聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

21

1耶稣在海边向七个门徒显现
1Baada ya hayo Yesu aliwatokea tena wanafunzi wake kando ya ziwa Tiberia. Aliwatokea hivi:
2当时西门.彼得、称为“双生子”的多马、加利利的迦拿人拿但业、西庇太的两个儿子,和另外两个门徒都聚在一起。
2Simoni Petro, Thoma (aitwaye Pacha), na Nathanieli mwenyeji wa Kana Galilaya, wana wawili wa Zebedayo na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa wote pamoja.
3西门.彼得对他们说:“我要打鱼去。”他们说:“我们也跟你一起去。”于是他们出去,上了船,可是那一夜他们并没有打到什么。
3Simoni Petro aliwaambia, "Nakwenda kuvua samaki." Nao wakamwambia, "Nasi tutafuatana nawe." Basi, wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakupata chochote.
4清早的时候,耶稣站在岸边;门徒却不知道他就是耶稣。
4Kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakujua kwamba alikuwa yeye.
5耶稣对他们说:“孩子们,打到鱼没有?”他们回答:“没有。”
5Basi, Yesu akawauliza, "Vijana, hamjapata samaki wowote sio?" Wao wakamjibu, "La! Hatujapata kitu."
6耶稣说:“把网撒在船的右边,就可以得着。”他们就把网撒下去,可是拉不上来,因为鱼太多。
6Yesu akawaambia, "Tupeni wavu upande wa kulia wa mashua nanyi mtapata samaki." Basi, wakatupa wavu lakini sasa hawakuweza kuuvuta tena kwa wingi wa samaki.
7耶稣所爱的那门徒对彼得说:“是主!”西门.彼得一听见是主,就立刻束上外衣(因为他当时赤着身子),纵身跳进海里。
7Hapo yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, "Ni Bwana!" Simoni Petro aliposikia ya kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa), akarukia majini.
8其他的门徒,因为离岸不远(约有一百公尺),就坐在小船上,把那网鱼拖过来。
8Lakini wale wanafunzi wengine walikuja pwani kwa mashua huku wanauvuta wavu uliojaa samaki; hawakuwa mbali na nchi kavu, ila walikuwa yapata mita mia moja kutoka ukingoni.
9他们上了岸,就看见那里有一堆炭火,上面有鱼有饼。
9Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.
10耶稣对他们说:“把你们刚才打的鱼拿几条来。”
10Yesu akawaambia, "Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua."
11西门.彼得就上船,把网拉到岸上;那网满了大鱼,共有一百五十三条。鱼虽然这么多,网却没有破。
11Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa mia moja na hamsini na watatu. Na ingawa walikuwa wengi hivyo wavu haukukatika.
12耶稣对他们说:“你们来,吃早饭吧。”门徒中没有一个人敢问他:“你是谁?”因为知道他是主。
12Yesu akawaambia, "Njoni mkafungue kinywa." Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza: "Wewe ni nani?" Maana walijua alikuwa Bwana.
13耶稣走过来,拿饼递给他们,又照样拿鱼递给他们。
13Yesu akaja, akatwaa mkate akawapa; akafanya vivyo hivyo na wale samaki.
14这是耶稣从死人中复活之后,第三次向门徒显现。
14Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kutoka wafu.
15耶稣三次问彼得是否爱他他们吃了早饭,耶稣问西门.彼得:“约翰的儿子西门,你爱我比这些更深吗?”他回答:“主啊,是的,你知道我爱你。”耶稣说:“你喂养我的小羊。”
15Walipokwisha kula, Yesu alimwuliza Simoni Petro, "Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi zaidi kuliko hawa?" Naye akajibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza wana kondoo wangu."
16耶稣第二次又问他:“约翰的儿子西门,你爱我吗?”他回答:“主啊,是的,你知道我爱你。”耶稣说:“你牧养我的羊。”
16Kisha akamwambia mara ya pili, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Petro akamjibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu."
17耶稣第三次问他:“约翰的儿子西门,你爱我吗?”彼得因为耶稣第三次问他:“你爱我吗?”就忧愁起来,对耶稣说:“主啊,你是无所不知的,你知道我爱你。”耶稣说:“你喂养我的羊。
17Akamwuliza mara ya tatu, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Hapo Petro akahuzunika kwa sababu alimwuliza mara ya tatu: "Wanipenda?" akamwambia, "Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu!
18我实实在在告诉你,你年轻的时候,自己束上腰带,随意往来;但到了年老的时候,你要伸出手来,别人要把你绑着,带你到你不愿意去的地方。”
18Kweli nakwambia, ulipokuwa kijana ulizoea kujifunga mshipi na kwenda kokote ulikotaka. Lakini utakapokuwa mzee utanyosha mikono yako, na mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikopenda kwenda."
19耶稣说这话,是指明彼得将怎样死,来荣耀 神。说了这话,就对彼得说:“你跟从我吧!”
19(Kwa kusema hivyo, alionyesha jinsi Petro atakavyokufa na kumtukuza Mungu.) Kisha akamwambia, "Nifuate."
20耶稣所爱的那门徒彼得转过身来,看见耶稣所爱的那门徒跟着,就是在晚饭的时候,靠着耶稣的胸膛,问“主啊,出卖你的是谁?”的那个人。
20Hapo Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda, anafuata (Huyu mwanafunzi ndiye yule ambaye wakati wa chakula cha jioni, alikaa karibu sana na Yesu na kumwuliza: "Bwana ni nani atakayekusaliti?")
21彼得看见他,就问耶稣:“主啊,这个人将来怎么样?”
21Basi, Petro alipomwona huyo akamwuliza Yesu, "Bwana, na huyu je?"
22耶稣回答他:“如果我要他活到我来的时候,跟你有什么关系呢?你只管跟从我吧!”
22Yesu akamjibu, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini? Wewe nifuate mimi."
23于是这话流传在弟兄中间,说那门徒不会死。其实耶稣并没有说他不会死,只是说:“如果我要他活到我来的时候,跟你有什么关系呢?”
23Basi, habari hiyo ikaenea miongoni mwa wale ndugu kwamba mwanafunzi huyo hafi. Lakini Yesu hakumwambia kwamba mwanafunzi huyo hafi, ila, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini?"
24为这些事作证,并且记述这些事的,就是这门徒;我们知道他的见证是真实的。
24Huyo ndiye yule aliyeshuhudia mambo haya na kuyaandika. Nasi twajua kwamba aliyoyasema ni kweli.
25耶稣所行的,还有许多其他的事;如果都一一写下来,所要写成的书,我想就是这个世界也容不下了。
25Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.