1所以,我们应当离开基督初步的道理,努力进到成熟的地步,不必在懊悔死行,信靠 神,洗礼,按手礼,死人复活,和永远审判的教训上再立根基。
1Basi, tusonge mbele kwa yale yaliyokomaa na kuyaacha nyuma yale mafundisho ya mwanzo ya Kikristo. Hatuhitaji kuweka msingi tena kwa kurudia yale mafundisho ya mwanzo kama vile kuachana na matendo ya kifo, kumwamini Mungu;
2
2mafundisho juu ya ubatizo na kuwekewa mikono; ufufuo wa wafu na hukumu ya milele.
3只要 神允许,我们就这样作。
3tusonge mbele! Hayo tutayafanya, Mungu akitujalia.
4因为那些曾经蒙了光照,尝过属天的恩赐的滋味,与圣灵有分,
4Maana watu wanaoiasi imani yao inawezekanaje kuwarudisha watubu tena? Watu hao walikwisha kuwa katika mwanga wa Mungu, walikwisha onja zawadi ya mbinguni na kushirikishwa Roho Mtakatifu;
5并且尝过 神美善的道和来世的权能的人,
5walikwisha onja wema wa neno la Mungu na nguvu za ulimwengu ujao,
6如果偏离了正道,就不可能再使他们重新悔改了。因为他们亲自把 神的儿子再钉在十字架上,公然羞辱他。
6kisha wakaiasi imani yao! Haiwezekani kuwarudisha watubu tena, kwa sababu wanamsulubisha tena Mwana wa Mungu na kumwaibisha hadharani.
7这就像一块地,吸收了常常下在它上面的雨水,如果长出对种植的人有用的菜蔬,就从 神那里得福。
7Mungu huibariki ardhi ambayo huipokea mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuotesha mimea ya faida kwa mkulima.
8但如果这块地长出荆棘和蒺藜来,就被废弃,近于咒诅,结局就是焚烧。
8Lakini kama ardhi hiyo ikiota miti ya miiba na magugu, haina faida; karibu italaaniwa na Mungu na mwisho wake ni kuchomwa moto.
9不过,亲爱的弟兄们,我们虽然这样说,但对于你们,我们却深信你们有更好的表现,结局就是得救。
9Lakini, ingawa twasema namna hii, wapenzi wetu, tunalo tumaini kubwa juu ya hali yenu. Tunajua kwamba mmepokea baraka zile bora za wokovu wenu.
10因为 神并不是不公义,以致忘记了你们的工作,和你们为他的名所表现的爱心,就是你们以前服事圣徒,现在还是服事他们。
10Mungu hakosi haki; yeye hataisahau kazi mliyoifanya au upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake katika huduma mliyowapa na mnayowapa sasa watu wake.
11我们深愿你们各人都表现同样的热诚,一直到底,使你们的盼望可以完全实现,
11Hamu yetu ni kwamba kila mmoja wenu aonyeshe bidii hiyohiyo mpaka mwisho, ili yale mnayotumainia yapate kutimia.
12并且不要懒惰,却要效法那些凭着信心和忍耐承受应许的人。
12Msiwe wavivu, bali muwe kama wale wanaoamini na wenye uvumilivu na hivyo wanapokea yake aliyoahidi Mungu.
13 神起誓保证他的应许 神应许亚伯拉罕的时候,因为没有比自己更大的可以指着起誓,他就指着自己起誓,
13Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa jina lake mwenyewe, maana hakuna aliye mkuu kuliko Mungu ambaye kwa huyo angeweza kuapa.
14说:“我必定赐福给你,必定使你的后裔繁多。”
14Mungu alisema: "Hakika nitakubariki na nitakupa wazawa wengi."
15这样,亚伯拉罕耐心等待,终于获得了所应许的。
15Abrahamu alisubiri kwa uvumilivu na hivyo alipokea kile alichoahidiwa na Mungu.
16因为人起誓都是指着比自己大的起誓。这誓言就了结了他们中间的一切纠纷,作为保证。
16Watu wanapoapa, huapa kwa mmoja aliye mkuu zaidi kuliko wao, na kiapo hicho husuluhisha ubishi wote.
17照样, 神定意向那些承受应许的人,更清楚地表明他的旨意是不更改的,就用起誓作保证。
17Naye Mungu aliimarisha ahadi yake kwa kiapo; na kwa namna hiyo akawaonyesha wazi wale aliowaahidia kwamba hatabadili nia yake.
18这两件事是不能更改的,因为 神是决不说谎的。因此,我们这些逃进避难所的人,就大得安慰,抓紧那摆在我们面前的盼望。
18Basi, kuna vitu hivi viwili: ahadi na kiapo, ambavyo haviwezi kubadilika na wala juu ya hivyo Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hiyo sisi tuliokimbilia usalama kwake, tunapewa moyo wa kushikilia imara tumaini lililowekwa mbele yetu.
19我们有这盼望,就像灵魂的锚,又稳当又坚固,通过幔子直进到里面。
19Tunalo tumaini hilo kama nanga ya maisha yetu. Tumaini hilo ni imara na thabiti, nalo lapenya lile pazia la hekalu la mbinguni mpaka patakatifu ndani.
20耶稣已经为我们作先锋进入了幔子里面;他是照着麦基洗德的体系,成了永远的大祭司。
20Yesu ametangulia kuingia humo kwa niaba yetu, na amekuwa kuhani mkuu milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.