asipozitii sheria za michezo.
6劳力的农夫理当先尝果实。
6Mkulima ambaye amefanya kazi ngumu anastahili kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
7你要想想我的话,因为凡事主必给你领悟力。
7Fikiria hayo ninayosema, kwani Bwana atakuwezesha uyaelewe yote.
8你要记得那从死人中复活的耶稣基督,他是大卫的后裔所生的,这就是我所传的福音。
8Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka wafu, aliyekuwa wa ukoo wa Daudi, kama isemavyo Habari Njema ninayoihubiri.
9我为了这福音受了磨难,甚至像犯人一样被捆绑起来;可是, 神的话却不被捆绑。
9Kwa sababu ya kuihubiri Habari Njema mimi nateseka na nimefungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu haliwezi kufungwa minyororo,
10因此,我为了选民忍受一切,好叫他们也可以得着在基督耶稣里的救恩,和永远的荣耀。
10na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele.
11“我们若与基督同死,就必与他同活;
11Usemi huu ni wa kweli: "Ikiwa tulikufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
12我们若能坚忍,就必与他一同作王;我们若不认他,他必不认我们;
12Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pia pamoja naye. Tukimkana, naye pia atatukana.
13我们纵然不信,他仍然是信实的,因为他不能否定自己。”这话是可信的。
13Tukikosa kuwa waaminifu, yeye hubaki mwaminifu daima, maana yeye hawezi kujikana mwenyewe."
14作无愧的工人你要在 神面前把这些事提醒众人,叮嘱他们不要作无益的争辩;这只能败坏听见的人。
14Basi, wakumbushe watu wako mambo haya, na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.
15你应当竭力在 神面前作一个蒙称许、无愧的工人,正确地讲解真理的道。
15Jitahidi kupata kibali kamili mbele ya Mungu kama mfanyakazi ambaye haoni haya juu ya kazi yake, na ambaye hufundisha sawa ule ujumbe wa kweli.
16总要远避世俗的空谈,因为这些必会引人进到更不敬虔的地步。
16Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ya kipumbavu; kwani hayo huzidi kuwatenga watu mbali na Mungu.
17他们的话好像毒瘤一样蔓延;他们当中有许米乃和腓理徒。
17Mafundisho ya aina hiyo ni kama donda linalokula mwili. Miongoni mwa hao waliofundisha hayo ni Humenayo na Fileto.
18他们偏离了真道,说复活的事已经过去了,于是毁坏了一些人的信心。
18Hawa wamepotoka kabisa mbali na ukweli, na wanatia imani ya watu wengine katika wasiwasi kwa kusema ati ufufuo wetu umekwisha fanyika.
19然而, 神坚固的根基已经立定,上面刻着这样的印:“主认识属于他的人”和“凡称呼主名的人都应当离开不义”。
19Lakini msingi thabiti uliowekwa na Mungu uko imara, na juu yake yameandikwa maneno haya: "Bwana anawafahamu wale walio wake," na "Kila asemaye yeye ni wa Bwana, ni lazima aachane na uovu."
20在富贵人的家里(“富贵人的家里”原文作“大房子”),不但有金器、银器,也有木器、瓦器;有贵重的,也有卑贱的。
20Katika nyumba kubwa kuna mabakuli na vyombo vya kila namna: vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine vya mbao na udongo, vingine ni vya matumizi ya pekee na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
21人若自洁,离开卑贱的事,就必作贵重的器皿,成为圣洁,合主使用,预备行各样的善事。
21Basi, kama mtu atajitakasa kwa kujitenga mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee, kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa Bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.
22你应当逃避年轻人的私欲,要和那些以清洁的心求告主的人,一同追求公义、信心、爱心、和平。
22Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.
23你要拒绝愚蠢无知的问难;你知道这些事会引起争论。
23Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.
24但主的仆人却不可争论,总要待人温和,善于教导,存心忍耐,
24Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,
25以温柔劝导那些对抗的人,或许 神给他们悔改的心,可以认识真理。
25ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.
26他们虽然曾经被魔鬼掳去,随从他的意思而行,或许也能醒悟过来,脱离魔鬼的陷阱。
26Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.