1肢体的联系
1Basi, mimi niliye mfungwa kwa kuwa namtumikia Bwana, nawasihi muishi maisha yanayostahili wito mlioitiwa.
2凡事谦虚、温柔、忍耐,用爱心彼此宽容;
2Muwe daima wanyenyekevu, wapole na wenye saburi; vumilianeni ninyi kwa ninyi kwa mapendo.
3以和睦联系,竭力持守圣灵所赐的合一。
3Fanyeni bidii ya kuhifadhi umoja uletwao na Roho kwa kuzingatia amani iliyo kati yenu.
4身体只有一个,圣灵只有一位,就像你们蒙召只是借着一个盼望。
4Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile tumaini mliloitiwa na Mungu ni moja.
5主只有一位,信仰只有一个,洗礼只有一种;
5Kuna Bwana mmoja, imani moja na ubatizo mmoja;
6 神只有一位,就是万有的父。他超越万有,贯彻万有,并且在万有之中。
6kuna Mungu mmoja na Baba wa wote, ambaye yuko juu ya wote, afanya kazi katika yote na yuko katika yote.
7我们各人蒙恩,是照着基督量给我们的恩赐。
7Kila mmoja wetu amepewa neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.
8所以他说:“他升上高天的时候,掳了许多俘虏,把赏赐给了人。”
8Kama yasemavyo Maandiko: "Alipopaa mbinguni juu kabisa, alichukua mateka; aliwapa watu zawadi."
9(“他升上”这句话是什么意思呢?他不是也曾降到地上吗?
9Basi, inaposemwa: "alipaa juu," ina maana gani? Maana yake ni kwamba, kwanza alishuka mpaka chini kabisa duniani.
10那降下的,就是那升到诸天之上的,为了要使他充满万有。)
10Basi, huyo aliyeshuka hapa duniani, ndiye aliyepaa juu ya mbingu zote apate kuujaza ulimwengu.
11他所赐的,有作使徒的,有作先知的,有作传福音的,也有作牧养和教导的,
11Ndiye aliyewapa watu zawadi: wengine aliwajalia wawe mitume, wengine manabii, wengine wawe waeneza Habari Njema, wengine wachungaji na walimu.
12为的是要装备圣徒,去承担圣工,建立基督的身体;
12Alifanya hivyo apate kuwatayarisha watu wote wa Mungu kwa ajili ya kazi ya huduma ya Kikristo ili kuujenga mwili wa Kristo,
13直到我们众人对 神的儿子都有一致的信仰和认识,可以长大成人,达到基督丰盛长成的身量;
13na hivyo sote tuufikie umoja wa imani na kumjua Mwana wa Mungu; tuwe watu waliokomaa na kuufikia utimilifu wake Kristo mwenyewe.
14使我们不再作小孩子,中了人的诡计和骗人的手段,给异教之风摇撼,飘来飘去,
14Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukitupwa na kupeperushwa huko na huko kwa kila upepo wa mafundisho wanayozua watu wadanganyifu, ili wawapotoshe wengine kwa hila.
15却要在爱中过诚实的生活,在各方面长进,达到基督的身量。他是教会的头,
15Ila, sisi tukisema ukweli kwa moyo wa mapendo tutakua zidi katika kila jambo kulingana na Kristo ambaye ndiye kichwa;
16全身靠着他,借着每一个关节的支持,照着每部分的功用,配合联系起来,使身体渐渐长大,在爱中建立自己。
16chini ya uongozi wake, viungo vyote vya mwili hushikamana pamoja, na mwili wote hutegemezwa kwa msaada wa viungo vyake. Basi, kila kiungo kikitekeleza kazi yake ipasavyo, mwili wote hukua na kujijenga katika upendo.
17要穿上新人所以,我要这样说,并且要在主里肯定地说:你们行事为人不要再像教外人,存着虚妄的意念。
17Basi, kwa jina la Bwana, nawaonyeni: msiishi tena kama watu wasiomjua Mungu, ambao fikira zao zimekuwa upuuzi mtupu,
18他们的心思昏昧,因为自己无知,心里刚硬,就与 神所赐的生命隔绝了。
18na akili zao zimo gizani. Wako mbali na uzima wa Mungu, kwa sababu ya upumbavu ulio ndani yao na ukaidi wao.
19他们既然麻木不仁,就任凭自己放纵情欲,贪行各样污秽的事。
19Wamepotoka na hawana aibu, wamejitosa katika ufisadi; hufanya kwa pupa kila aina ya mambo ya aibu.
20但是你们从基督所学的,却不是这样。
20Lakini ninyi hamkujifunza hivyo juu ya Kristo.
21如果你们听了他,在他里面受过教导,(因为真理是在耶稣里的,)
21Ni dhahiri kwamba mlisikia barabara habari zake, na mkiwa wafuasi wake mkafundishwa ukweli ulivyo katika Yesu.
22就要除去你们那照着从前生活方式而活的旧人。这旧人是随着迷惑人的私欲渐渐败坏的。
22Basi, acheni mwenendo wenu wa awali, yaani ule utu wenu wa kale uliokuwa unaangamizwa kwa tamaa zake danganyifu.
23你们要把心灵更换一新,
23Jirekebisheni upya rohoni na katika fikira zenu.
24并且穿上新人。这新人是照着 神的形象,在公义和真实的圣洁里创造的。
24Vaeni hali mpya ya utu ambayo imeumbwa kwa mfano wa Mungu na ambayo hujionyesha katika maisha ya kweli ya uadilifu na utakatifu.
25新人的表现所以,你们要除掉谎言,各人要与邻舍说真话,因为我们彼此是肢体。
25Kwa hiyo, acheni uongo. Kila mmoja anapaswa kumwambia mwenzake ukweli, maana kila mmoja wetu ni kiungo cha mwili wa Kristo.
26生气却不要犯罪;含怒不可到日落。
26Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima.
27不可给魔鬼留地步。
27Msimpe Ibilisi nafasi.
28偷窃的,不要再偷,却要作工,亲手作正当的事,使自己可以把所得到的,分给缺乏的人。
28Aliyekuwa akiiba, asiibe tena, bali na aanze kufanya kazi njema kwa mikono yake, apate kuwa na kitu cha kumsaidia mtu aliye maskini.
29一句坏话也不可出口,却要适当地说造就人的好话,使听见的人得益处。
29Maneno mabaya hata yasisikike kamwe miongoni mwenu; kila mara maneno yenu yawe ya kufaa na ambayo hujenga na kuwasaidia wengine, ili yawaneemeshe wasikilizaji wenu.
30不可让 神的圣灵忧伤,因为你们受了他的印记,等候得赎的日子。
30Msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu maana Roho huyo ni alama ya Mungu kwenu kwamba ninyi ni watu wake, na thibitisho kwamba siku itakuja ambapo Mungu atawakomboeni.
31一切苛刻、恼怒、暴戾、嚷闹、毁谤,连同一切恶毒,都应当从你们中间除掉。
31Basi, achaneni na uhasama, chuki, hasira, kelele, matusi! Achaneni na kila uovu!
32要互相友爱,存温柔的心,彼此饶恕,就像 神在基督里饶恕了你们一样。
32Muwe na moyo mwema na wenye kuhurumiana; kila mmoja na amsamehe mwenzake kama naye Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.