1要制伏舌头
1Ndugu zangu, wengi wenu msiwe walimu. Kama mjuavyo, sisi walimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine.
2我们在许多的事上都有过错,假如有人在言语上没有过错,他就是完全的人,也能够控制全身。
2Lakini kama mtu hakosi katika usemi wake, basi, huyo ni mkamilifu, na anaweza kutawala nafsi yake yote.
3我们若把嚼环扣入马嘴,使它们驯服,就能驾驭它们的全身。
3Sisi huwatia farasi lijamu kinywani mwao ili watutii; na kwa njia hiyo twaweza kuwaongoza kokote tunakotaka.
4试看,船只虽然甚大,又被狂风催逼,舵手只用小小的舵,就可以随意操纵。
4Meli nazo pia, ingawa ni kubwa sana, na husukumwa na upepo mkali, huweza kugeuzwa kwa usukani mdogo sana, zikaelekea kokote nahodha anakotaka.
5照样,舌头虽然是个小肢体,却会说夸大的话。试看,星星之火,可以燎原;
5Vivyo hivyo, ulimi, ingawa ni kiungo kidogo cha mwili, hujisifia makuu sana. Moto mdogo waweza kuteketeza msitu mkubwa.
6舌头就是火,在我们百体中,是个不义的世界,能污秽全身,把整个生命在运转中焚烧起来,而且是被地狱之火点燃的。
6Hali kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote. Huteketeza maisha yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe.
7各类飞禽、走兽、昆虫、水族,都可以驯服,而且都已经被人类制伏了;
7Binadamu anaweza kuwafuga wanyama, na amefaulu kufuga viumbe vyote--wanyama wa mwituni, ndege, nyoka na viumbe vya baharini.
8可是没有人能够制伏舌头;它是喋喋不休的恶物,充满了致命的毒素。
8Lakini hakuna mtu aliyeweza kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kiovu, hakitawaliki, na kimejaa sumu inayoua.
9我们用它来称颂我们的主和天父,又用它来咒诅照 神的形象被造的人。
9Kwa ulimi sisi twamshukuru Bwana na Baba yetu. Kwa ulimi huohuo twawalaani watu, watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
10同一张嘴竟然又称颂主,又咒诅人;我的弟兄们,这是不应该的!
10Maneno ya laana na ya kusifia hutoka katika kinywa kimoja. Ndugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa hivyo.
11同一泉眼里能够涌出甜水和苦水来吗?
11Je, chemchemi moja yaweza kutoa maji matamu na maji machungu pamoja?
12我的弟兄们,无花果树能结橄榄吗?葡萄树能长无花果吗?咸水也不能发出甜水来。
12Ndugu zangu, je, mti wa mtini waweza kuzaa zeituni? Au, mzabibu waweza kuzaa tini? Chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
13从天上来的智慧你们中间谁是有智慧、有见识的呢?他就应当有美好的生活,用明智的温柔,把自己的行为表现出来。
13Je, ni nani mwenye hekima na akili miongoni mwenu? Basi, aonyeshe jambo hilo kwa mwenendo wake mzuri na kwa matendo yake mema yanayofanyika kwa unyenyekevu na hekima.
14如果你们心中存着刻薄的嫉妒和自私,就不可夸口,也不可说谎抵挡真理。
14Lakini ikiwa mioyo yenu imejaa wivu, chuki na ubinafsi, basi, msijisifu na kusema uongo dhidi ya ukweli.
15这种智慧不是从天上来的,而是属地的、属血气的和属鬼魔的。
15Hekima ya namna hiyo haitoki juu mbinguni; hekima hiyo ni ya ulimwengu, na ya kidunia, tena ni ya kishetani.
16因为凡有嫉妒和自私的地方,就必有扰乱和各样的坏事。
16Maana popote palipo na wivu na ubinafsi hapo pana fujo na kila aina ya uovu.
17至于从天上来的智慧,首先是纯洁的,其次是和平的,温柔的,谦逊的,满有恩慈和善果,没有偏袒,没有虚伪。
17Lakini hekima itokayo juu mbinguni, kwanza ni safi; inapenda amani, upole na huwajali watu; imejaa huruma na huzaa matunda ya matendo mema; haina ubaguzi wala unafiki.
18这是缔造和平的人,用和平所培植出来的义果。
18Uadilifu ni mazao ya mbegu ambazo wapenda amani hupanda katika amani.