1彼得向耶路撒冷教会报告
1Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2彼得上到耶路撒冷的时候,那些守割礼的人与他争论,
2Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3说:“你竟然到未受割礼的人那里,跟他们一起吃饭!”
3"Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4彼得就按着次序向他们讲解,说:
4Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5“我在约帕城祷告的时候,魂游象外,见到异象:有一件东西,好像一块大布,绑着四角,从天上降下来,一直来到我面前。
5"Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6我定睛观察,看见里面有地上的四足牲畜、走兽,还有昆虫和天空的飞鸟。
6Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7我也听见有声音对我说:‘彼得,起来,宰了吃!’
7Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8我说:‘主啊,千万不可,因为俗物或不洁的东西,从来没有进过我的口。’
8Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9第二次又有声音从天上回答:‘ 神所洁净的,你不可当作俗物。’
9Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10这样一连三次之后,所有的东西都拉回天上去了。
10Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11就在那个时候,有三个从该撒利亚派到我这里来的人,站在我住的房子门前。
11Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12圣灵吩咐我跟他们一起去,一点也不要疑惑。这六位弟兄也跟我一起去,我们就进了那人的家。
12Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13他告诉我们,他怎样看见天使站在他家里说:‘派人到约帕去,请那个名叫彼得的西门来,
13Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14他有话要告诉你,使你和你全家都可以得救。’
14Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15我一开始讲话,圣灵就降在他们身上,正像当初降在我们身上一样。
15Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16我就想起主所说的话:‘约翰用水施洗,但你们要受圣灵的洗。’
16Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17 神既然把同样的恩赐给他们,像给我们这些信了主耶稣基督的人一样,我是谁,我能够阻止 神吗?”
17Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?"
18众人听见这些话,就默然无声,把荣耀归给 神,说:“这样看来, 神也把悔改的心赐给外族人,使他们得生命。”
18Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, "Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!"
19安提阿的教会那些因司提反事件遭受苦难而四散的门徒,一直走到腓尼基、塞浦路斯、安提阿;他们不对别人传讲,只对犹太人传讲。
19Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20但其中有些塞浦路斯人和古利奈人,来到安提阿,也对希腊人传讲主耶稣。
20Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21主的手与他们同在,信而归主的人就多起来。
21Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22这事传到耶路撒冷教会的耳中,他们就派巴拿巴到安提阿去。
22Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23他到了那里,看见 神所施的恩,就很欢喜,劝勉众人坚心靠主。
23Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24巴拿巴是个好人,满有圣灵和信心,于是许多人归了主。
24Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25后来他到大数去找扫罗,
25Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26找到了,就带他来安提阿。足足有一年,他们一同在教会聚集,教导了许多人。门徒称为基督徒,是从安提阿开始的。
26Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27那时,有几位先知从耶路撒冷下到安提阿。
27Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28其中有一个名叫亚迦布的站起来,借着圣灵指出天下将要有大饥荒;这事在革老丢时期果然发生了。
28Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29于是门徒决定按着各人的力量捐款,好送给住在犹太的弟兄。
29Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30他们就这样行了,由巴拿巴和扫罗经手送到长老们那里。
30Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.