聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Hebrews

13

1教导信徒该作的事
1Endeleeni kupendana kidugu.
2不要忘了用爱心接待人,有人就是这样作,在无意中就款待了天使。
2Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
3你们要记念那些被囚禁的人,好像跟他们一起被囚禁;也要记念那些受虐待的人,好像你们也亲自受过。
3Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
4人人都应该尊重婚姻,婚床也不要玷污,因为 神一定审判淫乱的和奸淫的人。
4Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
5你们为人不要贪爱钱财,要以现在所有的为满足;因为 神亲自说过:“我决不撇下你,也不离弃你。”
5Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: "Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa."
6所以我们可以放胆说:“主是我的帮助,我决不害怕,人能把我怎么样呢?”
6Ndiyo maana tunathubutu kusema: "Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?"
7你们要记念那些领导过你们,把 神的道传给你们的人;你们要观察他们一生的成果,要效法他们的信心。
7wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
8耶稣基督昨天、今天、一直到永远都是一样的。
8Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele.
9你们不要被各样怪异的教训勾引去了。人心靠着恩典,而不是靠着食物得到坚定,才是好的;因为那些拘守食物的人,从来没有得过益处。
9Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
10我们有一座祭坛,坛上的祭物,是那些在会幕中供职的人没有权利吃的。
10Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
11那些祭牲的血,由大祭司带进圣所作赎罪祭,祭牲的身体却要在营外焚烧。
11Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12所以耶稣也是这样在城门外受苦,为的是要借着自己的血使人民成圣。
12Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
13那么,让我们也出到营外到他那里去,担当他的凌辱。
13Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
14因为在这里我们没有长存的城,我们却是寻求那将要来的城。
14Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
15所以,我们要借着耶稣,常常把颂赞的祭品献给 神,这就是承认他的名的人嘴唇的果子。
15Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
16你们也不要忘记行善和捐输,这样的祭是 神所喜悦的。
16Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
17你们要听从那些领导你们的人,也要顺服他们;因为他们为你们的灵魂警醒,好像要交帐的人一样。你们要使他们交帐的时候快快乐乐,不至于叹息;如果他们叹息,对你们就没有好处了。
17Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18请为我们祷告,因为我们深信自己良心无亏,愿意凡事遵行正道。
18Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
19我更加要求你们为我们祷告,好使我们能够快点回到你们那里去。
19Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
20祝福和问安愿赐平安的 神,就是那凭着永约的血,把群羊的大牧人我们的主耶稣,从死人中领出来的那一位,
20Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele.
21在一切善事上成全你们,好使你们遵行他的旨意;又借着耶稣基督在我们里面,行他所喜悦的事。愿荣耀归给他,直到永永远远。阿们。
21Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina.
22弟兄们,我劝你们耐心接受我这劝勉的话,因为我只是简略地写给你们。
22Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
23你们要知道,我们的弟兄提摩太已经释放了;如果他来得早,我就跟他一起去看你们。
23Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
24请问候所有领导你们的人和所有圣徒。从意大利来的人也问候你们。
24Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
25愿恩惠与你们众人同在。
25Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.