聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

James

4

1与世俗为友就是与 神为敌
1Mapigano na magombano yote kati yenu yanatoka wapi? Hutoka katika tamaa zenu mbaya ambazo hupigana daima ndani yenu.
2你们放纵贪欲,如果得不到,就杀人;你们嫉妒,如果一无所得,就打斗争执。你们得不到,因为你们不求;
2Mnatamani vitu na kwa vile hamvipati mko tayari kuua; mwatamani sana kupata vitu, lakini hamvipati, hivyo mnagombana na kupigana. Hampati kile mnachotaka kwa sababu hamkiombi kwa Mungu.
3你们求也得不到,因为你们的动机不良,要把所得的耗费在你们的私欲上。
3Tena, mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya; mnaomba ili mpate kutosheleza tamaa zenu.
4淫乱的人哪,你们不知道与世俗为友,就是与 神为敌吗?所以与世俗为友的,就成了 神的仇敌。
4Ninyi ni watu msio na uaminifu kama wazinzi. Je, hamjui kwamba kuwa rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu? Yeyote anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya adui wa Mungu.
5圣经说:“ 神爱他那安置在我们里面的灵,爱到嫉妒的地步”(或译:“ 神安置在我们里面的灵,爱到嫉妒的地步”),你们想这话是徒然的吗?
5Msifikiri kwamba Maandiko Matakatifu yamesema maneno ya bure, yanaposema: "Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu ana wivu mkubwa."
6但 神所赐的恩更大;所以圣经上说:“ 神抵挡骄傲的人,赐恩给谦卑的人。”
6Lakini, neema tunayopewa na Mungu ina nguvu zaidi; kama yasemavyo Maandiko: "Mungu huwapinga wenye majivuno lakini huwapa neema wanyenyekevu."
7你们应当顺服 神,抵挡魔鬼,魔鬼就逃避你们。
7Basi, jiwekeni chini ya Mungu; mpingeni Ibilisi naye atawakimbieni.
8你们应当亲近 神, 神就亲近你们。罪人啊,要洁净你们的手;三心两意的人哪,要清洁你们的心。
8Mkaribieni Mungu, naye atakuja karibu nanyi. Osheni mikono yenu enyi wakosefu! Safisheni mioyo yenu enyi wanafiki!
9你们要愁苦、悲哀、哭泣,把欢笑变为伤痛,把快乐变为忧愁。
9Oneni huzuni, lieni na kuomboleza; kicheko chenu na kiwe kilio; na furaha yenu iwe huzuni kubwa.
10你们务要在主面前谦卑,他就使你们高升。
10Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.
11不可彼此批评弟兄们,不要互相毁谤;人若毁谤弟兄,或判断弟兄,就是毁谤律法、判断律法了。如果你判断律法,就不是实行律法的人,而是审判官了。
11Ndugu, msilaumiane ninyi kwa ninyi. Anayemlaumu ndugu yake na kumhukumu, huyo huilaumu na kuihukumu Sheria. Kama ukiihukumu Sheria, basi, wewe huitii Sheria, bali waihukumu.
12立法的,审判的,只有一位,就是那能拯救人,也能毁灭人的 神;你这判断邻舍的,你是谁呢?
12Mungu peke yake ndiye mwenye kuweka Sheria na kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi, wewe ni nani hata umhukumu binadamu mwenzako?
13不可自夸自恃你们说:“今天或明天,我们要到某城去,在那里住一年,作生意赚钱。”
13Basi, sasa sikilizeni ninyi mnaosema: "Leo au kesho tutakwenda katika mji fulani na kukaa huko mwaka mzima tukifanya biashara na kupata faida."
14其实明天怎样,你们并不知道。你们的生命是什么呢?你们本来是过眼云烟,转瞬之间就消逝了。
14Ninyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Ninyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena.
15你们倒不如说:“主若愿意,我们就可以活着,作这事或作那事。”
15Mngalipaswa kusema: "Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile."
16但现在你们竟然张狂自夸;这一切自夸,都是邪恶的。
16Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya.
17人若知道该行善事,却不去行,这就是他的罪了。
17Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.