1问安作使徒的保罗(不是由于人,也不是借着人,而是借着耶稣基督和那使他从死人中复活的父 神),
1Mimi Paulo mtume,
2和所有与我在一起的弟兄,写信给加拉太的众教会。
2na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
3愿恩惠平安从我们的父 神和主耶稣基督临到你们。
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
4基督照着我们父 神的旨意,曾经为我们的罪舍己,为的是要救我们脱离现在这邪恶的世代。
4Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa.
5愿荣耀归给他,直到永永远远。阿们。
5Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina.
6福音只有一个我很惊奇,你们这么快就离开了借着基督的恩呼召你们的那一位,去归向别的福音。
6Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
7其实那并不是另一个福音,只是有些搅扰你们的人,想把基督的福音改变了。
7Lakini hakuna "Habari Njema" nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
8但无论是我们,或是从天上来的使者,如果传给你们的和我们以前传给你们的福音不同,他就该受咒诅。
8Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
9我们已经说过,现在我要再说,如果有人传给你们的和你们以前所领受的福音不同,他就该受咒诅。
9Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
10我现在是要得人的欢心,还是要得 神的欢心呢?难道我想讨人欢喜吗?如果我仍然要讨人欢喜,就不是基督的仆人了。
10Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
11保罗得启示作使徒弟兄们,我要你们知道,我所传的福音,并不是照着人的意思,
11Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
12因为这福音我不是从人领受的,也不是人教导我的,而是借着耶稣基督的启示来的。
12Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
13你们听过我从前在犹太教中所行的:怎样极力逼迫残害 神的教会,
13Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
14怎样在犹太教中比许多本族同辈的人更激进,为我祖先的传统分外热心。
14Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
15然而,当我在母腹里就把我分别出来,又用他的恩呼召我的那一位,
15Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
16既然乐意把自己的儿子启示给我,使我可以在外族人中传扬他,我就没有和任何人(“人”直译“肉和血”)商量,
16Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
17也没有上耶路撒冷见那些比我先作使徒的,却去了阿拉伯,然后再回到大马士革。
17na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
18过了三年,我才上耶路撒冷去见矶法,和他住了十五天。
18Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
19至于其余的使徒,除了主的弟弟雅各以外,我都没有见过。
19Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20在 神面前我敢说,我写给你们的都不是谎话。
20Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
21后来,我到了叙利亚和基利家一带的地方。
21Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
22那时,在基督里的犹太众教会还没有见过我的面,
22Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
23不过听说“那个从前迫害我们的,现在竟然传扬他以前所残害的信仰”,
23Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: "Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza."
24他们就因着我的缘故颂赞 神。
24Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.