1信徒的责任
1Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, ninyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa.
2你们各人的重担要互相担当,这样就成全了基督的律法。
2Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.
3如果有人本来没有什么了不起,却自以为是了不起的,就是欺骗自己。
3Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe.
4各人应该省察自己所作的,这样,他引以为荣的,就只在自己而不在别人了;
4Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.
5因为各人的担子,是要自己担当的。
5Maana kila mmoja anao mzigo wake mwenyewe wa kubeba.
6在圣道上受教的,应该和施教的人分享自己的一切美物。
6Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
7不要自欺, 神是不可轻慢的。人种的是什么,收的也是什么:
7Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.
8顺着自己的肉体撒种的,必定从肉体收取败坏;顺着圣灵撒种的,必定从圣灵收取永生。
8Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele.
9我们行善,不要觉得厌烦;如果不松懈,到了适当的时候,就有收成。
9Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.
10所以,我们一有机会,就应该对众人行善,对信徒更要这样。
10Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
11劝勉和祝福请看,我亲手写给你们的字是多么的大。
11Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe.
12那些在外表上要体面的人,他们勉强你们受割礼,不过是怕为了基督的十字架受迫害。
12Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha ninyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.
13那些受割礼的人,自己也不遵守律法,反而要你们受割礼,为的是要借着你们的肉身夸口。
13Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki Sheria; huwataka ninyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu.
14至于我,我绝不以别的夸口,只夸我们主耶稣基督的十字架。借着这十字架,在我来说,世界已经钉在十字架上了;就世界来说,我也已经钉在十字架上了。
14Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.
15受割礼或不受割礼,都算不得什么,要紧的是作新造的人。
15Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.
16所有照这准则而行的人,愿平安怜悯临到他们,就是临到 神的以色列。
16Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli--Wateule wa Mungu.
17从今以后,谁也不要搅扰我,因为我身上带着耶稣的烙痕。
17Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
18弟兄们,愿我们主耶稣基督的恩惠与你们同在(“与你们同在”原文作“与你们的心灵同在”)。阿们。
18Ndugu, nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Kristo. Amina.