聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Colossians

1

1问安
1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
2写信给在歌罗西的圣徒,和在基督里忠心的弟兄。愿恩惠平安从我们的父 神临到你们。
2tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3为歌罗西信徒感谢 神我们为你们祈祷的时候,常常感谢 神我们主耶稣基督的父,
3Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
4因为听见你们在基督耶稣里的信心,和对众圣徒的爱心。
4Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
5这都是由于那给你们存在天上的盼望,这盼望是你们从前在福音真理的道上听过的。
5Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
6这福音传到你们那里,也传到全世界;你们听了福音,因着真理确实认识了 神的恩典之后,这福音就在你们中间不断地结果和增长,在全世界也是一样。
6Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
7这福音也就是你们从我们亲爱的、一同作仆人的以巴弗那里学到的。他为你们作了基督忠心的仆役,
7Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8也把你们在圣灵里的爱心告诉了我们。
8Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
9保罗的祈祷因此,我们从听见的那天起,就不停地为你们祷告祈求,愿你们借着一切属灵的智慧和悟性,可以充分明白 神的旨意,
9Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
10使你们行事为人对得起主,凡事蒙他喜悦;在一切善事上多结果子,更加认识 神;
10Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
11依照他荣耀的大能得着一切能力,带着喜乐的心,凡事忍耐宽容;
11Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
12并且感谢父,他使你们有资格分享圣徒在光明中的基业。
12Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
13他救我们脱离了黑暗的权势,把我们迁入他爱子的国里。
13Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
14我们在爱子里蒙了救赎,罪得赦免。
14ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
15基督在万有之上这爱子是那看不见的 神的形象,是首先的,在一切被造的之上。
15Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16因为天上地上的万有:看得见的和看不见的,无论是坐王位的,或是作主的,或是执政的,或是掌权的,都是本着他造的;万有都是借着他,又是为着他而造的。
16Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
17他在万有之先;万有也一同靠着他而存在。
17Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
18他是身体的头,这身体就是教会。他是元始,是死人中首先复生的,好让他在凡事上居首位;
18Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
19因为 神乐意使所有的丰盛都住在爱子里面,
19Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
20并且借着他在十字架上所流的血成就了和平,使万有,无论是地上天上的,都借着他与 神和好了。
20Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
21虽然你们从前也是和 神隔绝,心思上与他为敌,行为邪恶,
21Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
22但现今 神在爱子的肉身上,借着他的死,使你们与 神和好了,为了要把你们这些圣洁、无瑕疵、无可指摘的人,呈献在他面前。
22Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
23只是你们要常存信心,根基稳固,不受动摇偏离福音的盼望。这福音你们听过了,也传给了天下万民;我保罗也作了这福音的仆役。
23Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
24竭力传扬 神的奥秘现在我为你们受苦,我觉得喜乐;为了基督的身体,就是为了教会,我要在自己的肉身上,补满基督苦难的不足。
24Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
25我照着 神为你们而赐给我的管家职分,作了教会的仆役,要把 神的道,就是历世历代隐藏的奥秘,传得完备。现在这奥秘已经向他的众圣徒显明了。
25Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
26
26ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake.
27 神愿意使他们知道这奥秘在外族人中有多么荣耀的丰盛,这奥秘就是基督在你们里面成了荣耀的盼望。
27Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
28我们传扬他,是用各样的智慧,劝戒各人,教导各人,为了要使各人在基督里得到完全。
28Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
29我也为了这事劳苦,按着他用大能在我心中运行的动力,竭力奋斗。
29Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.