聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Acts

6

1选出七位执事
1Baadaye, idadi ya wanafunzi ilipokuwa inazidi kuongezeka, kulitokea manung'uniko kati ya wanafunzi waliosema Kigiriki na wale waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigiriki walinung'unika kwamba wajane wao walikuwa wanasahauliwa katika ugawaji wa mahitaji ya kila siku.
2于是十二使徒召集了众门徒,说:“要我们放下 神的道,去管理伙食,是不合适的。
2Kwa hiyo, mitume kumi na wawili waliita jumuiya yote ya wanafunzi, wakasema, "Si vizuri sisi tuache kulihubiri neno la Mungu ili tushughulikie ugawaji wa mahitaji.
3所以弟兄们,应当从你们中间选出七个有好见证、满有圣灵和智慧的人,我们就派他们负责这事。
3Hivyo, ndugu zetu, chagueni miongoni mwenu watu saba wenye sifa njema, waliojawa na Roho na wenye hekima; nasi tutawakabidhi jukumu hilo.
4至于我们,我们要专心祈祷、传道。”
4Sisi, lakini, tutashughulika na sala na kazi ya kuhubiri neno la Mungu."
5这个意见全会众都很满意,于是选出司提反,他是一位满有信心和圣灵的人,还有腓利、伯罗哥罗、尼加挪、提门、巴米拿,以及归信犹太教的安提阿人尼哥拉,
5Jambo hilo likaipendeza jumuiya yote ya waumini. Wakawachagua Stefano, mtu mwenye imani kubwa na mwenye kujawa na Roho Mtakatifu, Filipo, Prokoro, Nikanora, Timona, Parmena na Nikolao wa Antiokia ambaye hapo awali alikuwa ameongokea dini ya Kiyahudi.
6叫他们站在使徒面前。使徒祷告后,就为他们按手。
6Wakawaweka mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono.
7 神的道传开了;在耶路撒冷,门徒人数大大增加,有很多祭司也信从了真道。
7Neno la Mungu likazidi kuenea na idadi ya waumini huko Yerusalemu ikaongezeka zaidi, na kundi kubwa la makuhani wakaipokea imani.
8司提反被捕司提反满有恩惠能力,在民间施行大奇事和神迹。
8Mungu alimjalia Stefano neema tele, akampa nguvu nyingi hata akawa anatenda miujiza na maajabu kati ya watu.
9当时有几个称为“自由人”会堂的人,就是从古利奈和亚历山太来的人,另外还有基利家人和亚西亚人,他们出面与司提反辩论,
9Lakini watu fulani wakatokea ili wabishane na Stefano. Baadhi ya watu hao walikuwa wa sunagogi moja lililoitwa "Sunagogi la Watu Huru", nao walitoka Kurene na Aleksandria; wengine walitoka Kilikia na Asia.
10但司提反靠着圣灵和智慧说话,他们就抵挡不住。
10Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyeongoza maneno yake.
11于是他们唆使众人,说:“我们听过他说谤渎摩西和 神的话。”
11Kwa hiyo waliwahonga watu kadhaa waseme: "Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kumkashifu Mose na kumkashifu Mungu."
12又煽动民众、长老、经学家,这些人就来捉拿他,把他带到公议会,
12Kwa namna hiyo, waliwachochea watu, wazee na walimu wa Sheria. Basi, wakamjia Stefano, wakamkamata na kumleta mbele ya Baraza kuu.
13并且造了假的证供说:“这人不断抨击圣地和律法。
13Walileta Barazani mashahidi wa uongo ambao walisema, "Mtu huyu haachi kamwe kusema maneno ya kupakashifu mahali hapa patakatifu na Sheria ya Mose.
14我们听他说过:‘这拿撒勒人耶稣要毁坏这地方,改变摩西传给我们的规例。’”
14Kwa maana tulikwisha msikia akisema eti huyo Yesu wa Nazareti atapaharibu kabisa mahali hapa na kufutilia mbali desturi zile tulizopokea kutoka kwa Mose."
15当时,坐在公议会里的人,都注视他,见他的面貌像天使一样。
15Wote waliokuwa katika kile kikao cha Baraza walimkodolea macho Stefano, wakauona uso wake umekuwa kama wa malaika.