聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

14

1耶稣是道路真理生命
1Yesu aliwaambia, "Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia.
2在我父的家里,有许多住的地方;如果没有,我怎么会告诉你们我去是要为你们预备地方呢?(下半节或译:“如果没有,我早就对你们说了,因为我去是为你们预备地方。”)
2Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; la sivyo ningalikwisha waambieni. Sasa nakwenda kuwatayarishieni nafasi.
3我若去为你们预备地方,就必再来接你们到我那里去,好使我在哪里,你们也在哪里。
3Na nikienda na kuwatayarishieni nafasi, nitarudi na kuwachukueni kwangu, ili nanyi muwe pale nilipo mimi.
4我去的地方,你们知道那条路。”
4Mnajua njia ya kwenda huko ninakokwenda."
5多马说:“主啊,我们不知道你去的地方,怎能知道那条路呢?”
5Thoma akamwuliza, "Bwana, hatujui unakokwenda, tutawezaje basi, kuijua hiyo njia?"
6耶稣对他说:“我就是道路、真理、生命,如果不是借着我,没有人能到父那里去。
6Yesu akamjibu, "Mimi ni njia, na ukweli na uzima. Hakuna awezaye kwenda kwa Baba ila kwa kupitia kwangu.
7如果你们认识我,就必认识我的父;从今以后,你们认识他,并且看见了他。”
7Ikiwa mnanijua mimi mnamjua na Baba yangu pia. Na tangu sasa, mnamjua, tena mmekwisha mwona."
8腓力说:“主啊,请把父显示给我们,我们就满足了。”
8Filipo akamwambia, "Bwana, tuonyeshe Baba, nasi tutatosheka."
9耶稣说:“腓力,我跟你们在一起这么久了,你还不认识我吗?那看见了我的就是看见了父,你怎么还说‘把父显示给我们’呢?
9Yesu akamwambia, "Filipo, nimekaa nanyi muda wote huu, nawe hujanijua? Aliyekwisha niona mimi amemwona Baba. Unawezaje basi, kusema: Tuonyeshe Baba?
10你不信我是在父里面,父是在我里面吗?我对你们说的话,不是凭着自己说的,而是住在我里面的父作他自己的事。
10Je, huamini kwamba mimi niko ndani ya Baba, naye Baba yuko ndani yangu? Maneno ninayowaambieni nyote siyasemi kwa mamlaka yangu; Baba aliye ndani yangu anafanya kazi yake.
11你们应当信我是在父里面,父是在我里面;不然,也要因我所作的而相信。
11Mnapaswa kuniamini ninaposema kwamba mimi niko ndani ya Baba naye Baba yuko ndani yangu. Ama sivyo, aminini kwa sababu ya mambo ninayofanya.
12我实实在在告诉你们,我所作的事,信我的人也要作,并且要作比这些更大的,因为我往父那里去。
12Kweli nawaambieni, anayeniamini atafanya mambo ninayofanya mimi; naam, atafanya hata makuu zaidi, maana nakwenda kwa Baba.
13你们奉我的名无论求什么,我必定成全,使父在子的身上得着荣耀。
13Na chochote mtakachoomba kwa jina langu nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.
14你们若奉我的名向我求什么,我必定成全。
14Mkiniomba chochote kwa jina langu, nitawafanyieni.
15耶稣求父赐下保惠师“如果你们爱我,就要遵守我的命令。
15"Mkinipenda mtazishika amri zangu.
16我要请求父,他就会赐给你们另一位保惠师,使他跟你们永远在一起。
16Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa nanyi milele.
17这保惠师就是真理的灵,世人不能接受他,因为看不见他,也不认识他。你们却认识他,因为他跟你们住在一起,也要在你们里面。
17Yeye ni Roho wa kweli. Ulimwengu hauwezi kumpokea kwa sababu hauwezi kumwona wala kumjua. Lakini ninyi mnamjua kwa sababu anabaki nanyi na yu ndani yenu.
18我不会撇下你们为孤儿,我要回到你们这里来。
18"Sitawaacha ninyi yatima; nitakuja tena kwenu.
19不久以后,世人不再看见我,你们却要看见我,因为我活着,你们也要活着。
19Bado kidogo nao ulimwengu hautaniona tena, lakini ninyi mtaniona; na kwa kuwa mimi ni hai, nanyi pia mtakuwa hai.
20到那日,你们就知道我是在我父里面,你们是在我里面,我也在你们里面。
20Siku ile itakapofika mtajua kwamba mimi niko ndani ya Baba, nanyi mko ndani yangu, nami ndani yenu.
21那领受我的命令,并且遵守的,就是爱我的;爱我的,我父必定爱他,我也要爱他,并且要亲自向他显现。”
21Azipokeaye amri zangu na kuzishika, yeye ndiye anipendaye. Naye anipendaye mimi atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake."
22犹大(不是加略人犹大)对耶稣说:“主啊,你为什么要亲自向我们显现,不向世人显现呢?”
22Yuda (si yule Iskarioti) akamwambia, "Bwana, itawezekanaje wewe kujidhihirisha kwetu na si kwa ulimwengu?"
23耶稣回答:“人若爱我,就要遵守我的话,我父必定爱他,并且我们要到他那里去,跟他住在一起。
23Yesu akamjibu, "Mtu akinipenda atashika neno langu, na Baba yangu atampenda, nasi tutakuja kwake na kukaa naye.
24不爱我的,就不会遵守我的话。你们所听见的道,不是我的,而是那差我来的父的道。
24Asiyenipenda hashiki maneno yangu. Na neno mlilosikia si langu, bali ni lake Baba aliyenituma.
25“我还跟你们在一起的时候,就对你们讲了这些事。
25"Nimewaambieni mambo haya nikiwa bado pamoja nanyi
26但保惠师,就是父因我的名要差来的圣灵,他要把一切事教导你们,也要使你们想起我对你们所说过的一切话。
26lakini Msaidizi, Roho Mtakatifu, ambaye Baba atamtuma kwa jina langu, atawafundisheni kila kitu na kuwakumbusheni yote niliyowaambieni.
27我留下平安给你们,我把自己的平安赐给你们;我给你们的,不像世界所给的。你们心里不要难过,也不要恐惧。
27"Nawaachieni amani; nawapeni amani yangu. Siwapi ninyi kama vile ulimwengu ufanyavyo. Msiwe na wasiwasi, wala msifadhaike.
28你们听见我对你们说过:‘我去,但还要回到你们这里来。’你们若爱我,就要喜乐,因为我到父那里去,又因为父是比我大的。
28Mlikwisha sikia nikiwaambieni: Ninakwenda zangu, kisha nitarudi tena kwenu. Kama mngalinipenda mngalifurahi kwa sababu ninakwenda kwa Baba, maana yeye ni mkuu kuliko mimi.
29现在事情还没有发生,我就已经告诉你们,使你们在事情发生的时候可以相信。
29Nimewaambieni haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini.
30我不会再跟你们讲很多的事,因为这世界的统治者将到;他在我身上毫无作用,
30Sitasema nanyi tena mambo mengi, maana mtawala wa ulimwengu huu anakuja. Kwangu mimi hawezi kitu;
31但这些事是要使世人知道我爱父,并且知道父怎样吩咐了我,我就怎样作。起来,我们走吧!”
31lakini ulimwengu unapaswa kujua kwamba nampenda Baba, na ndiyo maana nafanya kila kitu kama Baba alivyoniamuru. Simameni, tutoke hapa!"