聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

16

1“我把这些事告诉了你们,使你们不致后退。
1"Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
2人要把你们赶出会堂;并且时候要到,所有要杀害你们的人,以为这样就是事奉 神。
2Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
3他们要作这些事,因为他们不认识父,也不认识我。
3Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
4我把这些事告诉了你们,让你们到了那个时候,可以想起我告诉过你们了。我起初没有把这些事告诉你们,因为我跟你们在一起。
4Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. "Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5圣灵的工作“现在我要到那差我来的那里去,你们中间并没有人问:‘你到哪里去?’
5Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
6然而因为我把这些事告诉了你们,你们心里就充满忧愁。
6Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
7但我要把实情告诉你们,我去是对你们有益的。如果我不去,保惠师就不会到你们这里来;我若去了,就会差他到你们这里来。
7Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
8他来了,就要在罪、在义、在审判各方面指证世人的罪。
8Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
9在罪方面,是因为他们不信我;
9Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
10在义方面,是因为我到父那里去,你们就再看不见我;
10kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
11在审判方面,是因为这世界的统治者已经受了审判。
11kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
12“我还有许多事要告诉你们,可是你们现在担当不了;
12"Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
13只等真理的灵来了,他要引导你们进入一切真理。他不是凭着自己说话,而是把他听见的都说出来,并且要把将来的事告诉你们。
13Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
14他要荣耀我,因为他要把从我那里所领受的告诉你们。
14Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
15父所有的一切,都是我的;所以我说,他要把从我那里所领受的告诉你们。
15Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
16你们的忧愁要变为喜乐“不久,你们不会再看见我;再过不久,你们还要看见我。”
16"Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!"
17于是他的门徒中有几个彼此说:“他对我们说:‘不久,你们不会看见我;再过不久,你们还要看见我。’又说:‘因为我到父那里去。’这是什么意思呢?”
17Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, "Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!"
18他们又说:“他所说的‘不久’,是什么意思呢?我们不晓得他在讲什么。”
18Basi, wakawa wanaulizana, "Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini."
19耶稣知道他们想问他,就说:“我所说的‘不久,你们不会看见我;再过不久,你们还要看见我’,你们为了这话彼此议论吗?
19Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, "Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
20我实实在在告诉你们,你们要痛哭哀号,世人却要欢喜;你们要忧愁,但你们的忧愁要变为喜乐。
20Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21妇人生产的时候会有忧愁,因为她的时候到了;但生了孩子以后,就不再记住那痛苦了,因为欢喜有一个人生到世上来。
21Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
22现在你们也有忧愁;但我要再见你们,你们的心就会喜乐,你们的喜乐是没有人能够夺去的。
22Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
23到了那天,你们什么也不会问我了。我实实在在告诉你们,你们奉我的名无论向父求什么,他必定赐给你们。
23Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
24你们向来没有奉我的名求什么;现在你们祈求,就必定得着,让你们的喜乐满溢。
24Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
25耶稣已经胜过世界“我用譬喻对你们说了这些事,时候要到,我不再用譬喻对你们说了,而是把关于父的事明明白白告诉你们。
25"Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
26到了那天,你们要奉我的名祈求,我不是说我要为你们请求父;
26Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
27父自己爱你们,因为你们已经爱我,并且信我是从 神那里来的。
27maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28我从父那里来,到了这世界;我又离开这世界,到父那里去。”
28Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba."
29门徒说:“你看,现在你是明说,不是用譬喻说了。
29Basi, wanafunzi wake wakamwambia, "Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
30现在我们知道你是无所不知的,不需要人向你发问。因此,我们信你是从 神那里来的。”
30Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu."
31耶稣对他们说:“现在你们信吗?
31Yesu akawajibu, "Je, mnaamini sasa?
32看哪,时候要到,而且已经到了,你们要分散,各人到自己的地方去,只留下我独自一个人。其实我不是独自一个人,因为有父与我同在。
32Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
33我把这些事告诉你们,是要使你们在我里面有平安。在世上你们有患难,但你们放心,我已经胜了这世界。”
33Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!"