聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Acts

15

1耶路撒冷的会议
1Basi, watu wengine walifika Antiokia kutoka Yudea wakaanza kuwafundisha wale ndugu wakisema, "Kama hamtatahiriwa kufuatana na mapokeo ya Sheria ya Mose, hamtaweza kuokolewa."
2保罗和巴拿巴,与他们大大地争执辩论起来。大家就派保罗、巴拿巴和他们中间的几个人,为这个问题上耶路撒冷去见使徒和长老。
2Jambo hili lilisababisha ubishi mkubwa, na baada ya Paulo na Barnaba kujadiliana nao, ikaamuliwa Paulo na Barnaba pamoja na waumini kadhaa wa lile kanisa la Antiokia waende Yerusalemu kuwaona wale mitume na wazee kuhusu jambo hilo.
3于是教会给他们送行,他们就经过腓尼基、撒玛利亚,述说外族人怎样归主的事,使弟兄们大大喜乐。
3Basi, kanisa liliwaaga, nao walipokuwa wanapitia Foinike na Samaria waliwaeleza watu jinsi mataifa mengine yalivyomgeukia Mungu. Habari hizo zikawafurahisha sana ndugu hao wote.
4到了耶路撒冷,他们受到教会、使徒和长老的接待,就报告 神同他们一起所行的一切。
4Walipofika Yerusalemu walikaribishwa na kanisa, mitume na wazee; nao wakawapa taarifa juu ya yote Mungu aliyoyafanya pamoja nao.
5然而有几个法利赛派的信徒站起来,说:“我们必须给外族人行割礼,吩咐他们遵守摩西的律法。”
5Lakini waumini wengine waliokuwa wa kikundi cha Mafarisayo walisimama, wakasema, "Ni lazima watu wa mataifa mengine watahiriwe na kufundishwa kuifuata Sheria ya Mose."
6使徒和长老聚集在一起,商议这件事。
6Basi, mitume na wazee walifanya mkutano maalum wa kuchunguza jambo hilo.
7经过了很多的辩论,彼得站起来对他们说:“弟兄们,你们知道,前些时候 神在你们中间拣选了我,使外族人从我的口中听见福音的道,而且信了。
7Baada ya majadiliano marefu, Petro alisimama, akasema, "Ndugu zangu, ninyi mnafahamu kwamba hapo awali Mungu alipenda kunichagua mimi miongoni mwenu niihubiri Habari Njema, ili watu wa mataifa wapate kusikia na kuamini.
8知道人心的 神也为他们作证──赐圣灵给他们,像给我们一样;
8Naye Mungu anayejua mioyo ya watu, alithibitisha kwamba amewakubali kwa kuwapa nao Roho Mtakatifu kama alivyotupa sisi.
9而且他待他们和我们没有分别,因为借着信,他洁净了他们的心。
9Hakufanya ubaguzi wowote kati yetu na wao; aliitakasa mioyo yao kwa imani.
10现在你们为什么试探 神,把我们祖先和我们所不能负的轭,放在门徒的颈上呢?
10Sasa basi, kwa nini kumjaribu Mungu kwa kuwatwika hao waumini mzigo ambao wala babu zetu, wala sisi hatukuweza kuubeba?
11我们相信,我们得救是借着主耶稣的恩,和他们也是一样。”
11Isiwe hivyo, ila tunaamini kwamba, sisi kama vile wao, tunaokolewa kwa njia ya neema ya Bwana Yesu."
12大家都静默无声,听巴拿巴和保罗述说 神借着他们在外族人中所行的神迹奇事。
12Kikundi chote kilikaa kimya, kikawasikiliza Barnaba na Paulo wakieleza miujiza na maajabu ambayo Mungu alitenda kwa mikono yao kati ya watu wa mataifa mengine.
13他们讲完了,雅各说:“弟兄们,请听我说!
13Walipomaliza kuongea, Yakobo alianza kusema: "Ndugu zangu, nisikilizeni!
14刚才西门述说 神当初怎样关怀外族人,从他们中间拣选了众人,归在自己的名下。
14Simoni ameeleza jinsi Mungu hapo awali alivyojishughulisha na watu wa mataifa mengine, akachagua baadhi yao wawe watu wake.
15众先知的话,也符合这个意思,正如经上所记:
15Jambo hili ni sawa kabisa na maneno ya manabii, kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:
16‘此后我要回来,重建大卫倒塌了的帐幕,重建它损坏之处,把它重新竖立起来,
16Baada ya mambo haya nitarudi. Nitaijenga tena ile nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitayatengeneza magofu yake na kuijenga tena.
17使余下的人,就是所有称为我名下的外族人,都寻求主,
17Hapo watu wengine wote, watu wa mataifa yote niliowaita wawe wangu, watamtafuta Bwana.
18这是自古以来就显明了这些事的主所说的。’
18Ndivyo asemavyo Bwana, aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale.
19“所以我认为不可难为这些归服 神的外族人,
19"Kwa hiyo, uamuzi wangu ni huu: tusiwataabishe watu wa mataifa wanomgeukia Mungu.
20只要写信叫他们禁戒偶像的污秽、淫乱,勒死的牲畜和血。
20Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa najisi kwa kutambikiwa sanamu za miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.
21因为自古以来,在各城里都有人宣讲摩西的书,每逢安息日,在各会堂里都有人诵读。”
21Kwa maana kwa muda mrefu maneno ya Mose yamekuwa yakihubiriwa katika kila mji na kusomwa katika masunagogi yote kila siku ya Sabato."
22会议的决定当时,使徒、长老和全教会都认为好,就从他们中间选出人来,差他们和保罗、巴拿巴一同到安提阿去,所选的就是别号巴撒巴的犹大和西拉,他们是弟兄中的领袖。
22Mitume, wazee na kanisa lote waliamua kuwachagua watu fulani miongoni mwao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Basi, wakamchagua Yuda aitwaye pia Barsaba, na Sila ambao wote walikuwa wanajulikana zaidi kati ya ndugu.
23于是写信给他们带去,信上说:“使徒和作长老的弟兄们,向安提阿、叙利亚、基利家的外族众弟兄问安。
23Wakawapa barua hii: "Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, tunawasalimuni ninyi ndugu wa mataifa mengine mlioko huko Antiokia, Siria na Kilikia.
24我们听说有人从我们这里出去,说了一些话搅扰你们,使你们心里不安,其实我们并没有吩咐他们。
24Tumesikia kwamba watu wengine kutoka huku kwetu waliwavurugeni kwa maneno yao, wakaitia mioyo yenu katika wasiwasi. Lakini wamefanya hivyo bila ya idhini yoyote kutoka kwetu.
25因此,我们一致同意,选派一些人跟我们亲爱的巴拿巴和保罗去见你们,
25Hivyo, tumeamua kwa pamoja kuwachagua watu kadhaa na kuwatuma kwenu pamoja na wapenzi wetu Barnaba na Paulo,
26这两个人为了我们主耶稣基督的名,曾经把性命置之度外。
26ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
27我们派了犹大和西拉一同去,他们也会亲口述说这些事。
27Kwa hiyo, tunawatuma Yuda na Sila kwenu; hawa watawaambieni wao wenyewe haya tuliyoandika.
28圣灵和我们都同意,不把别的重担加在你们身上,然而有几件事是重要的,
28Basi, Roho Mtakatifu na sisi tumekubali tusiwatwike mzigo zaidi ya mambo haya muhimu:
29就是禁戒祭过偶像的食物、血、勒死的牲畜和淫乱。这些事你们若能保守自己不作,那就好了。祝你们平安!”
29Msile vyakula vilivyotambikiwa sanamu; msinywe damu; msile nyama ya mnyama aliyenyongwa; na mjiepushe na uasherati. Mtakuwa mmefanya vema kama mkiepa kufanya mambo hayo. Wasalaam!"
30他们受了差派,下安提阿去,集合了众人,就把书信交上。
30Baada ya kuwaaga, hao wajumbe walielekea Antiokia ambako waliita mkutano wa waumini, wakawapa hiyo barua.
31众人读了,因信上的劝勉,就感到欣慰。
31Walipoisoma hiyo barua, maneno yake yaliwatia moyo, wakafurahi sana.
32犹大和西拉也是先知,说了许多话劝勉弟兄,坚固他们。
32Yuda na Sila, ambao nao walikuwa manabii, walizungumza na hao ndugu kwa muda mrefu wakiwatia moyo na kuwaimarisha.
33住了一段时间,弟兄们就给他们送行,祝一路平安;他们就回到差派他们的人那里去。
33Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, ndugu wa Antiokia waliwaaga wakiwatakia amani, kisha wakarudi kwa wale waliokuwa wamewatuma.
34(有些抄本在此有第34节:“但西拉认为自己应当在那里住下来,只有犹大回到耶路撒冷。”)
34Lakini Sila aliamua kubaki.
35保罗和巴拿巴却住在安提阿,跟许多别的人一同教导,传讲主的道。
35Paulo na Barnaba walibaki huko Antiokia kwa muda; wakafundisha na kuhubiri neno la Bwana, pamoja na watu wengine wengi.
36第二次宣教旅程过了一些时候,保罗对巴拿巴说:“我们要回到我们传过主道的各城,探望弟兄们,好知道他们的情形怎么样。”
36Baada ya siku kadhaa, Paulo alimwambia Barnaba, "Turudi tukawatembelee wale ndugu katika kila mji tulikolihubiri neno la Bwana tukajionee jinsi wanavyoendelea."
37巴拿巴有意要带别号马可的约翰一同去,
37Barnaba alitaka wamchukue pia Yohane aitwaye Marko.
38但保罗认为不应带他去,因为他从前在旁非利亚离开过他们,不跟他们一起去作工。
38Lakini Paulo hakupendelea kumchukua Marko, ambaye awali aliwaacha kule Pamfulia na kukataa kushiriki katika kazi yao.
39他们各持己见,以致彼此分手。巴拿巴带着马可,坐船到塞浦路斯去;
39Basi kukatokea ubishi mkali kati yao, na wakaachana. Barnaba akamchukua Marko, wakapanda meli kwenda Kupro.
40保罗却选了西拉,众弟兄把他交托在主的恩典中之后,他就出发了。
40Naye Paulo akamchagua Sila, na baada ya ndugu wa mahali hapo kumweka chini ya ulinzi wa neema ya Bwana, akaondoka.
41他走遍了叙利亚、基利家,坚固众教会。
41Katika safari hiyo alipitia Siria na Kilikia akiyaimarisha makanisa.