聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Acts

1

1吩咐门徒等候圣灵
1Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2一直到他借着圣灵吩咐所拣选的使徒之后,被接上升的日子为止。
2mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3他受难以后,用许多凭据向使徒显示自己是活着的。他向使徒显现,并且讲论 神的国的事,有四十天之久。
3Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4耶稣和他们一同吃饭的时候,吩咐他们不要离开耶路撒冷,说:“你们要等候父的应许,就是你们听我讲过的,
4Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: "Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5约翰是用水施洗,但再过几天,你们要受圣灵的洗。”
5Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu."
6耶稣升天他们聚集的时候,问耶稣说:“主啊,你要在这时候使以色列复国吗?”
6Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, "Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?"
7耶稣说:“父凭着自己的权柄所定的时间或日期,你们不必知道。
7Lakini Yesu akawaambia, "Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8可是圣灵降临在你们身上,你们就必领受能力,并且要在耶路撒冷、犹太全地、撒玛利亚,直到地极,作我的见证人。”
8Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia."
9说完了,他们还在看的时候,他被接上升,有一朵云把他接去,就看不见他了。
9Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10当他往上升,他们定睛望天的时候,忽然有两个人,身穿白衣,站在他们旁边,说:
10Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11“加利利人哪,为什么站着望天呢?这位被接升天离开你们的耶稣,你们看见他怎样往天上去,他也要怎样回来。”
11wakasema, "Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni."
12选出马提亚作使徒后来,他们从橄榄山回到耶路撒冷。那山靠近耶路撒冷,有一安息日可走的路程。
12Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13他们进了城,上了一间楼房,就是彼得、约翰、雅各、安得烈、腓力、多马、巴多罗迈、马太、亚勒腓的儿子雅各、激进派的西门、雅各的儿子犹大等人所住的。
13Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14这些人和几个妇女,耶稣的母亲马利亚,还有他的兄弟们,都在一起,同心地恒切祷告。
14Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15那时,约有一百二十人聚会,彼得在众弟兄中间站起来说:
15Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16“弟兄们,经上的话,就是圣灵借着大卫的口,预言那领人捉拿耶稣的犹大的事,是一定会应验的。
16akasema, "Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17他本是我们中间的一个,一同领受了这职分。
17Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18他用不义的酬劳买了一块田,结果倒头栽了下去,腹破肠流。
18("Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19这事住在耶路撒冷的人全都知道,所以按当地的话,那块地称为亚革大马,意思就是‘血田’。
19Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20因为诗篇上写着:‘愿他的住处变为荒场,无人居在其中。’又说:‘愿别人取代他的职分。’
20Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21所以,从约翰施洗起,直到主离开我们被接上升的那天为止,当他在我们中间来往的时候,那些跟我们常在一起的人中,应该有一个人出来与我们一同作耶稣复活的见证人。”
21Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22
22Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni."
23于是他们提出两个人:约瑟(号称巴撒巴,又名犹士都)和马提亚,
23Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24就祷告说:“主啊!你知道万人的心,求你从这两个人中,指明你要拣选谁,
24Kisha wakasali: "Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25来承担这使徒的职位和工作。这职位犹大已经放弃,往他自己的地方去了。”
25ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe."
26大家就为他们抽签,结果抽中了马提亚,他就与十一使徒同列。
26Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.