聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

James

5

1警告不义的有钱人
1Na sasa sikilizeni enyi matajiri! Lieni na kuomboleza kwa sababu ya taabu zitakazowajieni.
2你们的财物朽坏了,你们的衣服给蛀了,
2Mali zenu zimeoza, na nguo zenu zimeliwa na nondo.
3你们的金银生锈,这锈要成为控告你们的铁证,又要像火一样吞吃你们的肉。你们竟然在这末世积聚财宝。
3Dhahabu yenu na fedha vimeota kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu, nayo itakula miili yenu kama vile moto. Ninyi mmejilundikia mali katika siku hizi za mwisho!
4看哪,工人为你们收割庄稼,你们竟然克扣他们的工资;那工资必为他们呼冤;收割者的呼声,已经达到万军之主的耳中了。
4Hamkuwalipa mishahara watumishi waliofanya kazi katika mashamba yenu. Sikilizeni malalamiko yao! Kilio cha hao wanaovuna mashamba yenu kimefika masikioni mwa Bwana, Mwenye Nguvu.
5你们在世上穷奢极侈,养肥了自己,竟不知屠宰的日子到了。
5Mmeishi duniani maisha ya kujifurahisha na ya anasa. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa.
6你们把义人定罪杀害,但他并没有反抗。
6Mmemhukumu na kumwua mtu asiye na hatia, naye hakuwapigeni.
7忍耐的人有福了所以,弟兄们,你们应当忍耐,直到主来。看哪,农夫等待着地里宝贵的出产,为它忍耐,直到获得秋霖春雨。
7Basi, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapokuja. Tazameni mkulima anavyongoja kwa subira mimea yake itoe mavuno mazuri. Yeye hungojea kwa subira mvua za masika na za vuli.
8你们也应当忍耐,坚定自己的心;因为主再来的日子近了。
8Nanyi pia mnapaswa kuwa na subira; imarisheni mioyo yenu, maana siku ya kuja kwake Bwana inakaribia.
9弟兄们,不要彼此抱怨,免得你们受审判。看哪,审判的主已经站在门前了。
9Ndugu zangu, msinung'unikiane ninyi kwa ninyi msije mkahukumiwa na Mungu. Hakimu yu karibu, tayari kuingia.
10弟兄们,你们应当效法奉主的名说话的先知,以他们为受苦忍耐的榜样。
10Ndugu, mkitaka kuona mfano wa subira na uvumilivu katika mateso, fikirini juu ya manabii ambao walinena kwa jina la Bwana.
11看哪,那些忍耐的人,我们称他们是有福的;你们听过约伯的忍耐,也看见了主赐给他的结局,知道主是满有怜悯和仁慈的。
11Tunawaita hao wenye heri kwa sababu walivumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wa Yobu, na mnajua jinsi Bwana alivyomtendea mwishoni. Maana Bwana amejaa huruma na rehema.
12我的弟兄们,最要紧的是不可起誓:不可指着天起誓,也不可指着地起誓,任何的誓都当禁绝。你们的话,是就说是,不是就说不是;免得你们落在审判之下。
12Zaidi ya hayo yote, ndugu zangu, msiape kwa mbingu, wala kwa dunia, wala kwa kitu kingine chochote. Semeni "Ndiyo" kama maana yenu ni ndiyo, na "La" kama maana yenu ni la, na hapo hamtahukumiwa na Mungu.
13义人的祈祷大有功效你们中间有人受苦吗?他就应该祷告。有人心情愉快吗?他就应该歌颂。
13Je, pana mtu yeyote miongoni mwenu aliye na shida? Anapaswa kusali. Je, yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa.
14你们中间有人患病吗?他就应该请教会的长老来,让他们奉主的名为他抹油祈祷。
14Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
15出于信心的祈祷,可以使病人康复,主必叫他起来;他若犯了罪,也必蒙赦免。
15Wakiomba kwa imani mgonjwa ataponyeshwa; Bwana atampatia nafuu, na dhambi alizotenda zitaondolewa.
16所以你们应当彼此认罪,互相代求,这样你们就可以痊愈。义人祈祷所发出的力量,是大有功效的。
16Basi, ungamanianeni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.
17以利亚是与我们性情相同的人;他恳切祈求不要下雨,地上就三年零六个月没有雨;
17Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo mvua isinyeshe, nayo haikunyesha nchini kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita.
18他又祈祷,天就下雨,地就生出土产来。
18Kisha akaomba tena, mvua ikanyesha kutoka angani na nchi ikatoa mazao yake.
19我的弟兄们,你们中间若有人被骗离开了真道,如果有人使他回头,
19Ndugu zangu, mmoja wenu akipotoka kuhusu ukweli, na mwingine akamrudisha,
20你们应该知道,那使罪人从歧途上转回的,就会拯救他的灵魂脱离死亡,也会遮盖许多罪恶。
20fahamuni kwamba, huyo anayemrudisha mwenye dhambi kutoka njia yake ya upotovu, ataiokoa roho yake kutoka kifo, na dhambi nyingi zitaondolewa.