1问安
1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2愿恩惠平安从我们的父 神和主耶稣基督临到你们。
2Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3在基督里属灵的福分我们主耶稣基督的父 神是应当称颂的。他在基督里,曾经把天上各种属灵的福分赐给我们:
3Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4就如创立世界以前,他在基督里拣选了我们,使我们因着爱,在他面前成为圣洁,没有瑕疵。
4Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5他又按着自己旨意所喜悦的,预定我们借着耶稣基督得儿子的名分,
5Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6好使他恩典的荣耀得着颂赞。这恩典是他在爱子里赐给我们的。
6Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7我们在他爱子里,借着他的血蒙了救赎,过犯得到赦免,都是按着他丰盛的恩典。
7Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8这恩典是他用各样的智慧和聪明,充充足足地赐给我们的;
8aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9他照着自己在基督里预先安排的美意,使我们知道他旨意的奥秘,
9Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10到了所计划的时机成熟,就使天上地上的万有,都在基督里同归于一。
10Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11那凭着自己旨意所计划而行万事的,按着他预先所安排的,预定我们在基督里得基业(“得基业”或译:“成为 神的产业”),
11Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12借着我们这在基督里首先有盼望的人,使他的荣耀得着颂赞。
12Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13你们既然听了真理的道,就是使你们得救的福音,也信了基督,就在他里面受了所应许的圣灵作为印记。
13Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14这圣灵是我们得基业的凭据,直到 神的产业得赎,使他的荣耀得着颂赞。
14Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15保罗的祈祷因此,我听到你们在主耶稣里的信心,和对众圣徒的爱心,
15Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16就不住地为你们献上感谢。我祷告的时候,常常提到你们,
16sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17求我们主耶稣基督的 神,荣耀的父,赐给你们智慧和启示的灵,使你们充分地认识他,
17ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18并且使你们心灵的眼睛明亮,可以知道他的呼召有怎样的盼望;他基业的荣耀,在圣徒中是多么的丰盛;
18Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19 神照着他强大的力量,向我们信他的人显出的能力,是何等的浩大。
19mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20这力量运行在基督身上,使他从死人中复活,并且在天上坐在自己的右边,
20aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21远超过一切执政的、掌权的、有能的、作主的,和今生来世所能举出的一切名衔。
21Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao.
22 神又使万有都归服在他的脚下,并且使他作教会至高的元首。
22Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23教会是他的身体,是那充满万有者所完全充满的。
23Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.