聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Hebrews

8

1耶稣是更美的约的中保
1Basi, jambo muhimu katika hayo tunayosema ni hili: sisi tunaye Kuhani Mkuu wa namna hiyo, ambaye anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mwenyezi Mungu mbinguni.
2在至圣所和真会幕里供职;这真会幕是主支搭的,不是人支搭的。
2Yeye hutoa huduma ya Kuhani Mkuu katika Mahali Patakatifu sana, yaani ndani ya ile hema ya kweli iliyojengwa na Bwana, siyo na binadamu.
3所有大祭司都是为了献礼物和祭品而设立的,所以这位大祭司,也必须有所献上的。
3Kila Kuhani Mkuu ameteuliwa kumtolea Mungu vipawa na dhabihu, na hivyo Kuhani Mkuu wetu lazima pia awe na kitu cha kutolea.
4如果他在地上,就不会作祭司,因为已经有按照律法献礼物的祭司了。
4Kama yeye angekuwa wa hapa duninani, asingekuwa kamwe kuhani, kwani wako makuhani wengine wanaotoa sadaka kufuatana na Sheria.
5这些祭司所供奉的职事,不过是天上的事物的副本和影像,就如摩西将要造会幕的时候, 神曾经警告他说:“你要留心,各样物件,都要照着在山上指示你的样式去作。”
5Huduma zao za kikuhani ni mfano tu na kivuli cha yale yaliyoko mbinguni. Ndivyo pia ilivyokuwa kwa Mose. Wakati alipokuwa karibu kuitengeneza ile hema, Mungu alimwambia: "Tengeneza kila kitu kufuatana na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani."
6但是现在耶稣得了更尊贵的职分,正好像他是更美的约的中保,这约是凭着更美的应许立的。
6Lakini sasa Yesu amepewa huduma ya kikuhani iliyo bora zaidi kuliko yao, kama vile agano alilothibitisha kati ya watu na Mungu ni bora zaidi, kwani lina msingi wake katika ahadi za mambo yaliyo bora zaidi.
7如果头一个约没有缺点,就没有寻求另一个约的必要了。
7Maana kama lile agano la kwanza halingalikuwa na dosari, hakungalikuwa na haja ya agano la pili.
8可是 神指责他们,说:“看哪,主说,日子要到了,我要与以色列家和犹大家订立新约。
8Lakini Mungu aliwalaumu watu wake aliposema: "Siku zinakuja, asema Bwana, ambapo nitafanya agano jipya na watu wa Israeli na kabila la Yuda.
9这新约不像从前我拉他们祖先的手,领他们出埃及的日子与他们所立的约。因为他们没有遵守我的约,我就不理会他们。这是主说的。
9Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao siku ile nilipowaongoza kwa mkono kutoka nchi ya Misri. Hawakuwa waaminifu kwa agano langu; na hivyo mimi sikuwajali, asema Bwana.
10主说:‘因为在那些日子以后,我要与以色列家所立的约是这样:我要把我的律法放在他们的心思里面,写在他们的心上。我要作他们的 神,他们要作我的子民。
10Na hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa Israeli siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu akilini mwao, na kuziandika mioyoni mwao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
11他们各人必不用教导自己的邻居,和自己的同胞,说:你要认识主。因为所有的人,从最小到最大的,都必认识我。
11Hakuna mtu atakayemfundisha mwananchi mwenzake, wala atakayemwambia ndugu yake: Mjue Bwana. Maana watu wote, wadogo na wakubwa, watanijua mimi.
12我也要宽恕他们的不义,决不再记着他们的罪恶。’”
12Nitawasamehe makosa yao, wala sitakumbuka tena dhambi zao."
13 神既然说到新的约,就是把前约当作旧的了;那变成陈旧衰老的,就快要消逝了。
13Kwa kusema juu ya agano jipya, Mungu alilichakaza lile la kwanza; na chochote kinachochakaa na kuwa kikuukuu kitatoweka karibuni.