聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Colossians

3

1所以,你们既然与基督一同复活,就应当寻求天上的事,那里有基督坐在 神的右边。
1Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
2你们要思念的,是天上的事,不是地上的事。
2Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
3因为你们已经死了,你们的生命与基督一同隐藏在 神里面。
3Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4基督就是你们的生命,他显现的时候,你们也要和他一同在荣耀里显现。
4Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
5所以要治死你们在地上的肢体,就如淫乱、污秽、邪情、恶欲和贪心,贪心就是拜偶像。
5Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
6因着这些事, 神的忿怒必要临到悖逆的人(有些抄本无“悖逆的人”)。
6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
7你们从前在其中生活的时候,也曾经这样行过。
7Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
8但现在你们要除去忿怒、恼怒、恶毒、毁谤,以及粗言秽语这一切事。
8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
9不要彼此说谎,因为你们已经脱去了旧人和旧人的行为,
9Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
10穿上了新人。这新人照着他的创造者的形象渐渐更新,能够充分认识主。
10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
11在这一方面,并不分希腊人和犹太人,受割礼的和未受割礼的,未开化的人和西古提人,奴隶和自由人,唯有基督是一切,也在一切之内。
11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
12所以,你们既然是 神所拣选的,是圣洁、蒙爱的人,就要存怜悯的心肠、恩慈、谦卑、温柔和忍耐。
12Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13如果有人对别人有嫌隙,总要彼此宽容,互相饶恕;主怎样饶恕了你们,你们也要照样饶恕人。
13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
14在这一切之上,还要有爱心,爱心是联系全德的。
14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
15又要让基督的平安在你们心里作主;你们蒙召归为一体,也是为了这个缘故。你们要有感谢的心。
15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
16你们要让基督的道丰丰富富地住在你们心里,以各样的智慧,彼此教导,互相劝戒,用诗章、圣诗、灵歌,怀着感恩的心歌颂 神。
16Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
17凡你们所作的,无论是言语或行为,都要奉主耶稣的名,借着他感谢父 神。
17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
18过新人的生活你们作妻子的,要顺服丈夫,这在主里是合宜的。
18Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
19你们作丈夫的,要爱妻子,不可苦待她们。
19Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
20你们作儿女的,要凡事听从父母,因为这在主里是可喜悦的。
20Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
21你们作父亲的,不要激怒儿女,免得他们灰心丧志。
21Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
22你们作仆人的,要凡事听从世上的主人,作事不要只作给人看,像那些讨人欢心的一样,却要以真诚的心敬畏主。
22Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
23无论你们作什么,都要从心里去作,像是为主作的,不是为人作的,
23Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
24因为你们知道,你们一定会从主那里得到基业为赏赐。你们应当服事主基督,
24Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
25但那些不义的人,必按他所行的不义受报应。主并不偏待人。
25Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.