1彼得医好瘸腿的人
1Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
2有一个生来瘸腿的人被人抬来。他们天天把他放在那名叫美门的殿门口,让他好向进殿的人讨饭。
2Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao "Mlango Mzuri", palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
3他看见彼得和约翰将要进殿,就向他们讨饭。
3Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
4彼得和约翰定睛看着他,彼得说:“你看我们!”
4Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, "Tutazame!"
5那人就留意看着他们,希望从他们得些什么。
5Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6彼得却说:“金银我都没有,只把我有的给你:我奉拿撒勒人耶稣基督的名,吩咐你行走!”
6Kisha Petro akamwambia, "Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!"
7于是拉着他的右手,扶他起来;他的脚和踝骨立刻强壮有力,
7Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
8他一跳就站了起来,并且行走。他连走带跳,赞美 神,同他们进入殿中。
8Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
9群众看见他一边走一边赞美 神;
9Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
10他们一认出他就是那平时坐在圣殿美门口讨饭的,就因所经历的事,满心希奇,惊讶不已。
10Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule "Mlango Mzuri" wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
11彼得在所罗门廊下的讲道那人拉着彼得和约翰的时候,群众都很惊奇,跑到他们那里,就是所罗门廊的下面。
11Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa "Ukumbi wa Solomoni," ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
12彼得看见了,就对群众说:“以色列人哪,为什么因这事希奇呢?为什么瞪着我们,好像我们是凭着自己的能力和虔诚,使这人行走呢?
12Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, "Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
13亚伯拉罕、以撒、雅各的 神,就是我们祖宗的 神,荣耀了他的仆人耶稣。这位耶稣,你们把他送交官府。彼拉多本来定意要放他,你们却当着彼拉多的面拒绝他。
13Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
14你们把那圣者义者拒绝了,反而要求给你们释放一个杀人犯。
14Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
15你们杀了那‘生命的源头’, 神却使他从死人中复活。我们就是这件事的见证人。
15Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
16是他的名(因信他的名)使你们所看见所认识的这个人强壮了。这从耶稣而来的信心,当着你们众人面前,把他完全医好了。
16Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
17弟兄们,我知道你们所作的,是出于无知,你们的官长也是这样。
17"Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
18但 神曾经借着众先知的口,预先宣告他所立的基督将要受害的事,就这样应验了。
18Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
19所以你们应当悔改归正,使你们的罪得着涂抹。
19Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
20这样,那安乐的日子,必从主面前来到,并且他必把为你们预先选定的基督(耶稣)差来。
20Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
21他必留在天上,直到万物复兴的时候,就是 神自古借着圣先知的口所说的。
21Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani.
22摩西曾说:‘你们的主 神要从你们弟兄中间,给你们兴起一位先知像我;无论他对你们说什么,你们都应当听从。
22Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
23无论谁不听从那位先知,必定从民中灭绝。’
23Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
24所有从撒母耳起,以及相继兴起来讲话的先知,都曾经宣告这些日子。
24Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
25你们是先知的子孙,也是承受 神向你们祖先所立之约的人。 神曾经对亚伯拉罕说:‘地上万族,都要因你的后裔得福。’
25Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
26 神先给你们兴起他的仆人,差他来祝福你们,使你们各人回转,离开邪恶。”
26Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake."