聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Galatians

4

1我说,那承受产业的,虽然是全部产业的主人,但在孩童的时期,却和奴仆没有分别。
1Basi, nasema hivi: mrithi, akiwa bado mtoto, hawi tofauti na mtumwa ingawaje mali yote ni yake.
2他是在监护人和管家之下,直到父亲预先指定的时候。
2Wakati huo wote yuko chini ya walezi na wadhamini mpaka wakati ule uliowekwa na baba yake.
3我们也是这样,作孩童的时候,被世俗的言论所奴役;
3Hali kadhalika na sisi tulipokuwa bado watoto, tulikuwa watumwa wa pepo watawala wa ulimwengu.
4但到了时机成熟, 神就差遣他的儿子,由女人所生,而且生在律法之下,
4Lakini wakati ule maalumu ulipotimia, Mungu alimtuma Mwanawe aliyezaliwa na mwanamke, akaishi chini ya Sheria
5要把律法之下的人救赎出来,好让我们得着嗣子的名分。
5apate kuwakomboa wale waliokuwa chini ya Sheria ili sisi tufanywe wana wa Mungu.
6你们既然是儿子, 神就差遣他儿子的灵进入我们心里,呼叫“阿爸、父!”
6Kwa vile sasa ninyi ni wana, Mungu amemtuma Roho wa Mwanae mioyoni mwenu, Roho ambaye hulia "Aba," yaani "Baba."
7这样,你不再是奴仆,而是儿子;既然是儿子,就靠着 神承受产业了。
7Basi, wewe si mtumwa tena, bali mwana. Na ikiwa ni mwana, basi, wewe utapokea yote Mungu aliyowawekea watoto wake.
8保罗为加拉太信徒担忧从前你们不认识 神的时候,是给那些本来不是 神的作奴仆;
8Zamani hamkumjua Mungu na hivyo mkatumikia miungu isiyo miungu kweli.
9现在你们既然认识 神,更可以说是 神所认识的,怎么还回到那些软弱贫乏的言论,情愿再作它们的奴仆呢?
9Lakini sasa, kwa vile mnamjua Mungu, au tuseme mnajulikana na Mungu, mnawezaje tena kurudi kwa wale pepo maskini na dhaifu hata kutaka kuwatumikia tena?
10你们严守日子、月份、节期、年份;
10Bado mnaadhimisha siku, miezi na miaka!
11我为你们担心,恐怕我在你们身上的劳苦是白费了。
11Nahofu kwamba labda kazi niliyoifanya kwa ajili yenu imepotea bure!
12弟兄们,我请求你们要像我一样,因为我也像你们一样。你们并没有亏负过我。
12Ndugu, nawasihi muwe kama mimi, kwa vile hata mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea ubaya wowote.
13你们知道,我第一次传福音给你们,是因为身体有病。
13Mnajua kwamba ugonjwa wangu ndio ulionipatia fursa ya kuwahubirieni Habari Njema kwa mara ya kwanza.
14虽然我的身体对你们是个试炼,你们却没有轻看,也没有厌弃,反而接纳我,好像 神的天使,也好像基督耶稣。
14Hata hivyo, wakati ule hamkunidharau wala kunikataa kwa sababu ya udhaifu wangu ingawa mlishawishiwa kufanya hivyo; lakini mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama vile ningekuwa Kristo Yesu mwenyewe.
15现在,你们的欢乐在哪里呢?我可以为你们作证,那时如果可能,你们甚至愿意把你们的眼睛剜出来给我哩!
15Mlikuwa wenye furaha; sasa kumetokea nini? Naapa kwamba wakati ule mngaliweza hata kuyang'oa macho yenu na kunipa mimi.
16现在我把真理告诉你们,反而成了你们的仇敌吗?
16Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa sababu ya kuwaambieni ukweli?
17那些人热心待你们,并不是出于好意,而是想你们和我疏远,好使你们热心待他们。
17Hao watu wengine wanawahangaikia ninyi, lakini nia zao si njema. Wanataka kuwatenganisha nami ili ninyi muwahangaikie wao.
18常常在善事上热心,总是好的;只是不要我在你们那里的时候才是这样。
18Kwa kweli ni jambo jema daima kuwahangaikia wengine katika mambo mema, na si tu wakati mimi nipo pamoja nanyi.
19我的孩子们,为了你们我再受生产的痛苦,直到基督在你们里面成形。
19Watoto wangu, kama vile mama mja mzito anavyotaabika wakati wa kujifungua, mimi nataabika tena kwa ajili yenu mpaka hapo hali yake Kristo itakapoundwa ndani yenu.
20我恨不得现今就在你们那里,改变我的语气,因为我为你们十分困扰。
20Laiti ningekuwa pamoja nanyi sasa, maana ningalipata msimamo ufaao juu yenu! Nina wasiwasi sana nanyi!
21两个妇人的寓意你们这愿意在律法之下的人哪!请告诉我,你们没有听过律法吗?
21Niambieni, enyi mnaopenda kutawaliwa na sheria: Je, mnasikia isemavyo Sheria?
22经上记着说,亚伯拉罕有两个儿子,一个出于婢女,一个出于自由的妇人。
22Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Abrahamu alikuwa na watoto wawili: mmoja kwa mwanamke mtumwa, na wa pili kwa mwanamke huru.
23但那出于婢女的,是按着肉体生的;那出于自由的妇人的,是凭着应许生的。
23Yule wa mwanamke mtumwa alizaliwa kama kawaida, lakini yule wa mwanamke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.
24这都是寓意的说法:那两个妇人就是两个约,一个是出于西奈山,生子作奴仆,这是夏甲。
24Mambo hayo yamekuwa mfano; mama hao wawili ni mfano wa maagano mawili; la kwanza ni lile lililofanyika mlimani Sinai, mwakilishi wake ni Hagari, na watoto wake wanazaliwa utumwani.
25这夏甲是指着阿拉伯的西奈山,相当于现在的耶路撒冷,她和她的儿女都是作奴仆的。
25Hagari anawakilisha mlima Sinai ulioko Arabia, na ni mfano wa Yerusalemu ya sasa, ulio mtumwa pamoja na watoto wake.
26那在上面的耶路撒冷是自由的,她是我们的母亲,
26Lakini Yerusalemu ya juu mbinguni ni mji ulio huru, nao ni mama yetu.
27因为经上记着说:“不能生育、没有生养的啊,你要欢欣!没有受过生产痛苦的啊,你要呼喊,大声呼叫!因为弃妇比有夫之妇有更多儿子。”
27Maana imeandikwa: "Furahi, ewe uliye tasa usiyezaa; paaza sauti wewe usiyepata kujifungua mtoto; maana watoto wa yule aliyeachwa ni wengi zaidi kuliko wa yule aliye na mume."
28可是,弟兄们,你们是按着应许作儿女的,好像以撒一样。
28Sasa, basi, ndugu zangu, ninyi ni watoto wa Mungu kutokana na ahadi yake kama alivyokuwa Isaka.
29不过,当时那按着肉体生的,迫害那按着圣灵生的,现在也是这样。
29Lakini kama vile siku zile yule mtoto aliyezaliwa kwa njia ya kawaida alimdhulumu yule aliyezaliwa kwa uwezo wa Roho wa Mungu, vivyo hivyo na siku hizi.
30然而经上怎样说呢?”把婢女和她的儿子赶出去,因为婢女的儿子,绝对不可以和自由的妇人的儿子一同承受产业。”
30Lakini Maandiko Matakatifu yasemaje? Yasema: "Mfukuze mama mtumwa pamoja na mwanawe; maana mtoto wa mtumwa hatarithi pamoja na mtoto wa mama huru."
31所以,弟兄们,我们不是婢女的儿女,而是自由的妇人的儿女了。
31Kwa hiyo, basi, ndugu, sisi si watoto wa mtumwa bali wa mama huru.