1因此,你们既然是蒙爱的儿女,就应当效法 神。
1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
2要凭着爱心行事,好像基督爱我们,为我们舍己,当作馨香的供品和祭物献给 神。
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
3至于淫乱和任何污秽或贪心的事,在你们中间连提都不可提,才合圣徒的体统。
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
4更不要讲淫秽和愚妄的话,或下流的笑话,这些都与你们不相称;却要说感谢的话。
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
5因为你们确实知道,无论是淫乱的、污秽的或贪心的(贪心就是拜偶像),都得不到在基督和 神的国里的基业。
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
6要作光明的儿女不要给别人用空言欺骗了你们,正因为这些事, 神的震怒必定临到那些悖逆的人。
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
7所以,不要与他们同流合污。
7Basi, msishirikiane nao.
8你们从前是黑暗的,现今在主里却是光明的,行事为人就应当像光明的儿女。
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
9光明所结的果子,就是一切良善、公义、诚实。
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
10你们要察验什么是主所喜悦的。
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
11不要参与暗昧无益的事,倒要把它揭露出来,
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
12因为他们暗中所作的事,连提起来也是羞耻的。
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
13凡被光揭露的,都是显而易见的。
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
14因为一切显露出来的就是光,所以有话说:“睡了的人哪,醒过来,从死人中起来吧!基督必要照亮你。”
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
15所以,你们行事为人要谨慎,不要像愚昧人,却要像聪明人。
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
16要把握时机,因为这时代邪恶。
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
17因此,不要作糊涂人,要明白什么是主的旨意。
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
18不要醉酒,醉酒能使人放荡乱性,却要让圣灵充满。
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
19应当用诗章、圣诗、灵歌,彼此呼应,口唱心和地赞美主。
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
20凡事要奉我们主耶稣基督的名,常常感谢父 神,
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21还要存敬畏基督的心,彼此顺服。
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
22丈夫与妻子你们作妻子的,要顺服自己的丈夫,好像顺服主一样,
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
23因为丈夫是妻子的头,好像基督是教会的头;基督又是教会全体的救主。
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
24教会怎样顺服基督,妻子也要照样凡事顺服丈夫。
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
25你们作丈夫的,要爱妻子,好像基督爱教会,为教会舍己,
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
26为的是要用水借着道把教会洗净,成为圣洁,
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
27可以作荣耀的教会归给自己,什么污点皱纹等也没有,而是圣洁没有瑕疵的。
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
28丈夫也应当这样爱妻子,好像爱自己的身体一样。爱妻子的,就是爱自己了。
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
29从来没有人恨恶自己的身体,总是保养顾惜,好像基督对教会一样,
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
30因为我们是他身上的肢体。
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
31为了这缘故,人要离开父母,与妻子结合,二人成为一体。
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
32这是极大的奥秘,但我是指着基督和教会说的。
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
33无论怎样,你们各人都要爱自己的妻子,好像爱自己一样。妻子也应当敬重丈夫。
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.