聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

2 Timothy

4

1务要传道
1Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
2务要传道;无论时机是否适合,都要常作准备;要以多方的忍耐和教训责备人、警戒人、劝勉人。
2hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
3因为时候快要到了,人必容不下纯正的道理,反而耳朵发痒,随着自己的私欲,增添许多教师,
3Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
4而且转离不听真理,反倒趋向无稽之谈。
4Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
5你却要凡事谨慎,忍受磨难、作传福音者的工作,完成你的职务。
5Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
6我已经被浇奠;我离世的时候也到了。
6Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7那美好的仗我已经打过了,当跑的路我已经跑尽了,所持的信仰我已经守住了。
7Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
8从此以后,有公义的冠冕为我存留,就是按公义审判的主在那日要赏给我的;不但赏给我,也赏给所有爱慕他显现的人。
8Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
9最后的吩咐你要尽快到我这里来。
9Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
10因为底马贪爱现今的世界,就离弃我到帖撒罗尼迦去了。革勒士去了加拉太,提多去了达马太。
10Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.
11只有路加在我这里。你找到了马可,就把他带来,因为他在圣工上对我有益。
11Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
12我差派了推基古到以弗所去。
12Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
13我在特罗亚留在加布那里的外衣,你来的时候要把它带来,还有那些书卷,特别是那些羊皮卷,也要带来。
13Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
14铜匠亚历山大作了许多恶事陷害我,主必按着他所行的报应他。
14Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
15你也要提防他,因为他极力抵挡我们的话。
15Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
16我第一次申辩的时候,没有一个人支持我,反而离弃我。但愿这罪不要归在他们身上。
16Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
17然而主站在我旁边,加给我力量,使福音的信息借着我尽都传开,万国的人都可以听见;他并且把我从狮子口中救出来。
17Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
18主必救我脱离一切邪恶的事,也必救我进入他天上的国。愿荣耀归给他,直到永永远远。阿们。
18Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina.
19问候的话问候百基拉、亚居拉和阿尼色弗一家的人。
19Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
20以拉都在哥林多住下了。特罗非摩病了,我就留他在米利都。
20Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
21你要赶紧在冬天以前到我这里来。友布罗、布田、利奴、革老底亚和众弟兄都问候你。
21Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
22主与你同在。愿恩惠与你们同在。
22Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.