聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Acts

12

1雅各殉道,彼得被囚
1Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.
2用刀杀了约翰的哥哥雅各。
2Alimwua kwa upanga Yakobo ndugu yake Yohane.
3他见这事博得了犹太人的欢心,就在除酵节期间,再次捉拿彼得。
3Alipoona kuwa kitendo hiki kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu.)
4捉到了,就把他关在监里,交给四班士兵看守,每班四个人,打算过了逾越节,把他提出来交给民众。
4Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.
5彼得就这样被拘留在监里;但教会却为他迫切地祈求 神。
5Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.
6天使救彼得出监希律要提他出来的前一夜,彼得被两条锁链锁住,睡在两个士兵中间,还有卫兵守在门前。
6Usiku, kabla ya siku ile ambayo Herode angemtoa Petro hadharani, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili. Alikuwa amefungwa minyororo miwili, na walinzi walikuwa wanalinda lango la gereza.
7忽然,有主的一位使者出现,屋就光芒四射。天使拍拍彼得的肋旁,唤醒他,说:“快起来!”他手上的锁链就脱落了。
7Ghafla, malaika wa Bwana akasimama karibu naye na mwanga ukaangaza kile chumba cha gereza. Malaika akamgusa akisema, "Amka upesi!" Mara ile minyororo ikaanguka kutoka katika mikono yake.
8天使对他说:“束上带子,穿上鞋!”他就这样作了。天使又说:“披上外衣,跟我走!”
8Malaika akamwambia, "Jifunge mshipi wako, vaa viatu vyako." Akafanya hivyo. Kisha huyo malaika akamwambia, "Vaa koti lako, unifuate."
9他就出来跟着天使走,但他不知道天使所作的事是真的,还以为是见了异象。
9Petro akamfuata nje lakini hakujua kama hayo yaliyofanywa na huyo malaika yalikuwa ya kweli; alidhani alikuwa anaota ndoto.
10他们经过第一、第二两个岗位,来到通往城内的铁门,那门自动给他们开了。他们出来,往前走了一条街,天使立刻离开了他。
10Walipita kituo cha kwanza cha ulinzi na cha pili, halafu wakafika kwenye mlango wa chuma wa kuingilia mjini. Huo mlango ukawafungukia wenyewe, nao wakatoka nje. Wakawa wanatembea katika barabara moja na mara yule malaika akamwacha Petro peke yake.
11彼得清醒过来,说:“现在我确实知道,主差他的天使来,救我脱离希律的手和犹太人所期望的一切。”
11Hapo ndipo Petro alipotambua yaliyotukia, akasema, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa kutoka katika mkono wa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu wa Israeli waliyotazamia."
12他明白了之后,就到约翰(别名马可)的母亲马利亚家里去;有许多人聚集在那里祷告。
12Alipotambua hivyo alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Maria mama yake Yohane aitwaye Marko. Humo watu wengi walikuwa wamekusanyika wakisali.
13彼得敲了大门,有一个名叫罗大的使女,出来应门。
13Petro alibisha mlango wa nje na mtumishi mmoja msichana aitwaye Roda, akaenda mlangoni kuitikia.
14她认出是彼得的声音,欢喜到顾不得开门,就跑进去报告,说彼得站在门外。
14Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni.
15大家说:“你疯了!”她却坚持地说这是真的。他们说:“一定是他的天使。”
15Wakamwambia yule msichana, "Una wazimu!" Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, "Huyo ni malaika wake."
16彼得继续敲门;他们打开了,一见是他,就非常惊讶。
16Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa.
17彼得作了一个手势,要他们安静,然后对他们述说主怎样领他出监,又说:“你们把这些事告诉雅各和众弟兄。”就离开那里,到别的地方去了。
17Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
18天亮的时候,士兵们非常慌乱,不知彼得出了什么事。
18Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro.
19希律搜索他,却找不到,就审问卫兵,下令把他们带出去处死。后来希律离开犹太,到该撒利亚去,住在那里。
19Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea akaenda Kaisarea ambako alikaa.
20希律被 神击打当时希律对推罗和西顿人怀怒在心。这两地的人因为他们的地区都需要从王的领土得到粮食,就先拉拢了王的内侍臣伯拉斯都,然后同心地去见希律,要向他求和。
20Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
21到了定好的日期,希律穿上王服,坐在高台上,向他们演讲。
21Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme aliwahutubia watu.
22群众大声说:“这是 神的声音,不是人的声音!”
22Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, "Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu."
23他不归荣耀给 神,所以主的使者立刻击打他,他被虫咬,就断了气。
23Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa.
24 神的道日渐兴旺,越发广传。
24Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
25巴拿巴和扫罗完成了送交捐项的任务,就带着名叫马可的约翰,从耶路撒冷回来。
25Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza shughuli zao, walitoka tena Yerusalemu wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.