1你们作主人的,要公平地对待仆人,因为知道你们也有一位主在天上。
1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2训勉的话你们要恒切祷告,在祷告的时候存着感恩的心警醒;
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
3也要为我们祷告,求 神为我们开传道的门,宣讲基督的奥秘(我就是为了这个缘故被捆锁),
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
4使我照着我所应当说的,把这奥秘显明出来。
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
5你们要把握时机,用智慧与外人来往。
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
6你们的话要常常温和,好像是用盐调和的,使你们知道应当怎样回答各人。
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
7问候的话我的一切景况,推基古会告诉你们。他是我所爱的弟兄,是忠心的仆役,也是在主里同作仆人的。
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
8我派他到你们那里去,使你们知道我们的景况,并且安慰你们的心。
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
9他是跟欧尼西慕一同去的。欧尼西慕是忠心的亲爱的弟兄,是你们那里的人。他们会把这里的一切告诉你们。
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
10与我一同坐监的亚里达古,和巴拿巴的表弟马可,问候你们。(关于马可,你们已经受了吩咐:他若到你们那里,你们要接待他。)
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
11别号犹士都的耶数,也问候你们。在受过割礼的人中,只有这几位是为 神的国与我同工的,他们也成了我的安慰。
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
12以巴弗问候你们,他是你们那里的人,是基督耶稣的仆人;他祷告的时候,常常竭力为你们祈求,好使你们在 神的一切旨意中完全站稳,满有坚定的信念。
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
13我可以为他作证,他为了你们和在老底嘉、希拉波立的人,多受劳苦。
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
14亲爱的路加医生和底马问候你们。
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
15请问候在老底嘉的弟兄和宁法,以及在她家里的教会。
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
16这封信你们宣读了以后,也要交给老底嘉的教会宣读;你们也要读老底嘉的那封信。
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
17你们要对亚基布说:“你要留心在主里领受的职分,好把它完成。”
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
18我保罗亲笔问候你们。你们要记念我的捆锁。愿恩惠与你们同在。
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.