聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

13

1耶稣为门徒洗脚
1Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
2吃晚饭的时候(魔鬼已经把出卖耶稣的意念放在西门的儿子加略人犹大的心里),
2Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
3耶稣知道父已经把万有交在他手中,并且知道自己从 神而来,又要回到 神那里去,
3Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
4就起身离席,脱去外衣,拿一条手巾束腰。
4Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
5然后他倒了一盆水,洗门徒的脚,并且用束腰的手巾擦干。
5Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
6轮到西门.彼得,彼得就说:“主啊,你要洗我的脚吗?”
6Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, "Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?"
7耶稣回答:“我所作的,你现在不知道,以后就会明白。”
7Yesu akamjibu, "Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye."
8彼得说:“不行,你千万不可洗我的脚!”耶稣说:“如果我不洗你的脚,你就与我没有关系了。”
8Petro akamwambia, "Wewe hutaniosha miguu kamwe!" Yesu akamjibu, "Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena."
9西门.彼得说:“主啊,那就不单洗我的脚,连我的手和头都洗吧!”
9Simoni Petro akamwambia, "Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia."
10耶稣说:“洗过澡的人,全身都洁净,只需要洗脚就可以了。你们是洁净的,但不是人人都是这样。”
10Yesu akamwambia, "Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote."
11原来耶稣知道谁要出卖他,所以他说“你们不是人人都是洁净的”。
11(Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: "Ninyi mmetakata, lakini si nyote.")
12耶稣洗完了门徒的脚,就穿上外衣,再坐下来,对他们说:“我给你们作的,你们明白吗?
12Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, "Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
13你们称呼我‘老师,主’,你们说得对,我本来就是。
13Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
14我是主,是老师,尚且洗你们的脚,你们也应当彼此洗脚。
14Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
15我作了你们的榜样,是要你们也照着我所作的去行。
15Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
16我实实在在告诉你们,仆人不能大过主人,奉差遣的也不能大过差他的人。
16Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
17你们既然知道这些事,如果去实行,就有福了。
17Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
18我这话不是指着你们全体说的;我认识我所拣选的人,但是经上的话:‘那吃我饭的,用他的脚踢我’,必须应验。
18"Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
19现在,事情还没有发生,我就告诉你们,使你们到时可以信我就是‘那一位’。
19Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
20我实实在在告诉你们,那接待我所差遣的,就是接待我;接待我的,就是接待那差我来的。”
20Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma."
21耶稣预言要被人出卖(太26:20-25;可14:17-21;路22:21-23)耶稣说了这话,心里很难过,就明明地说:“我实实在在告诉你们,你们中间有一个人要出卖我。”
21Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, "Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!"
22门徒面面相觑,不知道他是指着谁说的。
22Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
23门徒中有一个人,是耶稣所爱的,他坐在耶稣旁边。
23Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
24西门.彼得向他示意,叫他问耶稣是指着谁说的。
24Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: "Mwulize anasema juu ya nani."
25于是那个门徒贴近耶稣的胸怀,问他:“主啊,是谁呢?”
25Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, "Bwana, ni nani?"
26耶稣回答:“我蘸一小块饼给谁,谁就是了。”于是他蘸了一小块饼,递给加略人西门的儿子犹大。
26Yesu akajibu, "Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye." Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
27犹大接过饼以后,撒但就进入他的心。耶稣对他说:“你要作的,快去作吧。”
27Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, "Unachotaka kufanya, kifanye haraka!"
28在座的人,没有一个知道耶稣为什么对犹大说这话。
28Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
29犹大是管钱的,所以有人以为耶稣叫他去买过节用的东西,或是吩咐他拿点东西去赒济穷人。
29Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
30犹大吃了饼,立刻就出去;那时是黑夜了。
30Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
31吩咐门徒要彼此相爱他出去以后,耶稣就说:“现在人子得了荣耀, 神也在人子身上得了荣耀,
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, "Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
32( 神既然在人子身上得了荣耀,)(有些抄本无此句)也要在自己身上荣耀人子,并且要立刻荣耀他。
32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
33孩子们啊,我跟你们在一起的时候不多了。你们要寻找我,但是我对犹太人说过,现在也照样对你们说:‘我去的地方,是你们不能去的。’
33"Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
34我给你们一条新命令,就是要你们彼此相爱;我怎样爱你们,你们也要怎样彼此相爱。
34Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
35如果你们彼此相爱,众人就会认出你们是我的门徒了。”
35Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu."
36预言彼得不认主(太26:33-35;可14:29-31;路22:33-34)西门.彼得对耶稣说:“主啊,你往哪里去?”耶稣回答:“我去的地方,你现在不能跟着我去,但后来却要跟着我去。”
36Simoni Petro akamwuliza, "Bwana, unakwenda wapi?" Yesu akajibu, "Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye."
37彼得说:“主啊,为什么我现在不能跟着你去?为了你,我舍命也愿意!”
37Petro akamwambia "Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!"
38耶稣说:“你愿意为我舍命吗?我实实在在告诉你,鸡叫之前,你必定三次不认我。”
38Yesu akajibu, "Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!"