1耶稣是真葡萄树
1"Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
2所有属我而不结果子的枝子,他就剪去;所有结果子的,他就修剪干净,让它结更多的果子。
2Yeye huliondoa ndani yangu kila tawi lisilozaa matunda, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi.
3现在你们因着我对你们所讲的道,已经干净了。
3Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya ule ujumbe niliowaambieni.
4你们要住在我里面,我也就住在你们里面。枝子若不连在葡萄树上,自己就不能结果子;你们若不住在我里面,也是这样。
4Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipokaa katika mzabibu hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu.
5我是葡萄树,你们是枝子。住在我里面的,我也住在他里面,他就结出很多果子;因为离开了我,你们就不能作什么。
5"Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi yake. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo atazaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote.
6人若不住在我里面,就像枝子丢在外面枯干了,人把它们拾起来,丢在火里烧掉了。
6Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue.
7你们若住在我里面,我的话也留在你们里面;无论你们想要什么,祈求,就给你们成就。
7Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.
8这样,你们结出很多果子,我父就因此得荣耀,你们也就是我的门徒了。
8Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.
9父怎样爱我,我也怎样爱你们;你们要住在我的爱里。
9Mimi nimewapenda ninyi kama vile Baba alivyonipenda mimi. Kaeni katika pendo langu.
10如果你们遵守我的命令,就必定住在我的爱里,正像我遵守了我父的命令,住在他的爱里一样。
10Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
11“我把这些事告诉了你们,好让我的喜乐存在你们心里,并且使你们的喜乐满溢。
11Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike.
12你们要彼此相爱,像我爱你们一样,这就是我的命令。
12Hii ndiyo amri yangu: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
13人为朋友舍命,人间的爱没有比这个更大的了。
13Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
14你们若行我所吩咐你们的,就是我的朋友了。
14Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.
15我不再称你们为仆人,因为仆人不知道主人所作的事;我已经称你们为朋友了,因为我从我父那里听见的一切,都已经告诉你们了。
15Ninyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita ninyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu.
16不是你们拣选了我,而是我拣选了你们,并且分派你们去结果子,就是结常存的果子,使你们奉我的名,无论向父求什么,他必定赐给你们。
16Ninyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapa ninyi chochote mumwombacho kwa jina langu.
17我把这些事吩咐你们,是要你们彼此相爱。
17Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: pendaneni.
18世人恨主也恨门徒“如果世人恨你们,你们要知道他们在恨你们以先,已经恨我了。
18"Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.
19你们若属于这世界,世人必定爱属自己的;但因为你们不属于世界,而是我从世界中拣选了你们,所以世人就恨你们。
19Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi kama watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni.
20你们要记住我对你们说过的话:‘仆人不能大过主人。’他们若迫害我,也必定迫害你们;他们若遵守我的话,也必定遵守你们的话。
20Kumbukeni niliyowaambieni: mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia; kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia.
21但他们因着我的名,要向你们行这一切,因为他们不认识那差我来的。
21Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma.
22如果我没有来,也没有对他们讲过什么,他们就没有罪;但现在他们的罪是无可推诿的了。
22Kama nisingalikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia; lakini sasa hawawezi kujitetea kwamba hawana dhambi.
23恨我的,也恨我的父。
23Anayenichukia mimi, anamchukia na Baba yangu pia.
24如果我没有在他们中间作过别人没有作过的事,他们就没有罪;但现在我和我的父,他们都看见了,也都恨恶。
24Kama nisingalifanya kwao mambo ambayo hakuna mtu mwingine amekwisha yafanya wasingalikuwa na hatia; lakini sasa wameona niliyoyafanya wakinichukia mimi, wakamchukia na Baba yangu pia.
25这就应验了他们律法上所写的话:‘他们无故地恨我。’
25Na hivi ni lazima yatimie yale yaliyoandikwa katika Sheria yao: Wamenichukia bure!
26“我从父那里要差来给你们的保惠师,就是从父那里出来的真理的灵,他来到的时候,要为我作见证。
26"Atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi.
27你们也要作见证,因为从开始你们就是跟我在一起的。”
27Nanyi pia mtanishuhudia kwa kuwa mmekuwa nami tangu mwanzo.