1耶稣临别为门徒祷告
1Yesu alipokwisha sema hayo, alitazama juu mbinguni, akasema, "Baba, saa imefika! Mtukuze Mwanao ili naye Mwana apate kukutukuza.
2正如你把管理全人类的权柄给了他,使他赐永生给你所赐给他的人。
2Maana ulimpa Mwanao mamlaka juu ya watu wote ili awape uzima wa milele wote hao uliompa.
3认识你是独一的真神,并且认识你所差来的耶稣基督,这就是永生。
3Na uzima wa milele ndio huu: kukujua wewe uliye peke yako Mungu wa kweli, na kumjua Yesu Kristo uliyemtuma.
4我在地上已经荣耀了你,你交给我要作的工,我已经完成了。
4Mimi nimekutukuza hapa duniani; nimeikamilisha ile kazi uliyonipa nifanye.
5父啊,现在让我在你自己面前得着荣耀,就是在创世以前我与你同享的荣耀。
5Sasa, Baba, nitukuze mbele yako kwa ule utukufu niliokuwa nao kabla ya kuumbwa ulimwengu.
6“你从世上分别出来赐给我的人,我已经把你的名显明给他们了。他们是你的,你把他们赐给了我,他们也遵守了你的道。
6"Nimekufanya ujulikane kwa watu wale ulionipa kutoka duniani. Walikuwa watu wako, nawe ukanipa wawe wangu; nao wamelishika neno lako.
7现在他们知道,你所给我的,无论是什么,都是从你那里来的;
7Sasa wanajua kwamba kila ulichonipa kimetoka kwako.
8因为你赐给我的话,我已经给了他们,他们也领受了,又确实知道我是从你那里来的,并且信你差了我来。
8Mimi nimewapa ule ujumbe ulionipa nao wameupokea; wanajua kwamba kweli nimetoka kwako, na wanaamini kwamba wewe ulinituma.
9我为他们求;我不为世人求,而是为你赐给我的人求,因为他们是你的。
9"Nawaombea hao; siuombei ulimwengu, ila nawaombea hao ulionipa, maana ni wako.
10我的一切都是你的,你的一切也是我的,并且我因着他们得了荣耀。
10Yote niliyo nayo ni yako, na yako ni yangu; na utukufu wangu umeonekana ndani yao.
11我不再在这世上,他们却在这世上,我要到你那里去。圣父啊,求你因你赐给我的名,保守他们,使他们合而为一,好像我们一样。
11Na sasa naja kwako; simo tena ulimwenguni, lakini wao wamo ulimwenguni. Baba Mtakatifu! Kwa nguvu ya jina lako ulilonipa, tafadhali uwaweke salama ili wawe kitu kimoja kama sisi tulivyo mmoja.
12我跟他们在一起的时候,因你赐给我的名,我保守了他们,也护卫了他们;他们中间除了那灭亡的人以外,没有一个是灭亡的,这就应验了经上的话。
12Nilipokuwa nao, mimi niliwaweka salama kwa nguvu ya jina lako ulilonipa. Mimi nimewalinda, wala hakuna hata mmoja wao aliyepotea, isipokuwa yule aliyelazimika kupotea ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia.
13现在我到你那里去,我在世上说这些话,是要他们心里充满我的喜乐。
13Basi, sasa naja kwako, na nimesema mambo haya ulimwenguni, ili waweze kushiriki kikamilifu furaha yangu.
14我把你的道赐给了他们;世人恨他们,因为他们不属于这世界,像我不属于这世界一样。
14Mimi nimewapa neno lako, nao ulimwengu ukawachukia, kwa sababu wao si wa ulimwengu kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
15我不求你使他们离开世界,只求你保守他们脱离那恶者。
15Siombi uwatoe ulimwenguni, bali naomba uwakinge na yule Mwovu.
16他们不属于这世界,像我不属于这世界一样。
16Wao si wa ulimwengu, kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
17求你用真理使他们成圣;你的道就是真理。
17Waweke wakfu kwa ukweli; neno lako ni ukweli.
18你怎样差我到世上来,我也怎样差他们到世上去。
18Kama vile ulivyonituma ulimwenguni, nami pia nimewatuma wao ulimwenguni;
19我为了他们的缘故,自己分别为圣,使他们也因着真理成圣。
19na kwa ajili yao mimi mwenyewe najiweka wakfu ili nao pia wafanywe wakfu katika ukweli.
20祈求使门徒合而为一“我不但为他们求,也为那些因他们的话而信我的人求,
20"Siwaombei hao tu, bali nawaombea pia wote watakaoamini kutokana na ujumbe wao.
21使他们都合而为一,像父你在我里面,我在你里面一样;使他们也在我们里面,让世人相信你差了我来。
21Naomba ili wote wawe kitu kimoja. Baba! Naomba wawe ndani yetu kama vile wewe ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Naomba wawe kitu kimoja kusudi ulimwengu upate kuamini kwamba wewe ulinituma.
22你赐给我的荣耀,我已经赐给了他们,使他们合而为一,像我们合而为一。
22Mimi nimewapa utukufu uleule ulionipa mimi, ili wawe kitu kimoja kama nasi tulivyo mmoja;
23我在他们里面,你在我里面,使他们完完全全合而为一,让世人知道你差了我来,并且知道你爱他们,好像爱我一样。
23mimi niwe ndani yao, nawe uwe ndani yangu; naomba wakamilishwe na kuwa kitu kimoja, ili ulimwengu upate kujua kwamba wewe ulinituma, na kwamba unawapenda wao kama unavyonipenda mimi.
24父啊,我在哪里,愿你赐给我的人也和我同在哪里,让他们看见你赐给我的荣耀,因为在创立世界以前,你已经爱我了。
24"Baba! Nataka wao ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili wauone utukufu wangu ulionipa; kwa kuwa ulinipenda kabla ya kuumbwa ulimwengu.
25公义的父啊,世人虽然不认识你,我却认识你,这些人也知道你差了我来。
25Baba Mwema! Ulimwengu haukujui, lakini mimi nakujua. Hawa nao wanajua kwamba wewe ulinituma.
26我已经把你的名指示他们,还要再指示,使你爱我的爱在他们里面,我也在他们里面。”
26Nimekufanya ujulikane kwao na nitaendelea kufanya hivyo, ili upendo ulio nao kwangu uwe ndani yao, nami niwe ndani yao."