聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Acts

2

1五旬节圣灵降临
1Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
2忽然有一阵好像强风吹过的响声,从天而来,充满了他们坐在里面的整间屋子。
2Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
3又有火焰般的舌头显现出来,分别落在他们各人身上。
3Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
4他们都被圣灵充满,就照着圣灵所赐给他们的,用别种的语言说出话来。
4Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
5那时住在耶路撒冷的,有从天下各国来的虔诚的犹太人。
5Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
6这声音一响,许多人都聚了来,人人都听见门徒讲出听众各人本乡的话,就莫名其妙。
6Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7他们又惊讶、又惊奇,说:“你看,这些说话的,不都是加利利人吗?
7Walistaajabu na kushangaa, wakisema, "Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
8我们各人怎么听见他们讲我们从小所用的本乡话呢?
8Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
9我们帕提亚人、玛代人、以拦人和住在美索不达米亚、犹太、加帕多家、本都、亚西亚、
9Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
10弗吕家、旁非利亚、埃及,并靠近古利奈的利比亚一带地方的人,客居罗马的犹太人和归信犹太教的人,
10Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
11克里特人以及阿拉伯人,都听见他们用我们的语言,讲说 神的大作为。”
11Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu."
12众人还在惊讶迷惘的时候,彼此说:“这是什么意思?”
12Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, "Hii ina maana gani?"
13另有些人讥笑说:“他们是给新酒灌醉了。”
13Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, "Watu hawa wamelewa divai mpya!"
14彼得在五旬节的讲道彼得和十一使徒站起来,他高声对众人说:“犹太人和所有住在耶路撒冷的人哪,你们应当明白这件事,也应该留心听我的话。
14Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: "Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
15这些人并不是照你们所想的喝醉了,现在不过是上午九点钟罢了。
15Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
16这正是约珥先知所说的:
16Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
17‘ 神说:在末后的日子,我要把我的灵浇灌所有的人,你们的儿女要说预言,你们的青年人要见异象,你们的老年人要作异梦。
17Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18在那些日子,我也要把我的灵浇灌我的仆人和使女,他们就要说预言。
18Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
19我要在天上显出奇事,在地上显出神迹,有血、有火、有烟雾;
19Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
20太阳将变为黑暗,月亮将变为血红,在主伟大显赫的日子临到以前,这一切都要发生。
20jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
21那时,凡求告主名的,都必得救。’
21Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
22“以色列人哪,请听听这几句话:正如你们所知道的, 神已经借着拿撒勒人耶稣在你们中间施行了大能、奇事、神迹,向你们证明他是 神所立的。
22"Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
23他照着 神的定旨和预知被交了出去,你们就借不法之徒的手,把他钉死了。
23Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
24 神却把死的痛苦解除,使他复活了,因为他不能被死亡拘禁。
24Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
25大卫指着他说:‘我时常看见主在我面前,因他在我右边,我必不会动摇。
25Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
26为此我的心快乐,我的口舌欢呼,我的肉身也要安居在盼望中。
26Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
27因你必不把我的灵魂撇在阴间,也必不容你的圣者见朽坏。
27kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze.
28你已经把生命之路指示了我,必使我在你面前有满足的喜乐。’
28Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
29“弟兄们,关于祖先大卫的事,我不妨坦白告诉你们,他死了,葬了,直到今日他的坟墓还在我们这里。
29"Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
30他是先知,既然知道 神向他起过誓,要从他的后裔中立一位,坐在他的宝座上,
30Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
31又预先看见了这事,就讲论基督的复活说:‘他不会被撇在阴间,他的肉身也不见朽坏。’
31Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza.
32这位耶稣, 神已经使他复活了,我们都是这事的见证人。
32Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
33他既然被高举到 神的右边,从父领受了所应许的圣灵,就把他浇灌下来,这就是你们所看见所听见的。
33Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
34大卫并没有升到天上,他却说:‘主对我主说:你坐在我的右边,
34Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
35等我使你的仇敌作你的脚凳。’
35hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
36因此,以色列全家应当确实知道,你们钉在十字架上的这位耶稣, 神已经立他为主为基督了。”
36"Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo."
37他们听了以后,觉得扎心,就对彼得和其余的使徒说:“弟兄们,我们应当作什么呢?”
37Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: "Ndugu zetu, tufanye nini?"
38彼得说:“你们应当悔改,并且每一个人都要奉耶稣基督的名受洗,使你们的罪得赦,就必领受所赐的圣灵。
38Petro akajibu, "Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
39这应许原是给你们和你们的儿女,以及所有在远方的人,就是给凡是我们主 神召来归他的人。”
39Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake."
40彼得还用许多别的话,郑重作证,并且劝勉他们,说:“你们应当救自己脱离这弯曲的世代!”
40Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, "Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu."
41于是接受他话的人都受了洗,那一天门徒增加了约三千人。
41Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
42他们恒心遵守使徒的教训,彼此相通、擘饼和祈祷。
42Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
43信徒的团契生活使徒行了许多奇事神迹,众人就都惧怕。
43Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
44所有信的人都在一起,凡物公用,
44Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
45并且变卖产业和财物,按照各人的需要分给他们。
45Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
46他们天天同心在殿里恒切地聚集,一家一家地擘饼,存着欢乐和诚恳的心用饭,
46Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
47又赞美 神,并且得到全民的喜爱。主将得救的人,天天加给教会。
47Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.