1至高 神的祭司麦基洗德
1Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
2亚伯拉罕也把自己得来的一切,拿出十分之一来给他。麦基洗德这名字翻译出来,头一个意思就是“公义的王”;其次是“撒冷王”,就是“平安的王”的意思。
2naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni "Mfalme wa Uadilifu"; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya "Mfalme wa Amani.")
3他没有父亲,没有母亲,没有族谱,也没有生死的记录,而是与 神的儿子相似,永远作祭司。
3Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
4麦基洗德的祭司职分你们想一想这人是多么伟大啊!祖先亚伯拉罕也要从上等的掳物中,拿出十分之一来给了他。
4Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
5那些领受祭司职分的利未子孙,奉命按照律法向人民,就是自己的弟兄,收取十分之一;虽然他们都是出于亚伯拉罕的。
5Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
6可是那不与他们同谱系的麦基洗德,反而收纳了亚伯拉罕的十分之一,并且给这蒙受应许的人祝福。
6Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
7向来都是位分大的给位分小的祝福,这是毫无疑问的。
7Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
8在这里,收取十分之一的,都是必死的;但在那里,收纳十分之一的,却被证实是一位活着的。
8Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
9并且可以这样说,连那收取十分之一的利未,也透过亚伯拉罕缴纳了十分之一。
9Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
10因为麦基洗德迎接亚伯拉罕的时候,利未还在他祖先的身体里面。
10Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
11耶稣按麦基洗德体系作祭司这样看来,如果借着利未人的祭司制度能达到完全的地步(人民是在这制度下领受律法的),为什么还需要照着麦基洗德的体系,另外兴起一位祭司,而不照着亚伦的体系呢?
11Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
12祭司的制度既然更改了,律法也必须更改。
12Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
13因为这些话所指的那位,原是属于另外一个支派的,这支派向来没有人在祭坛前供职。
13Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
14我们的主明明是从犹大支派出来的,关于这个支派,摩西并没有提及祭司的事。
14Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
15如果有另一位像麦基洗德那样的祭司兴起来,那么,这里所说的就更明显了。
15Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
16他成了祭司,不是按着律法上肉身的条例,却是按着不能毁坏的生命的大能。
16Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
17因为有为他作证的说:“你永远作祭司,是照着麦基洗德的体系。”
17Maana Maandiko yasema: "Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki."
18一方面,从前的条例因为软弱,没有用处,就废弃了;
18Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
19(因为律法从来没有使什么得到完全,)另一方面,它却带来了更美的盼望,借着这盼望,我们就可以亲近 神。
19Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
20此外,还有关于誓言的事。其他成为祭司的,并不是用誓言立的;
20Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
21只有耶稣是用誓言立的,因为那立他的对他说:“主已经起了誓,决不改变,你永远作祭司。”
21Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: "Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele."
22耶稣既然是用誓言立的,就成了更美好的约的保证。
22Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
23一方面,从前那些作祭司的,因为受死亡的限制,不能长久留任,所以人数众多。
23Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
24另一方面,因为耶稣是永远长存的,就拥有他永不更改的祭司职位。
24Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.
25因此,那些靠着他进到 神面前的人,他都能拯救到底;因为他长远活着,为他们代求。
25Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
26这样的一位大祭司,对我们本是合适的。他是圣洁、没有邪恶、没有玷污、从罪人中分别出来、高过众天的。
26Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
27他不必像那些大祭司,天天先为自己的罪献祭,然后为人民的罪献祭;因为他献上了自己,就把这事一次而永远的成全了。
27Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
28律法所立的大祭司,都是软弱的人;可是在律法以后,用誓言所立的儿子,却是成为完全直到永远的。
28Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele.