聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Acts

22

1“各位父老弟兄,请听听我现在对你们的申辩。”
1"Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni sasa nikijitetea mbele yenu!"
2他们听见保罗用希伯来语说话,就更加安静了。保罗说:
2Waliposikia akiongea nao kwa Kiebrania wakazidi kukaa kimya zaidi kuliko hapo awali. Naye Paulo akaendelea kusema,
3“我是犹太人,生在基利家的大数,在城里长大,按照我们祖宗律法的严格要求,在迦玛列门下受教,我为 神热心,好像你们大家今天一样。
3"Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia. Lakini nililelewa papa hapa mjini Yerusalemu chini ya mkufunzi Gamalieli. Nilifundishwa kufuata kwa uthabiti Sheria ya wazee wetu. Nilijitolea kwa moyo wote kwa Mungu kama ninyi wenyewe mlivyo hivi leo.
4我曾经迫害信奉这道的人直至死地,把男男女女都捆绑起来,送进监狱,
4Niliwatesa hata kuwaua wale watu waliofuata Njia hii. Niliwatia nguvuni wanaume kwa wanawake na kuwafunga gerezani.
5这是大祭司和全公议会都可以给我作证的。我也从他们那里得到了写给众弟兄的信,就去大马士革,要把那里的人捆绑起来,带到耶路撒冷接受惩罚。
5Kuhani Mkuu na baraza lote la wazee wanaweza kushuhudia jambo hilo. Kutoka kwao nilipokea barua walioandikiwa wale ndugu Wayahudi waliokuwa huko Damasko. Nilikwenda Damasko ili niwatie nguvuni watu hao na kuwaleta wamefungwa mpaka Yerusalemu ili waadhibiwe.
6保罗自述信主经过“约在正午,当我走近大马士革的时候,忽然有大光从天上向我四面照射,
6"Basi, nilipokuwa njiani karibu kufika Damasko, yapata saa sita mchana, mwangu mkubwa kutoka mbinguni ulitokea ghafla ukaniangazia pande zote.
7我仆倒在地上,听见有声音对我说:‘扫罗,扫罗,你为什么迫害我?’
7Hapo nilianguka chini, nikasikia sauti ikiniambia: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?
8我回答:‘主啊,你是谁?’他说:‘我就是你所迫害的拿撒勒人耶稣。’
8Nami nikauliza: Nani wewe, Bwana? Naye akaniambia: Mimi ni Yesu wa Nazareti ambaye wewe unamtesa.
9跟我在一起的人,只看见那光,却听不清楚那位对我说话的声音。
9Wale wenzangu waliuona ule mwanga lakini hawakusikia sauti ya yule aliyeongea nami.
10我说:‘主啊,我应当作什么呢?’主说:‘起来,进大马士革去,在那里有人会把指定给你作的一切事告诉你。’
10Basi, mimi nikauliza: Nifanye nini Bwana? Naye Bwana akaniambia: Simama, nenda Damasko na huko utaambiwa yote ambayo umepangiwa kufanya.
11因为那光太强烈,我的眼睛就瞎了,跟我在一起的人就牵着我的手,进了大马士革。
11Kutokana na ule mwanga mkali sikuweza kuona na hivyo iliwabidi wale wenzangu kuniongoza kwa kunishika mkono mpaka nikafika Damasko.
12“有一个人名叫亚拿尼亚的,他是一个虔诚而遵守律法的人,当地所有的犹太人都称赞他。
12"Huko kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Anania, mtu mcha Mungu, mwenye kuitii Sheria yetu na aliyeheshimika sana mbele ya Wayahudi waliokuwa wanaishi Damasko.
13他来见我,站在我旁边,对我说:‘扫罗弟兄,你现在可以看见了。’我立刻往上一看,看见了他。
13Yeye alikuja kuniona, akasimama karibu nami, akasema: Ndugu Saulo! Ona tena. Papo hapo nikaona tena, nikamwangalia.
14他又说:‘我们祖先的 神选派了你,让你明白他的旨意,看见那义者,听见他口中的声音。
14Halafu Anania akasema: Mungu wa babu zetu amekuchagua upate kujua matakwa yake na kumwona yule mtumishi wake mwadilifu na kumsikia yeye mwenyewe akiongea.
15因为你要把所看见所听见的,向万人为他作见证。
15Kwa maana utamshuhudia kwa watu wote ukiwaambia yale uliyoyaona na kuyasikia.
16现在你为什么还耽搁呢?起来受洗,求告他的名,洗净你的罪吧。’
16Sasa basi, ya nini kukawia zaidi? Simama ubatizwe na uondolewe dhambi zako kwa kuliungama jina lake.
17保罗蒙差遣向外族人传福音“后来,我回到耶路撒冷,在殿里祷告的时候,魂游象外,
17"Basi, nilirudi Yerusalemu, na nilipokuwa nikisali Hekaluni, niliona maono.
18看见主对我说:‘你要快快离开耶路撒冷,因为你为我作的见证,他们是不会接受的。’
18Nilimwona Bwana akiniambia: Haraka! Ondoka Yerusalemu upesi kwa maana watu wa hapa binadamu hawataukubali ushuhuda wako juu yangu.
19我说:‘主啊,他们知道我曾把信你的人监禁起来,又在各会堂拷打他们,
19Nami nikamjibu: Bwana, wao wanajua wazi kwamba mimi ni yule aliyekuwa anapitapita katika masunagogi na kuwatia nguvuni na kuwapiga wale waliokuwa wanakuamini.
20并且你的见证人司提反受害流血的时候,我也亲自在场,表示同意,并且为杀他的人看守衣服。’
20Na kwamba wakati shahidi wako Stefano alipouawa, mimi binafsi nilikuwako pale nikakubaliana na kitendo hicho na kuyalinda makoti ya wale waliokuwa wanamuua.
21他对我说:‘你走吧,我要派你到远方的外族人那里去。’”
21Naye Bwana akaniambia: Nenda; ninakutuma mbali kwa mataifa mengine."
22保罗与千夫长众人听见他说到这句话,就高声说:“这样的人应该从地上除掉,不应该活着!”
22Mpaka hapa, wale watu walikuwa wanamsikiza, lakini aliposema maneno haya, walianza kusema kwa sauti kubwa, "Mwondoe duniani! Mtu wa namna hiyo hastahili kuishi."
23大家正在喊叫着,拋掷衣服,向空中扬灰撒土的时候,
23Waliendelea kupayukapayuka huku wakitikisa makoti yao na kurusha vumbi angani.
24千夫长下令把保罗带到营楼去,吩咐人用鞭子拷问他,要知道群众为什么这样向他喊叫。
24Mkuu wa jeshi aliwaamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome, akawaambia wamchape viboko ili wapate kujua kisa cha Wayahudi kumpigia kelele.
25士兵正用皮带绑他的时候,保罗对站在旁边的百夫长说:“你们鞭打一个还没有定罪的罗马公民,是合法的吗?”
25Lakini walipokwisha mfunga ili wamchape viboko, Paulo alimwuliza jemadari mmoja aliyesimama hapo, "Je, ni halali kwenu kumpiga viboko raia wa Roma kabla hajahukumiwa?"
26百夫长听了,就去报告千夫长,说:“这个人是罗马公民,你要怎么办呢?”
26Yule jemadari aliposikia hayo, alimpasha habari mkuu wa jeshi akisema, "Unataka kufanya nini? Mtu huyu ni raia wa Roma!"
27千夫长就来问保罗:“告诉我,你是罗马公民吗?”他说:“是的。”
27Basi, mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamwambia, "Niambie; je, wewe ni raia wa Roma?" Paulo akamjibu, "Naam."
28千夫长说:“我花了一大笔钱,才取得罗马籍。”保罗说:“我生下来就是罗马公民。”
28Mkuu wa jeshi akasema, "Mimi nami nimekuwa raia wa Roma kwa kulipa gharama kubwa." Paulo akasema, "Lakini mimi ni raia wa Roma kwa kuzaliwa."
29于是那些要拷问他的人,立刻离开他走了。千夫长既知道他是罗马公民,又因捆绑过他,就害怕起来。
29Wale watu ambao walikuwa tayari kumchunguza Paulo walitoweka mara. Hata yule mkuu wa jeshi aliogopa alipojua kwamba Paulo ni raia wa Roma na kwamba alikuwa amekwisha mfunga minyororo.
30保罗在公议会面前申辩第二天,千夫长为要知道犹太人控告保罗的真相,就解开他,召集了祭司长和公议会全体在一起,把保罗带下来,叫他站在他们面前。
30Kesho yake, mkuu wa jeshi alitaka kujua mashtaka kamili ambayo Wayahudi walikuwa wamemwekea Paulo. Hivyo, alimfungua Paulo minyororo, akaamuru makuhani wakuu na Baraza lote wafanye kikao. Kisha alimleta Paulo, akamsimamisha mbele ya Baraza.