聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Galatians

5

1基督释放了我们,为了要使我们得自由。所以你们要站立得稳,不要再被奴役的轭控制。
1Kristo alitupa uhuru akataka tubaki huru. Basi, simameni imara wala msikubali tena kuwa chini ya nira ya utumwa.
2基督徒的自由我保罗现在告诉你们,如果你们受割礼,基督对你们就毫无益处了。
2Sikilizeni! Ni mimi Paulo ninayesema nanyi! Kama mkikubali kutahiriwa, Kristo hatawafaidia chochote.
3我再对所有受割礼的人郑重声明:他有责任遵行全部的律法。
3Nasema tena wazi: kila anayekubali kutahiriwa itambidi kuishika Sheria yote.
4你们这些靠律法称义的人,是和基督隔绝,从恩典中坠落了。
4Kama mnatazamia kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Sheria, basi, mmejitenga mbali na Kristo; mko nje ya neema ya Mungu.
5我们靠着圣灵,凭着信,热切等候所盼望的义。
5Kwa upande wetu, lakini, sisi tunatumaini kwamba kwa nguvu ya Roho tunakubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani.
6因为在基督耶稣里,受割礼或不受割礼,都没有用处,唯有那借着爱表达出来的信,才有用处。
6Maana ikiwa tumeungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutotahiriwa hakuna maana; cha maana ni imani ifanyayo kazi kwa mapendo.
7你们向来跑得好,谁拦阻了你们,使你们不顺从真理呢?
7Mwenendo wenu ulikuwa mzuri! Nani, basi aliyewazuia kuuzingatia ukweli?
8这种劝诱不是出于那召你们的。
8Aliyesababisha hali hiyo si Mungu ambaye amewaiteni.
9一点面酵能使全团面发起来。
9"chachu kidogo tu huchachusha donge lote la unga!"
10我在主里深信你们不会存别的意念;但那搅扰你们的,无论是谁,必定要受刑罚。
10Kutokana na kuungana kwetu na Bwana, nina tumaini kubwa kwamba ninyi hamtakuwa na msimamo tofauti nami. Tena yeyote huyo anayewavurugeni--awe nani au nani--hakika ataadhibiwa.
11弟兄们,如果我仍旧传割礼,我为什么还受迫害呢?若是这样,十字架绊倒人的地方就没有了。
11Na kwa upande wangu, ndugu zangu, kama bado ninahubiri kwamba kutahiriwa ni lazima, kwa nini basi, bado ninadhulumiwa? Kama ingalikuwa hivyo, mahubiri yangu juu ya msalaba wa Kristo yasingalileta aibu yoyote.
12我恨不得那些扰乱你们的人把自己阉割了!
12Laiti hao wanaowavurugeni wangejikatakata wenyewe!
13弟兄们,你们蒙召得了自由;只是不可把这自由当作放纵情欲的机会,总要凭着爱心互相服事。
13Ninyi, ndugu, mliitwa muwe watu huru. Lakini uhuru huo usiwe kisingizio cha kutawaliwa na tamaa za kidunia; ila mnapaswa kutumikiana kwa upendo.
14因为全部的律法,都在“爱人如己”这一句话里面成全了。
14Maana Sheria yote hutimizwa katika kushika amri hii moja: "Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
15你们要谨慎,如果相咬相吞,恐怕彼此都要毁灭了。
15Lakini ikiwa mtaumana na kutafunana kama wanyama, jihadharini msije mkaangamizana wenyewe kwa wenyewe!
16肉体与圣灵为敌我是说,你们应当顺着圣灵行事,这样就一定不会去满足肉体的私欲了。
16Basi, nasema hivi: mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia.
17因为肉体的私欲和圣灵敌对,圣灵也和肉体敌对;这两样互相敌对,使你们不能作自己愿意作的。
17Maana, tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamwezi kufanya yale mnayotaka ninyi wenyewe.
18但你们若被圣灵引导,就不在律法以下了。
18Kama mkiongozwa na Roho, basi, hamko tena chini ya Sheria.
19肉体所行的都是显而易见的,就如淫乱、污秽、邪荡、
19Basi, matendo ya kidunia yanajulikana: uzinzi, uasherati, ufisadi;
20拜偶像、行邪术、仇恨、争竞、忌恨、忿怒、自私、分党、结派、
20kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, choyo, mabishano, mafarakano;
21嫉妒、醉酒、荒宴,和类似的事。我从前早就告诉过你们,现在又事先告诉你们:行这些事的人,必定不能承受 神的国。
21husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine kama hayo. Nawaambieni tena kama nilivyokwisha sema: watu wanaotenda mambo hayo hawatakuwa na nafasi yao katika ufalme wa Mungu.
22圣灵的果子但圣灵的果子是仁爱、喜乐、平安、忍耐、恩慈、良善、信实、
22Lakini matokeo ya kuongozwa na Roho ni mapendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu,
23温柔、节制;这样的事,是没有律法禁止的。
23upole na kuwa na kiasi. Hakuna Sheria inayoweza kupinga mambo hayo.
24属基督耶稣的人,是已经把肉体和邪情私欲都钉在十字架上了。
24Wale walio wa Kristo wameisulubisha hali yao ya kidunia pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
25如果我们靠圣灵活着,就应该顺着圣灵行事。
25Tukiishi kwa msaada wa Roho, na tuufuate mwongozo wake.
26我们不可贪图虚荣,彼此触怒,互相嫉妒。
26Basi, tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.