1以试炼为喜乐
1Mimi Yakobo, mtumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, nawaandikia ninyi, makabila kumi na mawili, yaliyotawanyika ulimwenguni! Salaam!
2我的弟兄们,你们遭遇各种试炼的时候,都要看为喜乐;
2Ndugu zangu, muwe na furaha mnapopatwa na majaribu mbalimbali,
3因为知道你们的信心经过考验,就产生忍耐。
3kwani mwajua kwamba imani yenu ikisha stahimili, itawapatieni uvumilivu.
4但忍耐要坚持到底(“坚持到底”原文作“有完全的功效”),使你们可以完全,毫无缺乏。
4Muwe na hakika kwamba uvumilivu wenu utawategemeza mpaka mwisho, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa chochote.
5你们中间若有人缺少智慧,就当向那厚赐众人,而且不斥责人的 神祈求,他就必得着。
5Lakini kama mmoja wenu ametindikiwa hekima, basi, anapaswa kumwomba Mungu ambaye atampatia; kwani Mungu huwapa wote kwa wingi na kwa ukarimu.
6可是,他应该凭着信心祈求,不要有疑惑;因为疑惑的人,就像被风吹荡翻腾的海浪。
6Lakini anapaswa kuomba kwa imani bila mashaka yoyote. Mtu aliye na mashaka ni kama mawimbi ya bahari ambayo husukumwa na kutupwatupwa na upepo.
7那样的人,不要想从主得到什么;
7Mtu wa namna hiyo, mwenye nia mbili na asiye na msimamo katika mwenendo wake wote,
8因为三心两意的人,在他的一切道路上,都摇摆不定。
8asidhani ya kwamba atapata chochote kile kutoka kwa Bwana.
9富贵荣华转眼消逝卑微的弟兄应当以高升为荣;
9Ndugu aliye maskini anapaswa kufurahi wakati Mungu anapomkweza,
10富足的也不应该以降卑为辱;因为他如同草上的花,必要过去。
10naye tajiri anapaswa kufurahi anaposhushwa na Mungu. Maana tajiri atatoweka kama ua la porini.
11太阳一出,热风一吹,草必枯干,花必凋谢,它的美容就消失了;富足的人也必在他的奔波经营中这样衰落。
11Jua huchomoza na kwa joto lake kali hukausha mimea, nayo maua yake huanguka, na uzuri wake wote huharibika. Vivyo hivyo, tajiri ataangamizwa katika shughuli zake.
12忍受试炼的人有福了能忍受试炼的人,是有福的;因为他经过考验之后,必得着生命的冠冕,这冠冕是主应许给爱他的人的。
12Heri mtu anayebaki mwaminifu katika majaribu, kwani akisha stahimili atapewa tuzo la uzima ambalo Mungu aliwaahidia wale wanaompenda.
13人被试探,不可说“我被 神试探”;因为 神不能被恶试探,他也不试探任何人。
13Kama mtu akijaribiwa, asiseme: "Ninajaribiwa na Mungu." Maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, wala yeye hamjaribu mtu yeyote.
14每一个人受试探,都是被自己的私欲所勾引诱惑的。
14Lakini mtu hujaribiwa anapovutwa na kunaswa na tamaa zake mbaya.
15私欲怀了胎,就生出罪;罪长成了,就产生死亡。
15Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo.
16我亲爱的弟兄们,不要看错了。
16Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike!
17各样美好的赏赐,各样完备的恩赐,都是从上面、从众光之父降下来的,他本身并没有改变,也没有转动的影子。
17Kila kipaji chema na kila zawadi kamilifu hutoka mbinguni; hutoka kwa Baba, Muumba wa mianga, ambaye habadiliki wala hana alama yoyote ya ugeugeu.
18他凭着自己的旨意,借着真理的道生了我们,使我们作他所造的万物中初熟的果子。
18Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa kwa neno lake la ukweli, ili tuwe namna ya matunda ya kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
19要作行道的人我亲爱的弟兄们,你们要知道,人人都应该快快地听,慢慢地说,慢一点动怒;
19Ndugu zangu wapenzi, kumbukeni jambo hili! Kila mtu na awe mwepesi wa kusikia lakini asiwe mwepesi wa kusema wala mwepesi wa kukasirika.
20因为人的忿怒并不能成全 神的义。
20Mwenye hasira hawezi kutimiza matakwa ya Mungu yaliyo ya haki.
21所以你们应当摆脱一切污秽和所有的邪恶,以温柔的心领受 神栽种的道;这道能救你们的灵魂。
21Kwa hiyo, tupilieni mbali mwenendo mchafu na tabia zote mbovu; jiwekeni chini ya Mungu na kupokea ule ujumbe uliopandwa mioyoni mwenu, ambao waweza kuziokoa nafsi zenu.
22你们应该作行道的人,不要单作听道的人,自己欺骗自己;
22Msijidanganye wenyewe kwa kusikiliza tu neno lake, bali litekelezeni kwa vitendo.
23因为人若只作听道的人,不作行道的人,他就像一个人对着镜子看自己本来的面貌,
23Yeyote anayesikiliza hilo neno lakini halitekelezi, huyo ni kama mtu anayejiangalia sura yake mwenyewe katika kioo.
24看过走开以后,马上就忘记自己的样子。
24Hujiangalia mwenyewe, kisha huenda zake, na mara husahau jinsi alivyo.
25唯有详细察看那使人自由的全备的律法,并且时常遵守的人,他不是听了就忘记,而是实行出来,就必因自己所作的蒙福。
25Lakini mtu anayeangalia kwa makini sheria kamilifu ambayo huwapa watu uhuru, mtu anayeendelea kuizingatia, na si kuisikia tu na kuisahau baadaye, bali anaitekeleza, mtu huyo atabarikiwa katika kila kitu anachofanya.
26如果有人自以为虔诚,却不约束他的舌头,反而自己欺骗自己,这人的虔诚是没有用的。
26Kama mtu akijiona kuwa ni mtu mwenye dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, dini yake haifai kitu, na anajidanganya mwenyewe.
27在父 神看来,纯洁无玷污的虔诚,就是照顾患难中的孤儿寡妇,并且保守自己不被世俗所污染。
27Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.