聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

2 Timothy

3

1末世的情况
1Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu.
2那时,人会专爱自己、贪爱钱财、自夸、高傲、亵渎、悖逆父母、忘恩负义、不圣洁、
2watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu;
3没有亲情、不肯和解、恶言中伤、不能自律、横蛮凶暴、不爱良善、
3watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema;
4卖主卖友、容易冲动、傲慢自大、爱享乐过于爱 神,
4watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu.
5有敬虔的形式,却否定敬虔的能力;这些人你应当避开。
5Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.
6他们中间有人潜入别人的家里,操纵无知的妇女。这些妇女被罪压住,又被各种私欲拖累,
6Baadhi yao huenda katika nyumba za watu na huwateka wanawake dhaifu waliolemewa mizigo ya dhambi na ambao wanaongozwa na tamaa za kila aina;
7虽然常常学习,总不能充分明白真理。
7wanawake ambao wanajaribu daima kujifunza lakini hawawezi kuufikia ujuzi wa huo ukweli.
8从前雅尼和杨蓓怎样反对摩西,这些人也怎样反对真理。他们的心思败坏,信仰也经不起考验。
8Watu hao huupinga ukweli kama vile Yane na Yambre walivyompinga Mose.
9然而他们不能再这样下去了,因为他们的愚昧终必在众人面前显露出来,好像那两个人一样。
9Lakini hawataweza kuendelea zaidi kwa maana upumbavu wao utaonekana wazi kwa wote. Ndivyo ilivyokuwa kwa akina Yane na Yambre.
10圣经都是 神默示的但是,你已经了解我的教训、品行、志向、信心、宽容、爱心和忍耐,
10Wewe lakini, umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, subira yangu,
11以及我在安提阿、以哥念、路司得所受的苦和迫害。我所忍受的是怎样的迫害;这一切主都救我脱离了。
11udhalimu na mateso yangu. Unayajua mambo yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Lustra. Nilivumilia udhalimu mkubwa mno! Lakini Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.
12其实,所有立志在基督耶稣里过敬虔生活的,都必遭受迫害。
12Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kumcha Mungu katika kuungana na Kristo Yesu lazima adhulumiwe.
13但恶人和骗子必越来越坏,他们欺骗人,也必受欺骗。
13Watu waovu na wadanyanyifu watazidi kuwa waovu zaidi na zaidi kwa kuwadanganya wengine na kudanganyika wao wenyewe.
14你应当遵守所学和确信的;你知道是跟谁学的,
14Lakini wewe dumu katika ukweli ule uliofundishwa, ukaukubali kabisa. Unawajua wale waliokuwa walimu wako.
15并且知道自己从小就明白圣经,这圣经能够使你有智慧,可以因信基督耶稣得着救恩。
15Unakumbuka kwamba tangu utoto wako umeyajua Maandiko Matakatifu ambayo yaweza kukupatia hekima iletayo wokovu kwa njia ya imani kwa Kristo Yesu.
16全部圣经都是 神所默示的,在教训、责备、矫正和公义的训练各方面,都是有益的,
16Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya, kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili,
17为要使属 神的人装备好,可以完成各样的善工。
17ili mtu anayemtumikia Mungu awe mkamilifu, na tayari kabisa kufanya kila tendo jema.