1在以哥念
1Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
2但不顺从的犹太人,煽动外族人,激起他们仇恨的心,来反对弟兄们。
2Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
3两人却仍住了很久,靠着主放胆讲论,主也借着他们的手行神迹奇事,证实他恩惠的道。
3Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
4城里众人就分裂了,有的附从犹太人,也有的附从使徒。
4Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
5当时,外族人、犹太人,和他们的首领,蠢蠢欲动,想要侮辱使徒,用石头打他们。
5Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
6两人知道了,就逃往吕高尼的路司得和特庇两城,以及周围的地方,
6Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
7在那里传福音。
7wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
8在路司得路司得城有一个双脚无力的人,坐在那里。他生来就是瘸腿的,从来没有走过路。
8Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
9他听保罗讲道;保罗注视他,见他有信心,可以治好,
9Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
10就大声说:“你起来,两脚站直!”他就跳起来,并且走起路来。
10akasema kwa sauti kubwa, "Simama wima kwa miguu yako!" Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
11众人看见保罗所作的事,就用吕高尼话大声说:“有神明成了人形,降到我们这里来了!”
11Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: "Miungu imetujia katika sura za binadamu!"
12于是他们称巴拿巴为宙斯,称保罗为汉密士,因为保罗带头讲话。
12Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
13城门前宙斯庙的祭司,牵着几头公牛,拿着一些花圈来到门口,要同群众一起献祭。
13Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14巴拿巴和保罗两个使徒听见了,就撕裂衣服,跳进群众中间,喊着说:
14Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15“各位,为什么这样作呢?我们也是人,性情和你们一样,我们传福音给你们,正是要你们远离这些虚妄的事,归向永活的 神,就是那创造天、地、海和其中万物的 神。
15"Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16在从前的世代里,他容忍万国各行其道,
16Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17然而却未尝不为自己留下明证,就如常常行善事,从天上降下雨来,常常赏赐丰年,使你们吃喝充足,满心欢乐。”
17Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha."
18两人说完了这些话,这才阻止群众,不向他们献祭。
18Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
19但有些犹太人,从安提阿、以哥念来,挑唆群众,用石头打保罗,以为他死了,就拖到城外去。
19Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
20门徒正围着他的时候,他竟然站起来,走进城里去了。第二天,他跟巴拿巴一同到特庇去。
20Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
21结束第一次宣教旅程他们在那城里传福音,使许多人作了门徒,然后回到路司得、以哥念、安提阿,
21Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
22坚固门徒的心,劝他们恒守所信的道,又说:“我们进入 神的国,必须经历许多苦难。”
22Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, "Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu."
23两人在各教会为他们指派了长老;禁食祈祷之后,就把他们交托给所信的主。
23Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24两人经过彼西底,来到旁非利亚,
24Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25在别加讲道以后,就下到亚大利。
25Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26从那里坐船往安提阿。从前众人就是在这地方,把他们交托在 神的恩典中,派他们去工作,现在他们已经完成了。
26Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27他们到了那里,就召集了会众,报告 神跟他们一起所行的一切,并且他为外族人开了信道的门。
27Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28两人同门徒住了不少日子。
28Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.