1不可重富轻贫
1Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.
2如果有一个手戴金戒指、身穿华丽衣服的人,进入你们的会堂;又有一个衣衫褴褛的穷人,也进去了。
2Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.
3你们就看重那穿华丽衣服的人,说:“请坐在这好位上。”又对那个穷人说:“你站在那里。”或说:“坐在我的脚凳下边。”
3Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: "Keti hapa mahali pazuri," na kumwambia yule maskini: "Wewe, simama huko," au "Keti hapa sakafuni miguuni pangu,"
4这不是你们对人有歧视,成了心怀恶意的审判官吗?
4je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?
5我亲爱的弟兄们,请听: 神不是拣选了在世上被认为贫穷的人吗?这些人却在信心上富足,而且是承受 神的国的人。这国是 神应许赐给爱他的人的。
5Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.
6然而你们却侮辱穷人。其实,那些欺压你们,拉你们上法庭的,不就是富足的人吗?
6Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?
7难道不是他们亵渎那召你们的尊名吗?(或译:“难道不是他们毁谤你们蒙召的美名吗?”)
7Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?
8你们若照着圣经所说“要爱人如己”这话,去完成这至尊的律法,你们就作对了。
8Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: "Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe", mtakuwa mnafanya vema kabisa.
9如果你们凭外貌待人,就是犯罪,律法就要裁定你们是犯法的。
9Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.
10因为凡是遵守全部律法的,只要在一条上失足,就违犯所有的了。
10Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.
11就像那说“不可奸淫”的,也说“不可杀人”;你纵然不奸淫,却杀人,还是犯法的。
11Maana yuleyule aliyesema: "Usizini," alisema pia "Usiue". Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.
12你们既然按着使人自由的律法受审判,就应照着这律法说话行事。
12Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.
13因为对不行怜悯的人,审判他们的时候就没有怜悯;怜悯胜过审判。
13Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.
14信心没有行为是死的我的弟兄们,人若说他有信心,却没有行为,有什么益处呢?这信心能救他吗?
14Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?
15如果有弟兄或姊妹缺衣少食,
15Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.
16而你们中间有人对他们说:“平平安安地去吧!愿你们穿得暖,吃得饱。”却不给他们身体所需用的,那有什么用处呢?
16Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: "Nendeni salama mkaote moto na kushiba," bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?
17照样,如果只有信心,没有行为,这信心就是死的。
17Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.
18也许有人要说,你有信心,我有行为;请把你没有行为的信心指给我看,我就借着我的行为,把我的信心指给你看。
18Lakini mtu anaweza kusema: "Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!" Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19你信 神只有一位,你信的不错;就连鬼魔也信,却是战兢。
19Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.
20愚昧的人哪,你愿意知道没有行为的信心是没有用的吗?
20Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?
21我们的祖先亚伯拉罕,把他的儿子以撒献在祭坛上,不是因行为称义吗?
21Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.
22你看,他的信心与行为是一致的,信心就因着行为得到完全了;
22Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.
23这正应验了经上所说的:“亚伯拉罕信 神,这就算为他的义。”他也被称为 神的朋友。
23Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: "Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu."
24可见人称义是因着行为,不仅是因着信心。
24Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.
25照样,妓女喇合接待了探子,又从另一条路把他们送走,不也是因行为称义吗?
25Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.
26身体没有灵魂是死的,照样,信心没有行为也是死的。
26Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.