1我愿意你们知道,我为你们和在老底嘉的人,以及所有没有跟我见过面的人,是怎样竭力奋斗,
1Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
2为的是要他们的心得着勉励,在爱中彼此联系,可以得着凭悟性、因确信而来的一切丰盛,也可以充分认识 神的奥秘,这奥秘就是基督;
2Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
3一切智慧和知识的宝库都蕴藏在基督里面。
3Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
4我说这些话,免得有人用花言巧语欺骗你们。
4Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
5我虽然不在你们那里,心却与你们同在。我看见你们循规蹈矩,并且对基督有坚定的信心,就欢喜了。
5Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
6在基督里得丰盛你们怎样接受了基督耶稣为主,就当照样在他里面行事为人,
6Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
7按着你们所学到的,在他里面扎根、建造,信心坚定,满有感谢的心。
7Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
8你们要谨慎,免得有人不照着基督,而照着人的传统,和世俗的言论,借着哲学和骗人的空谈,把你们掳去。
8Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
9因为 神本性的一切丰盛,都有形有体地住在基督里面,
9Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
10你们也是在他里面得了丰盛。他是一切执政掌权者的元首。
10nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
11你们也在他里面受了不是由人手所行的割礼,而是受了基督的割礼,就是除掉你们的罪身。
11Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
12你们在洗礼中已经与他一同埋葬,也在洗礼中,因信那使基督从死人中复活的 神所运行的动力,与他一同复活了。
12Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
13你们因着过犯和肉体未受割礼,原是死的,然而 神赦免了我们的一切过犯,使你们与基督一同活过来,
13Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
14涂抹了那写在规条上反对我们、与我们为敌的字句,并且把这字句从我们中间拿去,钉在十字架上。
14alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
15他既然靠着十字架胜过了一切执政掌权的,废除了他们的权势,就在凯旋的行列中,把他们公开示众。
15Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
16所以不要让人因着饮食、节期、月朔、安息日批评你们,
16Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
17这些不过是将来的事的影子,那真体却是属于基督的。
17Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
18不要让人夺去你们的奖赏,他们以故意谦卑,敬拜天使为乐;迷于自己所见过的;凭着肉体的意念,无故地自高自大;
18Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
19不与头紧密相连。其实全身都是借着关节和筋络从头得着供应和联系,就照着 神所要求的,生长起来。
19na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
20在基督里作新人你们若与基督一同死了,脱离了世俗的言论,为什么仍然好像活在世俗中一样,
20Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
21拘守那“不可摸、不可尝、不可触”的规条呢?
21"Msishike hiki," "Msionje kile," "Msiguse kile!"
22(这一切东西,一经使用,就都朽坏了。)这些规条是照着人的命令和教训而定的,
22Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
23在随着己意敬拜,故作谦卑,和苦待己身等事上,似乎是智慧之言,其实只能叫人放纵肉体,再没有任何价值。
23Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.