聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Ephesians

2

1出死入生
1Ninyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu.
2那时你们在过犯和罪恶中行事为人,随着时代的潮流,也服从空中掌权的首领,就是现今在悖逆的人身上运行的灵。
2Wakati ule mliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, mkawa mnamtii mtawala wa pepo wenye nguvu wa anga, pepo ambao huwatawala sasa watu wasiomtii Mungu.
3我们从前也都和他们在一起,放纵肉体的私欲,随着肉体和心意所喜好的去行;我们与别人一样,生来都是可怒的儿女。
3Na hata sisi sote tulikuwa kama wao; tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya tu mambo yale yaliyoipendeza miili na akili zetu. Kidunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu.
4然而 神满有怜悯,因着他爱我们的大爱,
4Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa mapendo yasiyopimika,
5就在我们因过犯死了的时候,使我们与基督一同活过来,(你们得救是靠着恩典,)
5hata, ingawa tulikuwa tumekufa kwa sababu ya dhambi, alitufanya hai pamoja na Kristo. Kwa neema ya Mungu ninyi mmeokolewa.
6又使我们在基督耶稣里,与他一同复活,一同坐在天上,
6Kwa kuungana na Kristo Yesu, Mungu alitufufua pamoja naye, tukatawale pamoja naye mbinguni.
7为的是要在将来的世代中,显明他在基督耶稣里赐给我们的恩典,是多么的丰盛。
7Ndivyo alivyopenda kuonyesha kwa watu wa nyakati za baadaye, ukuu wa neema yake aliyotujalia kwa ukarimu katika kuungana kwetu na Kristo Yesu.
8你们得救是靠着恩典,借着信心。这不是出于自己,而是 神所赐的;
8Maana, kwa neema ya Mungu mmekombolewa kwa njia ya imani. Jambo hili si matokeo ya juhudi zenu, bali ni zawadi ya Mungu.
9这也不是出于行为,免得有人自夸。
9Wala halitokani na matendo yenu wenyewe, asije mtu akajivunia kitu.
10我们原是 神所作成的,是在基督耶稣里创造的,为的是要我们行各样的善事,就是 神预先所安排的。
10Sisi ni viumbe vyake Mungu, na kwa kuungana na Kristo Yesu, alituumba kwa ajili ya kuishi maisha ya matendo mema aliyotutayarishia tuyatende.
11在基督里合而为一你们应当记得,你们从前按肉体来说是外族人;那些所谓在肉体上受过人手所行的割礼的人,称你们为未受割礼的。
11Ninyi mlio kwa asili watu wa mataifa mengine--mnaoitwa, "wasiotahiriwa" na Wayahudi ambao hujiita, "Waliotahiriwa," (kwa sababu ya kile wanachoifanyia miili yao) --kumbukeni mlivyokuwa zamani.
12那时,你们是在基督以外,与以色列国无分,在带有应许的约上是外人,在世上没有盼望,没有 神。
12Wakati ule ninyi mlikuwa bila Kristo; mlikuwa nje ya jamii ya Israeli; mlikuwa wageni na hamkuwa na sehemu yoyote katika lile agano la zile ahadi. Mlikuwa bila matumaini Mungu hapa duniani.
13你们从前远离的人,现今在基督耶稣里,靠着他的血已经可以亲近了。
13Lakini sasa, kwa kuungana na Kristo Yesu, ninyi ambao hapo awali mlikuwa mbali, mmekaribishwa kwa njia ya damu yake Kristo.
14基督就是我们的和平:他使双方合而为一,拆毁了隔在中间的墙,就是以自己的身体除掉双方的仇恨,
14Maana Kristo mwenyewe ametuletea amani kwa kuwafanya Wayahudi na watu wa mataifa mengine kuwa jamii moja. Kwa mwili wake yeye mwenyewe aliubomoa ule ukuta uliowatenganisha na kuwafanya maadui.
15并且废掉了律法的规条,使两者在他里面成为一个新人,这样就缔造了和平。
15Aliiondoa ile Sheria ya Wayahudi pamoja na amri zake na kanuni zake, ili kutokana na jamii hizo mbili aumbe jamii moja mpya katika umoja naye na hivyo kuleta amani.
16基督既然借着十字架消灭了仇恨,就借着十字架使双方与 神和好,成为一体,
16Kwa mwili wake, Kristo aliuangamiza uadui wao; kwa msalaba wake aliziunganisha jamii hizo kuwa moja na kuzipatanisha na Mungu.
17并且他来把和平的福音传给你们在远处的人,也给在近处的人。
17Basi, Kristo alikuja akahubiri Habari Njema ya amani kwenu ninyi watu wa mataifa mengine mliokuwa mbali na Mungu, na pia kwa Wayahudi ambao walikuwa karibu na Mungu.
18我们双方都借着他,在同一位圣灵里,可以进到父面前。
18Hivyo, kwa njia yake, sisi sote, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, tunaweza kumwendea Baba katika Roho mmoja.
19这样看来,你们不再是外人和客旅,而是与圣徒一同作国民,是 神家里的人了,
19Basi, ninyi si wageni tena, wala si watu wa nje; ninyi ni raia pamoja na watu wa Mungu, na ni watu wa jamaa ya Mungu.
20并且建造在使徒和先知的根基上,基督耶稣自己就是奠基石,
20Mmejengwa juu ya msingi uliowekwa na mitume na manabii, naye Kristo mwenyewe ndiye jiwe kuu la msingi.
21整座建筑都靠着他连接配合,渐渐增长成为在主里面的圣所。
21Yeye ndiye mwenye kulitengeneza jengo lote na kulikuza hata liwe hekalu takatifu kwa ajili ya B wana.
22你们在他里面也一同被建造,成为 神借着圣灵居住的所在。
22Katika kuungana naye, ninyi pia mnajengwa pamoja na wote wengine, muwe makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.